Washington, USA: Mahakama yaitupilia mbali rufaa ya familia ya Valambhia dhidi ya Tanzania

Washington, USA: Mahakama yaitupilia mbali rufaa ya familia ya Valambhia dhidi ya Tanzania

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
1618917681054.png

Mjane na Watoto wa Vdevram Purshotam Valambhia waliishtaki Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani.

Walitaka kulipwa dola 64,500,750 kutokana na Mkataba wa ununuzi wa vifaa vya kijeshi kati ya Kampuni ya Transport Equipment Ltd (TEL) ya Marehemu Valambhia na Serikali ya Tanzania ulioingiwa miaka ya 1980.

Kampuni ya TEL ilidai haijakamilishiwa malipo yote ya fedha zitokanazo na Mkataba. Kampuni hiyo iliamua kufungua Kesi Na. 210 ya mwaka 1989 iliyotolewa uamuzi na Mahakama za Tanzania.

Katika harakati za kudai malipo walikata rufaa katika Mahakama Kuu ya Washngton DC, na uamuzi uliotolewa na mahakama hiyo Aprili 19, 2021 umeonesha kukataliwa kwa madai yao.
==
 
Kwanini wasifungulie shitaka leo hapa Bongoland?
 
Ukisikia kuipambania nchi, ndio huko, Asanteni Sana Wanasheria waungwana, Naomba mh Raisi wetu awape japo tuzo ya heshima!

Nchi sasa itaheshimiwa hata na mataifa ya kinyonyaji

Kuipambania nchi, si kuichongea na kuitishia kushitakiwa MIGA na kuiombea mabaya kila leo,
 
Ingekuwa enzi zile tungejifanyisha kushindwa watu wagawane hizo fedha. CAG kashatishia uwezekano wa ndege za ATCL kukamatwa.

Hatushangai watu kumpiga vita mwanasheria mkuu wa serikali ya JMT. Mcha Mungu huyu hawezi kukubali kushindwa kesi ili akagawiwe pato la dhuluma.
 
Ingekuwa enzi zile tungejifanyisha kushindwa watu wagawane hizo fedha. CAG kashatishia uwezekano wa ndege za ATCL kukamatwa.

Hatushangai watu kumpiga vita mwanasheria mkuu wa serikali ya JMT. Mcha Mungu huyu hawezi kukubali kushindwa kesi ili akagawiwe pato la dhuluma.

..ulaji uko kwenye makampuni ya wanasheria wanaokodiwa na serikali ya Tz kututetea huko ktk mahakama za mabeberu.

..pia kesi hii ni ya muda mrefu sana. Kama unavyoona chanzo chake ni manunuzi ya silaha yaliyofanyika miaka ya 1980. Na kwa mara ya kwanza kesi iliamuliwa hapa Tz mwaka 1989.
 
Kwanini wasifungulie shitaka leo hapa Bongoland?

..hii kesi imeshakwenda mpaka mahakama ya rufaa ya hapa Tz na serikali ilishindwa.

..walalamikaji wamepeleka shauri nje kwasababu serikali imekataa kuwalipa.

..soma hapa chini taarifa zinaonyesha kwamba serikali ilishindwa ktk mahakama za hapa Tz.

" In 1991, the High Court of Tanzania entered a High Court Decree which stated that Valambhia and his family were entitled to 45% of the amount unpaid on the contract between Tanzania and TEL. In 2001, after roughly a decade of further litigation, the High Court of Tanzania entered a Garnishee Order that required the Bank of Tanzania to pay Valambhia the amount owed under the High Court Decree. The Bank challenged the validity of the Garnishee Order, but the High Court found it to be proper. The Bank then appealed this ruling in the Court of Appeal of Tanzania. In 2003, the Court of Appeal held that the Garnishee Order was “final and conclusive” and denied the Bank any right to appeal. "
 
Habari mbaya kwa Tundu na Chadema...huu uzi umewakera sana.
Kweli sisi Watanzania ni watu wa kipekee hapa duniani.Hata masuala ya kesi za kisheria tunaingiza uvyama vya siasa?Sifahamu umekigusisha CHADEMA na Lissu kwa misingi gani kwenye Uzi huu!Ila ni aibu kufanya siasa za kichovu katika issues za kitaifa.
Siamini kama Wakili Msomi kama Mh.Lissu anafurahia Tanzania inavyoshtakiwa shtakiwa kwa uzembe wa watawala arrogant tuliokuwa nao tangia enzi za Tanganyika,wanaingia mikataba ya hovyo kwa niaba ya nchi na hawawezi kutimiza hizo terms kwa tamaa zao ndipo zinazaliwa kesi za ajabu ajabu.Ulikuwepo wakati Bombardier ilipozuiliwa Canada?Watawala arrogant wakataka kuficha issue waimalize kimya kimya.Unafamfahamu aliyewaambia Watanzania kuwa ndege yetu imekamatwa? Nadhani sasa Unafahamu jibu la kwa nini Mh.Lissu hafurahii Tanzania kushtakiwa Ama kuchukia Tanzania ikishinda kesi,mashindano nk.Jiongeze.
 
Duh unateseka sana
..ulaji uko kwenye makampuni ya wanasheria wanaokodiwa na serikali ya Tz kututetea huko ktk mahakama za mabeberu.

..pia kesi hii ni ya muda mrefu sana. Kama unavyoona chanzo chake ni manunuzi ya silaha yaliyofanyika miaka ya 1980. Na kwa mara ya kwanza kesi iliamuliwa hapa Tz mwaka 1989.
 
Back
Top Bottom