Washington, USA: Mahakama yaitupilia mbali rufaa ya familia ya Valambhia dhidi ya Tanzania

Duh unateseka sana

..Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ilishaamua kwamba huyo supplier wa silaha alipwe.

..Sasa jiulize kwanini huyu supplier amekwenda kushitaki nje ya nchi wakati alishinda kesi hapa Tanzania?

..Je, serikali yetu imegoma kuheshimu maamuzi ya mahakama ya Rufaa ya Tanzania?
 
Kwahiyo unataka alipwe?dogo acha hizo
 
Kwa uhusika uleule uliyomfanya akasemaga tutashitakiwa.

..tulishtakiwa.

..na ndio maana serikali ikaachana na madai ya usd 191 billion dhidi ya accacia.

..na makinikia bado yanasafirishwa kwenda nje.
 
Kwa uhusika uleule uliyomfanya akasemaga tutashitakiwa.
Hujitambui bado. Soma bandiko Tena. Au hii kesi serikali ilishitaki au ilishitakiwa? Mataga mna kazi ngumu Sana hasa msimu huu usiohitaji mapambio yenu! Tafuteni mbinu nyingine ya kumshangilia vinginevyo mnakwenda kupotea kabisa kwenye siasa za msimu huu!
 
Lisu na wenzie pale bungeni ndo walioanzisha siasa za ajabu za kutojali maslahi ya Taifa hasa pale alipoitishia serikali kwamba ingeshitakiwa na MIGA kisa Serikali kuvunja mikataba ya kinyonyaji,Cdm walihusika kumsupport yule mkimbizi hewa
 
Lisu na wenzie pale bungeni ndo walioanzisha siasa za ajabu za kutojali maslahi ya Taifa hasa pale alipoitishia serikali kwamba ingeshitakiwa na MIGA kisa Serikali kuvunja mikataba ya kinyonyaji,Cdm walihusika kumsupport yule mkimbizi hewa
Halafu hiyo MIGA ni taasisi tu ya World Bank ambayo jukumu lake ni kutoa guarantee kwa wawekezaji katika nchi zinazoendelea, lisu alituingiza chaka na stori zake za kushitakiwa miga.
 
Nisome tena nini wakati nilichokiandika hujakielewa. Maadamu chama bado kinaendelea kinaongoza hakuna kilichoharibika sijui wewe.
 
Lisu na wenzie pale bungeni ndo walioanzisha siasa za ajabu za kutojali maslahi ya Taifa hasa pale alipoitishia serikali kwamba ingeshitakiwa na MIGA kisa Serikali kuvunja mikataba ya kinyonyaji,Cdm walihusika kumsupport yule mkimbizi hewa

..siyo kweli.

..Lissu ni kati ya Watz wa kwanza kabisa kupaza sauti kwamba mikataba ya madini ni mibaya.

..Na hakuna wakati Lissu ametetea makampuni ya madini na unyonyaji wao hapa nchini.

..Alichokisema Lissu, na ambacho kinapotoshwa, ni kwamba ripoti za uchunguzi zilikuwa za kizushi na zenye kulidhalilisha taifa.

..Alitutahadharisha kwamba tuking'ang'ania madai ya usd 191 billion tutashitakiwa na tutashindwa kesi hiyo.

..Alichokisema Lissu ndicho kilichotokea kwasababu zifuatazo :-

1. Hatujalipwa usd 191 billion.
2. Accacia waliishitaki serikali, na waliondoa kesi yao baada ya Barrick kufika bei na kuwanunua.
3. Makinikia yanasafirishwa kuchenjuliwa nje ya nchi.
5. Tumesaini mikataba inayoruhusu Barrick kutushitaki ktk mahakama za nje ya nchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…