Wasichana wa kazi wa ndani

Nikishaona mtu anachanganya kingereza na kiswahili, uandishi flan wa kupalilia penzi na dogo wa kidato Cha pili hua inanikata vibe ya kusoma

Ila kwa mada Yako ni ngumu sana kukomboa jamii yenye umaskini wa kutisha ni ngumu sana
 
Dah... Umeandika lugha gani!??
 
Watu wenyewe tunaowaajiri hao wadada unga unga mwana , huo mshahara wa laki mbili tunatoa wapi. Cha msingi wasiteswe tuishi nao kama sehemu ya familia zetu.
Dah huu Uzi ni mzuri lkn nimesoma mpk nmechoka wahindi umewai fanya kazi nao ww utaomba uondoke
 
Mbona vingereza sasa ni kwamba ueleweke na wachache au nini lengo lako,simamia lugha moja kasuku wewe
 
Mawazo chanya lakini boss wake mwenyewe mwisho wa mwezi anachukua laki tatu ... Alafu yeye anakaa na kulala bure achukue laki mbili kwenye tatu ya boss wake ??
 
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] Jf nakupenda kwa moyo wote maan nikiingia humu napata raha [emoji23][emoji23]
Jamaa mpuuzi sana maisha yenyewe magumu yeye anatuandikia vingereza vyake na kiswahili mara Dad mara nini kanikera sana
 
Mbona huko huko umeenda mbali sana.Kwanini usiwaangazie maisha ya walinzi wa usiku,wale wanaolinda ATMs imejaa hela lafu mshahara wake anatake home ya 150k(all inclusive).wale wanaolinda magodown ili akija jambazi kuiba ama amue au auliwe yeye.

Huyu msaidizi wa Nyumbani mshahara ukichelewa ana uhakika wa kula,kulala.Ila siyo huyu wa day.unajua mtu analipwa sh.150k halafu akitoa nauli ya kwenda kazini na kurudi,kula,kodi ababaki na negative salary inayokuwa financed na duka la mangi

point yako kubwa hapo ni kwamba kama una nafasi muwezeshe.Pili tuwaheshimu hawa watu kama watoto wetu kwa sababu msaada wao ni mkubwa sana

Unajua take
 
Mwandiko mbaya .....
Point hakuna .....
 
Wewe utafanya wakose hata hizo 50k sababu hakuna Mtanzania mwenye uwezo wa kumpa mtu anayepika, kufua, kufagia na kuosha vyombo 200k kwa mwezi ukichangia anakula na kupata huduma nyingine hapohapo.

Well, unless kuna kazi nyingine ambayo haijaorodheshwa. Otherwise sahau.
 
Mshahara elfu 50 ,kula kulala kwa tajiri .Hapo hatujahebu milo yake mitatu kwa siku,sabani ya kuoga na kufulia,matibabu akiugua gharama zote tajiri.
Elfu 50 +gharama zote inazidi huo mshahara.
Mtoa mada umengalia mshahara tu hukufikiria gharama nyingine anazotoa tajiri.
 
Watanzania bwana na akili zao; so nipochanganya ngeli hapo hujaelewa Au ndo kuwashwa tu? Basi ungekuwa hujaelewa usingekuwa unapiga kelele ungepita pembeni tu km umeona kichina🤣🤣🤣
Mbona vingereza sasa ni kwamba ueleweke na wachache au nini lengo lako,simamia lugha moja kasuku wewe
 
Narudia basi fanya kazi mwenyewe km huna uwezo wa kulipa watu mbona simple
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…