Hili tatizo ni la pande zote, anayevuliwa na ayemvua mwenzake wote ni wale wale
Unajua haya maisha ya kijamii huwezi toa sababu moja tu kuleta athari ni mkusanyiko wa kila kitu
Suluhisho naweza kuligawa katika ngazi 3
Kwanza kama jamii ya kitanzania, values zetu ni zipi
Kipi tunaona ni aibu kikifanyika kwa maneno na matendo
Nikisema kwa maneno na matendo namaanisha ishi unachohubiri sio kuhubiri A afu unafanya B
Ngazi ya familia, values gani tunarithisha kwa vizazi vyetu.
Sijui kwa nini huwa naipa familia nafasi kubwa sana ya kujenga values na morals kwa mtu
Lakini naamini mchando wa institution hii ni mkubwa.
Kuna ngazi ya Individual, kuwa responsibl;e na maisha yakop
Na kuweza kuwa mtu wa kiasi, kuweza fanya maamuzi ya kipi kina kipaumbele kwako
Kuna wengine wanapata degree ya kyupi si kwamba hawana uwez wa kufaulu ila wanataka sifa ya kuwa alipata 1st class aliki ana uwezo kwa kupata upper 2nd class
Afu, swali lako umeniuliza kama mtangazaji wa CNN:lol:
Tukirejea kwenye mfano wa The Bawse kuhusu yule mama ambaye aliona ni haki kwa mwanae kuuwawa na polisi, swali tu linakuja maybe ambalo sijui kama lilijibiwa kwenye movie hiyo ya kihindi, ni kuhusiana na hizo chapati ambazo huyo mama alikuwa akizila kabla ya mauti hayajamkuta mwanae.
Ina maana pia, kutokana na shida na njaa ya mama yule, basi hakuweza kuzigomea chapati za wizi despite the fact kuwa she had a knowledge of what went on kuhusiana na wizi wa kijana wake.
Kwenye jamii yetu, ni the same kwenye ngazi zote, fisadi ndo anayepewa respect na hata nyadhifa nk.
Kuna familia nying sana zinaendeshwa kwa wizi, yani ndugu ni wezi na ndiyo wanategemewa na famila, sometimes jamii.
Watu wanajuwa kabisa hizi pesa huyu kakwiba, lakini utamu wake unawasahaulisha hayo yote, na level za wananchi wengi bongo ni za chini sana, couple with other divisive issue that have impacted the general society psychologically, things like rice, pilao and some booze can buy you some heads!
Level ya awareness kwenye jamii ambayo itatufanya tuone haya yote n mabaya, hatutoweza kufikia huko kama hatupigi hatua za kiuchumi kwenye taifa letu.
Sasa kwamfano kisaikolojia watanzania wako confused, wanajuwa kabisa kuwa serikali ni masikini mwenye silaha lakini, na polisi nk., wanajuwa kabisa kuwa serikali ni masikini ndo maana tunapata msaada kutoka mataifa ya magharibi na kwingineko, na kwahiyo somewhere kwenye ubongo wao wana harbor sympathysing feelings towards the govt, na wakiona kuwa wanaambiwa amani ipo, pamoja na hizo rushwa za hapa na pale, basi wanaona kama serikali inajtahidi sana.
Hawajui kwamba wanachofahamu kuhusu serikali ni just a tip of an iceberg, pia hawajui kama tuna uwezo pia wa kuwa matajiri.
Vita hivyo hivyo vya kisakolojia, hata wale wanaoamini kuwa we need massive changes kwenye jamii yetu kama tunataka mabadilko, bado wamegawanyika, either kwa misingi ya kidini, ama uhafidhina wa vyama vyao vya kisiasa.
Ni kitu gani kina tu unify kama taifa zaidi ya jina la nchi na mipaka yake?ni kiswahili? If so kimetusaidia vipi kuondokana na hizi adha zinazotukabili?
Ni hadi pale tunapoweza kuwa na issue zinazotuunganisha kiukweli kama taifa, basi hatutajuwa pa kuanzia.