Wasichokijua Wengi Kuhusu Marko 10: 25 katika Biblia

Wasichokijua Wengi Kuhusu Marko 10: 25 katika Biblia

Hashpower7113

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
1,353
Reaction score
2,142
Katika kitabu kitakatifu cha Biblia, Marko 10: 25 inasema: Ni rahisi ngamia kupenya katika tundu ya sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.

Wanachokielewa wengi, wakiwemo baadhi ya watumishi wa Mungu, ni kwamba ngamia anayezungumziwa hapa ni yule mnyama mwenye nundu kubwa mgongoni, pengine hata wewe kwa miaka mingi umekuwa ukijua hivyo.

Hata hivyo, ngamia iliyomaanishwa hapa, ni kamba! Ndiyo, kamba! Zile kamba nene zinazotumika kuvuta kwa mfano meli iliyozama na kadhalika. Makosa ya tafsiri hii yanaanzia kwenye kufasiri kifungu hiki cha Biblia kutoka kwenye Kiingereza kuja kwenye Kiswahili. Kwa Kiingereza, Mark 10:25 inasomeka hivi: It is easier for a camel to go through the eye of a needle than for a rich person to enter the kingdom of God.

Ukichukua kamusi yako, angalia maana ya neno camel, ya kwanza utaona ni ngamia mnyama lakini kuna maana ya pili ambayo ni hii: Camel: An apparatus for raising a sunken ship, consisting of one or more watertight chests to provide buoyancy. Kwa tafsiri nyepesi, ni kamba nene zinazotumika kuvuta meli iliyozama...

Kwa commoni sense ya kawaida tu, ngamia mnyama anawezaje kufananishwa na kupenya kwenye tundu la sindano? Hakuna uhusiano wowote, lakini kuna uhusiano wa kamba nene kupenya kwenye tundu la sindano kwa sababu kamba nyembamba (uzi) unapenya kirahisi!

Kwa hiyo tunahitimisha kwa kusema, ngamia/camel inayomaanishwa kwenye bible ni kamba. I stand to be corrected!

passing-a-camel-through-the-eye-of-a-needle-heavy-rope-on-dark-wooden-background-RGE0NF.jpg
 
Embu wataalam wengne wa teolojia watupe maana Yao apa, I'm real confused
Usiwe confused mkuu! Ni rahisi tu, neno camel la Kiingereza, limetokana na neno camelum la Kilatini, sasa ukiangalia maana ya camel ya Kiingereza, si ngamia mnyama pekee, kuna maana nyingine ya pili ambayo ndiyo hiyo ya kamba!
 
Ndio hivyo mkuu, ni kamba. Shida imekuja kwa miaka ya karibuni kuibuka 'Viongozi wa dini' wasiopitia chuo cha theolojia kazi kubwabwaja tu kuhusu miujiza na mafanikio!
Kweli mkuu, siku hizi viongozi wa dini wengi hawajasomea theolojia! Ukishajua kukemea pepo tu basi tayari mchungaji
 
Mkuu, yawezekana "tundu la sindano" ikawa ni metaphor tu ikimaanisha lango dogo katika mji wa Yerusalemu.
Kwamba malango mengine makubwa ktk mji huu yalifungwa wakati wa usiku na hili lango dogo lilifunguliwa kwa sababu za kiusalama na wale waliochekewa kuingia maskani walipia mlango huu.
Aidha wanyama kama ngamia kunako late hours walipitishwa ktk mlango mdogo lakini kwa kupunguziwa mzigo waliobeba na kuwa push kwa nguvu ili wapite pale. Iliwezekana ngamia kupita ktk mlango mdogo (tundu la sindano).
Hapa maneno 'tundu la sindano' yametumika kama hyperbole.
 
Mkuu, yawezekana "tundu la sindano" ikawa ni metaphor tu ikimaanisha lango dogo katika mji wa Yerusalemu.
Kwamba malango mengine makubwa ktk mji huu yalifungwa wakati wa usiku na hili lango dogo lilifunguliwa kwa sababu za kiusalama na wale waliochekewa kuingia maskani walipia mlango huu.
Aidha wanyama kama ngamia kunako late hours walipitishwa ktk mlango mdogo lakini kwa kupunguziwa mzigo waliobeba na kuwa push kwa nguvu ili wapite pale. Iliwezekana ngamia kupita ktk mlango mdogo (tundu la sindano).
Hapa maneno 'tundu la sindano' yametumika kama hyperbole.
Sasa mkuu ukiangalia tafsiri yako hii ambapo tuna-assume tundu la sindano ni metaphor (hatuwezi kuthibitisha) ambayo maana yake ni mlango mdogo, ukiangalia na tafsiri niliyoitoa pale juu, unadhani ipi ina make sense zaidi?
 
Nilishawahi kuwafundisha wanafunzi wangu kuhusu hili suala, lakini twende sawa hapa.

Ile kamba inaitwa NGAMIA na Yule mnyama nae anaitwa NGAMIA. Kwa Lugha ya Kiswahili, nikaja kubadili mtazamo siku nimesoma na version ya kiingereza, nikakuta imeandikwa CAMEL. Je, Camel nayo ina maanisha kamba?

[emoji3166]
 
Nilishawahi kuwafundisha wanafunzi wangu kuhusu hili suala, lakini twende sawa hapa.

Ile kamba inaitwa NGAMIA na Yule mnyama nae anaitwa NGAMIA. Kwa Lugha ya Kiswahili, nikaja kubadili mtazamo siku nimesoma na version ya kiingereza, nikakuta imeandikwa CAMEL. Je, Camel nayo ina maanisha kamba?

[emoji3166]
Ndiyo mkuu, Camel ina maana zaidi ya moja kwa Kiingereza, ngamia mnyama na maana ya pili ni kamba, prove mwenyewe utaona!
 
Back
Top Bottom