Wasifu wa Rais Samia Suluhu Hassan

Wasifu wa Rais Samia Suluhu Hassan

Nilikuwa napekua makabrasha nikakumbana na kijihabari kwamba Samia alikuwa sekretari wa NGO.

Kiukweli nilifadhaika. Sikutarajia kama angeweza kuwa na kisomo cha hadhi ya NGO.

Na hapa sitaki kubeza. Wala sina lengo la kutweza. Nataka kuondosha mashaka yangu.

Binafsi sijawahi kuona CV ya samia. Nimefukua kila mahali lakini sijaipata.

Naamini baadhi yenu mna CV yake humu. Lakini sijui kwanini mmeificha?

Kuna wanawake wa shoka wako CCM wana CV zina ujazo kweli kweli — Kama Asha Rose Migiro.

Ukizisoma mpaka unatoka udenda wa hamasa.

Lakini hii CV ya samia sijui wameifukia kwenye shimo gani. Hata uitafute vipi huipati.

Hivi ni kweli alikuwa sekretari wa NGO?
Nashauri asigombee.

Yeyote atakaehusika kuhujumu upatikanaji wa KATIBA mpya itokanayo na Rasimu ya Judge Warioba ndo adui no moja wa Watanzania.

Amen.
 
Hamuwezi kuamini ila mi nishawahi kumpiga biti huyu madam president. Ila ndio maisha
 
Sheria zetu zinakataza ajira kwa watoto chini ya miaka kumi na nne (14-).

Watoto wanaoanzia miaka kumi na nne (14+) wanaruhusiwa kuajiriwa kwa sharti kuwa ajira hizo zisihusishe kazi ngumu zitakazohatarisha ustawi wa mtoto, Samia aliajiriwa kuwa Karani.

Kazi kama za Migodini, Ubaharia melini, Kilimo na Viwandani ni hatarishi kwa watoto chini ya miaka kumi na nane (18) hivyo ni kinyume cha sheria.

Ila sheria imeacha mwanya kwa Wizara kutoa rukhsa maalum kwa watoto kuwepo maeneo hayo ikiwa ni kwa kusudi la Mafunzo, na Mafunzo hayo ni lazima yazingatie usalama wa mtoto.
Huku mtaani Kuna wauza mitumba waliomaliza degree.

Hawana ajira wengine miaka 20 imepita.

Yaani ktk Nchi yangu mtu anaweza ajiriwa kwanza ndo aende kutafuta ELIMU na qualification baada ya kuajiriwa tena wizarani?
 
Mwaka gani na mwaka gani?

Shule za msingi alisoma miaka ya 1960s mpaka mwaka 1972 akihama ktk shule hizo tajwa.

Mwaka 1973-77 alisoma shule ya upili Ngambo na Lumumba sekondari.


Shule ya Ngambo?

Naam, ilikuwa ikifahamika Ng’ambo na sasa Lumumba sekondari.


Alama zake za ufaulu zilikuwaje?

Si rahisi kujua.

Baada ya kidato cha nne akaenda chuo cha utawala wa fedha? Elimu ya ngazi gani? Na umesema alifeli mitihani?

Bila shaka ngazi ya Cheti.

Nimesema “matokeo hayakuwa mazuri”.

Aliajiriwa akiwa na umri wa mtoto? (underage)?

Sheria zetu zinakataza ajira kwa watoto chini ya miaka kumi na nne (14-).

Watoto wanaoanzia miaka kumi na nne (14+) wanaruhusiwa kuajiriwa kwa sharti kuwa ajira hizo zisihusishe kazi ngumu zitakazohatarisha ustawi wa mtoto, Samia aliajiriwa kuwa Karani.

Kazi kama za Migodini, Ubaharia melini, Kilimo na Viwandani ni hatarishi kwa watoto chini ya miaka kumi na nane (18) hivyo ni kinyume cha sheria.

Ila sheria imeacha mwanya kwa Wizara kutoa rukhsa maalum kwa watoto kuwepo maeneo hayo ikiwa ni kwa kusudi la Mafunzo, na Mafunzo hayo ni lazima yazingatie usalama wa mtoto.
 
Huku mtaani Kuna wauza mitumba waliomaliza degree.

Hawana ajira wengine miaka 20 imepita.

Yaani ktk Nchi yangu mtu anaweza ajiriwa kwanza ndo aende kutafuta ELIMU na qualification baada ya kuajiriwa tena wizarani?

Umakini unahitajika ktk kuoanisha suala la Samia aliyeajiriwa miaka ya 70s ambako hapakuwa na wasomi wengi na sasa ambapo tuna wasomi wengi.
 
Mama aongezewe kumi mingine eeeenh bwana ukimparura atatuparura tuuu
 
Nilikuwa napekua makabrasha nikakumbana na kijihabari kwamba Samia alikuwa sekretari wa NGO.

Kiukweli nilifadhaika. Sikutarajia kama angeweza kuwa na kisomo cha hadhi ya NGO.

Na hapa sitaki kubeza. Wala sina lengo la kutweza. Nataka kuondosha mashaka yangu.

Binafsi sijawahi kuona CV ya samia. Nimefukua kila mahali lakini sijaipata.

Naamini baadhi yenu mna CV yake humu. Lakini sijui kwanini mmeificha?

Kuna wanawake wa shoka wako CCM wana CV zina ujazo kweli kweli — Kama Asha Rose Migiro.

Ukizisoma mpaka unatoka udenda wa hamasa.

Lakini hii CV ya samia sijui wameifukia kwenye shimo gani. Hata uitafute vipi huipati.

Hivi ni kweli alikuwa sekretari wa NGO?
Nani asiyejuwa cv ya Prof. Tibaijuka ilivyosheheni lakini c tuliona alivyopokea mamilioni ya iptl bila aibu mpaka ikabidi alazimishwe kujiuzulu kwa hivyo ndugu yangu hayo ma cv mkubwa hayana maana yoyote katika uongozi ni wizi tu elimu ya kiasi na uadilifu ndio muhimu.
 
Umakini unajitajika ktk kuoanisha suala la Samia aliyeaniriwa miaka ya 70s ambako hapakuwa na wasomi wengi na sasa ambapo tuna wasomi wengi.
Elimu inayohitajika ni angalau Degree 1 au 2 kwenda PhD na mbele ni ishu za Academic tu. Hazina impact yoyote kwenye utawala. MAGUFULI alikuwa na PhD lkn alikuwa hovyo kabisa compare to Samia.

Samia amepiga shule, amefanya kazi na mashirika makubwa ya kimataifa, ameishi nje, amesoma nje zaidi ya miaka 5 nk.

Hoja yako ni ya kijinga na haina mashiko.
 
Mnauliza CV ya Mkuu wa Nchi, lengo lenu lipi hasa? Mnataka kuipindua nchi? Kwani Royo Tuwa hamjaiona? Watalii wamejaa Serengeti mpaka tumeamua kuwaondoa Wamaasai ili kuzipisha pesa ziingie hazinani. Alaaa!
 
Nani asiyejuwa cv ya Prof. Tibaijuka ilivyosheheni lakini c tuliona alivyopokea mamilioni ya iptl bila aibu mpaka ikabidi alazimishwe kujiuzulu kwa hivyo ndugu yangu hayo ma cv mkubwa hayana maana yoyote katika uongozi ni wizi tu elimu ya kiasi na uadilifu ndio muhimu.
Hoja dhaifu.

Wasomi wenye uadilifu wamekosekana Hadi tupuuze qualification ktk nafasi nyeti?

Mbona wamejaa kitaa? Juzi wametangaza ajira watendaji Serikali za mitaa nafasi 8,

wakajitokeza Kwa interview waombaj wenye vyeti Zaid ya 1000, nkasema tumetunza bomu.
 
Lakini hii CV ya samia sijui wameifukia kwenye shimo gani. Hata uitafute vipi huipati.
Nadhani hujui tu namna ya kutafuta taarifa. Hata hapa JF kitu kinachofanana na hicho unachotafuta kilishawekwa. Pekuwa vizuri utaona. Naamini kila kiingiacho JF huwa hakifutiki.

Huyo aliwahi kuwa mbunge/Mwakilishi. Anzia huko.

Niliwahi kuiona, hiyo niliyoona siwezi kuiita CV.

Lakini niseme tu hapa, CCM imeidhalilisha sana nchi yetu kwa kuokoteza kila anayekuwa Mwenzao kuwa kwenye uongozi bila kujali anao uwezo wa kuongoza au la.

Lakini ni lazima nieleweke, sisemi kisomo kizito ndiyo silaha ya uongozi, la hasha, lakini ni sehemu muhimu kwa kiongozi yeyote.
Samia hana kisomo cha kumsaidia ili kuziba penye upungufu wa uongozi alionao.
 
Nilikuwa napekua makabrasha nikakumbana na kijihabari kwamba Samia alikuwa sekretari wa NGO.

Kiukweli nilifadhaika. Sikutarajia kama angeweza kuwa na kisomo cha hadhi ya NGO.

Na hapa sitaki kubeza. Wala sina lengo la kutweza. Nataka kuondosha mashaka yangu.

Binafsi sijawahi kuona CV ya Samia. Nimefukua kila mahali lakini sijaipata.

Naamini baadhi yenu mna CV yake humu. Lakini sijui kwanini mmeificha?

Kuna wanawake wa shoka wako CCM wana CV zina ujazo kweli kweli — Kama Asha Rose Migiro.

Ukizisoma mpaka unatoka udenda wa hamasa.

Lakini hii CV ya Samia sijui wameifukia kwenye shimo gani. Hata uitafute vipi huipati.

Hivi ni kweli alikuwa sekretari wa NGO?
Ni kweli 100% Mkuu.
 
Back
Top Bottom