Wasimamizi wa mirathi ya Mengi wagoma kuhudumia watoto, waburuzwa mahakamani

Wasimamizi wa mirathi ya Mengi wagoma kuhudumia watoto, waburuzwa mahakamani

huyo dada anashindwaje yeye kuwalea watoto wake...Yeye si amebaki na mikono, miguu, macho na ule uzuri wake aendelee tu kulea watoto vizuri kama alivyokuwepo baba yao, Huo ndio utakuwa upendo otherwise hata kwa baba yao alifuata mali tu..
Utakuta aliye leta hii mada hapa ni huyo huyo mwanamke mwenyewe mwenye tamaa na mali ambazo hakuzitolea jasho yeye, hawa wadada wa sasa ni tatizo sana
 
Mirathi ya marehemu Dkt Mengi imezua balaa baada wasimamizi wake kuburuzwa mahakamani kwa tuhuma za kukataa kuwahudumia watoto wa Mengi aliozaa na Jacqueline Ntuyabaliwe.

Kesi hii imefunguliwa ikiwa mke huyo mdogo wa Mengi akiwa amezuiwa kukanyaga Kilimanjaro hata kwenda kusafisha kaburi la marehemu mme wake.

Kuna kila dalili hao watoto mapacha wa billionea Mengi wakaishi maisha ya dhiki na umasikini uliotopea ili hali baba yao amewaachia mali nyingi sana ikiwemo kampuni ya IPP Media, yote hayo yatasababishwa na tamaa za mali za ndugu na watoto wa mke mkubwa wa Dkt Mengi.

Source. Gazeti la mwananchi.

=====

Wasiamamizi wa mirathi ya aliyekuwa mfanyabiashara maarufu nchini Reginald Mengi wameburuzwa mahakamani wakidaiwa kukataa kuwahudumia watoto wa mfanyabiashara huyo aliowazaa na mkewe Jacqueline Ntuyabaliwe
Kesi hiyo imefunguliwa na Jacqueline katika Mahakama ya Watoto iliyoko katika eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam

Wasimamizi wa mirathi hiyo wanaokabiliwa na kesi ni mtoto wa marehemu, Benjamini Mengi.

Habari zambazo Mwananchilimezipata ni na kuthibitishwa na wakili wa mjane huyo, Audax Kahendaguza, kwa ridhaa ya mteja wake, katika shauri hilo la madai namba 50 la mwaka 202, Jacqueline anadai matunzo ya watoto hao ikiwamo ada ya shule.

Anadai kuwa watoto hao walikuwa wakigharamiwa ada na baba yao pamoja na huduma nyingine zote walizostahili kutokana na kipato alichokuwa anakipata kwenye shughuli zake za kibiashara, ambazo kwa sasa zipo chini ya wasimamizi hao wa mirathi.

Anadai kuwa hata baada ya kifo cha baba yao, awali wasimamizi hao walikuwa wakwalipia ada na huduma nyingine japo mara mojamoja; kwamba sasa wameacha kabisa kuwalipia ada ya shule pamoja na huduma nyingine licha ya kuwaomba mara kadhaa.

Mawakili wa wadaiwa walieleza kuwa hawajaandaa majibu ya madai hayo kwa kuwa wateja wao wako mikoani huku mahakama ikiwataka kuwasilisha majibu yao Februari 17, mwaka huu siku ambayo pia kesi hiyo itatajwa tena.

Kesi hii iekuja wakati bado kuna mgogoro wa mirathi ya marehemu Mengi kati ya pande hizo mbili, kwani bado kuna shauri la mirathi linasubiri uamuzi.

Chanzo: Mwananchi

View attachment 2108732View attachment 2108733

Huyu mwanamke Lazima ana matatizo tu! Kuanzia Kesi y kwanza mpaka sasa ndo matokeo yake na hatopata anachotafuta
 
Funzo kwa wasichana wa siku hizi wakome kudandia Ndoa za watu wenye ukwasi wao.

Huyo Ntuyabaliwe mwenyewe kapuyanga na wengi mno.

Isisahaulike kuwa alikuwa na kashfa ya kuhusishwa na mwarabu aliekuwa master mind wake akusafiri nae sambamba na Marehemu kwa siri.

Ukimuuliza hata historia kamili ya Marehemu haijui zaidi ya kukariri akaunti zake tu.

Mleta topic umeandika kimaslahi binafsi.
Mleta topic utakuta ndo yeye mwenyewe mwanamke tamaa
 
huyo dada anashindwaje yeye kuwalea watoto wake...Yeye si amebaki na mikono, miguu, macho na ule uzuri wake aendelee tu kulea watoto vizuri kama alivyokuwepo baba yao, Huo ndio utakuwa upendo otherwise hata kwa baba yao alifuata mali tu..
Yap!....ila hao watoto wana haki ya kurithi mali zilizoachwa na baba yao na mama yao ni lazima alisimamie hili.
 
Pale aibu inapokupata kuingiza udini pasipostahili. Acha kukurupuka kuleta udini. Kesi za mirathi hazijali ni ndugu wala mtu baki. Iwe muislamu wala mkristo mambo yale yale.

Nimeshajibu swali lako la kusema kwenye uislamu hakuna longolongo,wamsaidie basi mtoto wa mpakanjia na wenzie
Msimamiz wa mirathi wa kina mengi ni ukoo wa kina mengi. Nimeuliza watoto wa mpakanjia wamezurimiwa na ukoo wa mpakanjia ama wa ukoo wa chifupa ama ukoo wa nani ?
 
Hapana hao wasimamizi wanapaswa watenguliwe usimamizi mara moja.
aliye stahili kuwa msimamizi ni mjane wa marehemu akisaidiwa na ndugu mwengine.


Lengo la hao wasimamizi naa ndugu ni kumdhulumu mjane na watoto wake.

wanawake mko wapi? mjane huyu Jaquline ananyanyaswa kiasi hiki wakati ana haki!!

Vyama vya kutetea Haki za wanawake mko wapi? taasisi na NGO mbalimbali mko wapi kinacho fanyika ktk sakata hili ni unyanyasaji wa kijinsia.
mfumo dume unakandamiza haki za mjane.
 
Watoto wakubwa sio rizki, mzee akaona isiwe tabu manake nisipoangalia kizazi changu kinaishia hapa...bora hata alivyowapata hao twins.
Utajiri una mambo sana huu usikute ni maagano kuwa apatecutajiri ila kizazi kisiendelee,motie alikufa akiwa kijana,hawa wengine dah unakufa na mihela hata mjukui huna
 
Hapana hao wasimamizi wanapaswa watenguliwe usimamizi mara moja.
aliye stahili kuwa msimamizi ni mjane wa marehemu akisaidiwa na ndugu mwengine.


Lengo la hao wasimamizi naa ndugu ni kumdhulumu mjane na watoto wake.

wanawake mko wapi? mjane huyu Jaquline ananyanyaswa kiasi hiki wakati ana haki!!

Vyama vya kutetea Haki za wanawake mko wapi? taasisi na NGO mbalimbali mko wapi kinacho fanyika ktk sakata hili ni unyanyasaji wa kijinsia.
mfumo dume unakandamiza haki za mjane.
Mjane wapi sema jambazi lililotumia silaha za kibailojia kwa maana ya urembo wake
 
Yule demu ana tamaa sema kabila lake lina mbeba
Ana wakilisha vizuri kwao.
 
Mjane wapi sema jambazi lililotumia silaha za kibailojia kwa maana ya urembo wake
ndiye aliye kuwa anampa furaha marehemu.
hivyo anayo haki utake usitake.
Ndugu wa Marehemu wanataka kupora na kudhulumu Haki ya Mjane kwa kutumia mfumo dume kandamizi.
 
Back
Top Bottom