..Sijui kwanini unapandwa hasira kuhusiano na mawazo na mapendekezo yenye faida kwa mustakabali wa amani, na umoja wa taifa letu.
..Tunapojadili hoja kama TUME HURU YA UCHAGUZI hatupaswi kuwa na hasira kwa jambo jema kama hilo kama unavyoonyesha.
..Mwenezi wa CCM aliyesema Tume Huru haitasimamia uchaguzi wa 2025, bali itasimamia uchaguzi wa 2030, anatokea Zanzibar, na alionekana ktk vyombo vya habari.
..Kuhusu uteuzi wa Makamishna wa Tume Huru labda ungetueleza kwanini Raisi hajawateua mpaka hivi sasa. Sheria imeishasainiwa, kwanini Makamishna wa Tume ya zamani bado wako ofisini?
..Sheria inasema Tume Huru itasimamia chaguzi zote. Na uchaguzi wa serikali za mitaa utasimamiwa na Tume Huru baada ya serikali kuandaa sheria yake.
..Kilichotokea ni serikali kuburuza miguu na kutokuandika sheria ya uchaguzi serikali za mitaa, ili kutoa upenyo kwa Ofisi ya Raisi ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM kusimamia uchaguzi huo.
Matokeo yake ofisi ya Raisi ikaharibu uchaguzi wa serikali na mitaa na kusababisha aibu, na malalamiko mengi.
View: https://www.youtube.com/watch?v=30yx5KU2wWo
..Kwa hiyo mpaka hapo utaona kwamba hakuna nia njema, na uaminifu, kwa upande wa serikali ya CCM katika suala zima la Tume ya uchaguzi, na mifumo ya kidemokrasia, hapa nchini.
..Naomba tunapojadili suala hili tutangulize MASLAHI YA NCHI mbele, kabla ya maslahi ya vyama au kiongozi wa chama.