Pre GE2025 Wasira awatetemesha akina Tundu Lissu na Wenzake: "Kauli Mbiu ya "No Reform, No Election" Haina Maana Kwa Sasa"

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Huwa nashangaa na kuhuzunika kuona saa zingine mtu alie soma hata civics na mweny hakili akikataa mabadiliko ya katiba, daaa nikweli ndomaana hata mbuzi ukiwa unampeleka malishoni ukiwa umemfunga kamba unamvita na yee analudi nyuma asijue kuwa unampeleka dehemu sahihi,, vivyo hivyo wapinzani wana tetea wananchi ila wwananchi wamekua kama mbuzi baadhi
 
Jifunze kwanza kuandika vizuri ndio uje kwenye topics hizi nzito. Kwa sasa kiwango chako cha juu kabisa ni kujadiliana na bata
 

..Kwanza Chadema, Mbowe, Lissu, hawakukimbia kushiriki mchakato wa kurekebisha sheria za uchaguzi.

..Kilichotokea ni serikali na Bunge kupuuza maoni ya wadau ambayo yangepelekea marekebisho ya maana ktk Tume ya uchaguzi, na mifumo inayosimamia uchaguzi.

..Marekebisho yamefanyika lakini hayajakidhi matarajio ya vyama vya siasa, viongozi wa dini, asasi za kiraia, na wananchi mbalimbali waliojitokeza kutoa maoni kwa Kamati ya Bunge.

..Hata hayo marekebisho yasiyokidhi viwango ambayo Bunge limepitisha serikali bado haitaki kuyatekeleza.

..Kwa mfano, Bunge limepitisha sheria chaguzi zote zisimamiwe na Tume, serikali imepuuza na Tamisemi wakasimamia uchaguzi wa serikali za mitaa.

..Mfano mwingine, Bunge limepitisha sheria kuanzisha Tume Huru, lakini serikali imegoma kuteua Tume hiyo, makamishna wa Tume ya zamani bado wako ofisini.

..Hii nchi ni yetu sote. Rais Samia ashauriwe vizuri katika suala hili na atende HAKI.
 
Ndomana nakuuliza ulilelewa na wazazi wote au wewe ni mtoto wa nnje ya ndoa? Nijibu plz bro
Maelezo yako yote ni fake. 🤣 🤣 🤣 🤣 Ukionesha certificate ya kujua kutumia kiswahili sanifu nitakujibu.
 
Hoja za majuha, kama msingempiga zile risasi 16 angekimbilia huko Ubelgiji? CCM weupe kweli kichwani kama tlaatlaah
Usha ona kaka af wengi wao ni wazee walio soma elimu ya watu wazima ko wanabuluzwatu kwenye matope
 
Usha ona kaka af wengi wao ni wazee walio soma elimu ya watu wazima ko wanabuluzwatu kwenye matope
Chama cha majuha wanakimbilia jf kuja kuzima moto wa TL huku, tatizo lao wanavyofanywa wapumbavu huko na kushindwa kuhoji wanakubali na kushangilia wanafikiria wakija huku kuna wajinga wenzao
 
Lissu ameshawahi kulifanyia nini Taifa la Tanzania? 🤣 🤣 🤣 🤣 Taja jambo moja tu
Huyo mzee wa hovyo Wassira kwa muda wote alioishi Tanzania anewahi kulifanyia nini taifa? Taja jambo moja tu
 
..Kwanza Chadema, Mbowe, Lissu, hawakukimbia kushiriki mchakato wa kurekebisha sheria za uchaguzi.
Naomba tuanze kwa hili. Katika mazungumzo na majadiliano ya mabadiliko ya sheria za uchaguzi. Makatibu wa vyama vyote vya siasa hapa Tanzania walihudhuria kwenye majadiliano ispokuwa CHADEMA tu. Tueleze ni sababu zipi hao CHADEMA iliwapelekea kugomea mazungumzo?

..Kilichotokea ni serikali na Bunge kupuuza maoni ya wadau ambayo yangepelekea marekebisho ya maana ktk Tume ya uchaguzi, na mifumo inayosimamia uchaguzi.
Tuambie kuhusu katiba ya Tanzania wawakilishi wa wananchi kama siyo wabunge. Nitaomba uniwekee ibara ya katiba yetu na sheria za Tanzania zinazoeleza kuwa Wabunge siku hizi siyo wawakilishi wa watanzania.
..Marekebisho yamefanyika lakini hayajakidhi matarajio ya vyama vya siasa, viongozi wa dini, asasi za kiraia, na wananchi mbalimbali waliojitokeza kutoa maoni kwa Kamati ya Bunge
Fafanua matarajio ya vyama vya siasa. Vyama vya siasa vipi? Vitaje
Viongozi wa dini zipi? Na asasi za kiraia zipi? Hivi unajua kuwa hapa Tanzania tupo na asasi za kiraia zaidi ya 10,000?
Unajua zaidi ya 80% ya vyama vya siasa nchini vilikubaliana na mabadiliko haya ya sheria?
Tuambie matarajio yapi ulitaka hao uliowataja wayapate?**

..Kwa mfano, Bunge limepitisha sheria chaguzi zote zisimamiwe na Tume, serikali imepuuza na Tamisemi wakasimamia uchaguzi wa serikali za mitaa.
Hapa mzee mbona unajichanganya? Umesema Bunge halikusikiliza matarajio ya hao uliowataja. Halafu tena unakuja kusema bunge lilipitisha serikali haikusimamia. Which is Which?

Tueleze kigungu kipi cha sheria kimesema TAMISEMI isisimamie chaguzi za serikali za mitaa? Taja hicho kifungu

..Hii nchi ni yetu sote. Rais Samia ashauriwe vizuri katika suala hili na atende HAKI.
Sentensi yako hii haina mashiko kama vitu vidogo tu umeshindwa kuvitolea ufafanuzi.

Kama huwezi kufikiria kwa vitu vidogo tu hivi, Tuache sisi wenye akili tufikirie kwa niaba yako
 
..badala ya kufanya uchaguzi kwa kutumia sheria mbovu kwanini tusiuahirishe mpaka 2016 ili tufanye marekebisho ktk Tume ya Uchaguzi?

..hii nchi ni yetu sote. Raisi apewe ushauri mzuri kwa maslahi ya taifa letu.
Mtu anayemshauri kaamua kumteua mzee wa hovyo Wassira, unategemea ashauriwe nini?
 
Hoja za majuha, kama msingempiga zile risasi 16 angekimbilia huko Ubelgiji? CCM weupe kweli kichwani kama tlaatlaah
Kumbe unawajua waliompiga risasi. Kwanini huendi kutoa taarifa na kufungua kesi? 🤣 🤣 🤣
 
CCM ndio imepewa dhamana ya Watanzania wote. Ndio maana Lissu anapewa misaada yote anayoihitaji na Serikali ya CCM. So hakuna anayemchukia LIsuu
Misaada kama kumpiga risasi 16 na kukataa kumtibia? Zaidi toka 2017 September hadi leo hakuna hata mtu mmoja aliyekamatwa ndio dhamana hiyo?
 
Chama cha majuha wanakimbilia jf kuja kuzima moto wa TL huku, tatizo lao wanavyofanywa wapumbavu huko na kushindwa kuhoji wanakubali na kushangilia wanafikiria wakija huku kuna wajinga wenzao
Huna uwezo kijana wa kujadili hizi hoja nzito. Utaishia kutaja Majuha, majuha, majuha bila kuongea chochote chamaa. 🤣🤣🤣🤣Inaonekana unaupenda sana Ujuha
 
Chama cha majuha wanakimbilia jf kuja kuzima moto wa TL huku, tatizo lao wanavyofanywa wapumbavu huko na kushindwa kuhoji wanakubali na kushangilia wanafikiria wakija huku kuna wajinga wenzao
Hata hawajiulizi kwanini hawajafanya uchaguzi ndani ya chama wa kumuchagua mgombea uraisi?? Tatz avijifkilii ndomaana unaambiwa kuongoza wamarekani wawili bora uongoze watanzania 100000
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…