Wasomi elimu isiwapumbaze mnapishana na fursa nyingi

Wasomi elimu isiwapumbaze mnapishana na fursa nyingi

Kwaiyo amesomea kazi ya kuuza uji?
Ujinga wenu ni kuwa mnawaza kuajiriwa tuu, yan hamtaki kufanya chochote kile ,tulitegema taaluma zenu ziwasaidie hata kuanzisha miradi midogo midogo sio lazima muanzie juu
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] nimeshangaa sana. Kuna vitu watu tunafanya kutafuta riziki ila hata sio vya kujivunia mbele za watu hadi kutolea mifano. Kuuza uji ni nini mbona hata asiyejua kusoma wala kuandika anaweza kuuza.
Point hapo sio kuuza uji , point ni kuanza kufanya chochote kitakachoweza kukupa kipato
 
Wanashindwa lakini huwakuti wamekaa tuu, wanajishughulisha mtaani
Kila mtu na namna yake ya kuishi, hata huyo aliyekaa tu ana target zake za kuishi. Kama asingekuwa na uhakika wa kula angeenda tu hata kubeba zege. Ukiona kakaa tu keshapiga hesabu zake kuhusu fursa zinazomzunguka kaona hazimlipi. Na kuhusu kuilalamikia serikali hilo halikwepeki, lazima italalamikiwa tu as long as madudu yapo. Ushahidi ni report ta cag, na sio wote wanailalamikia ili iwape tu ajira hapana, wanalalamika ili serikali ifanye equal distribution za resources
 
Oya we hujanielewa kabisa yaan still bado umekaza fuvu, nazungumzia mtu ambae hawezi kuonana na Manager na hamjui Manager au unafikiri Manager anajuana na kila mtu ovyo ovyo tu? Nimekwambia kuhusu HR sababu ushahidi ninao bila HR hupati kazi shikiria hapo na wanawala sana dada zenu

Afadhali umekubali mwenyewe kwamba manager hajuani na kila mtu hovyo hovyo, so unahitaji kujuana na HR kama dalali maana yeye(HR) ni rahisi kupatikana.

Hao dada zetu wanaoliwa wapo kwenye kundi moja na wewe mnaodhani HR ni mtu mkubwa sana, ndio maana wanaliwa, still wengi kazi hawapati baada ya mission kufeli kwa sababu HR hana ukubwa huo mnaodhani anao.

Sasa wewe ndiyo uendelee kukaza fuvu maana ukweli umeshaujua na utakua unapingana na kauli yako mwenyewe.
 
Kila mtu na namna yake ya kuishi, hata huyo aliyekaa tu ana target zake za kuishi. Kama asingekuwa na uhakika wa kula angeenda tu hata kubeba zege. Ukiona kakaa tu keshapiga hesabu zake kuhusu fursa zinazomzunguka kaona hazimlipi. Na kuhusu kuilalamikia serikali hilo halikwepeki, lazima italalamikiwa tu as long as madudu yapo. Ushahidi ni report ta cag, na sio wote wanailalamikia ili iwape tu ajira hapana, wanalalamika ili serikali ifanye equal distribution za resources
Kuilalamikia serikali ni kwa kila mtu haijalishi hali ya kiuchumi, hata ukienda kwa matajiri wanailalamikia pia ni haki yao huwezi kuwazuia
 
Narudia tena, kuna dada mmoja alimaliza degree yake pale mlimani, badala ya kutembea na CV yake maofisini kuomba kazi, alifanya kazi ya kuuza uji wa ulezi. Anatembeza na chupa yake kubwa ya uji na kuuza uji na ucheshi mzuri. Sasa hivi amefungua saloon yake kwa kutumia kipato cha kuuza uji na mambo yake ni mazuri. Kazi ni kazi, ili mradi ujue kwa siku unaingiza ngapi.
Hahahahah kwamba uji ndio umempa million 7 za kufungulia saluni. Kaa kijanja wewe ogopa sana hizo success stories za watoto wa kike 😀
 
Narudia tena, kuna dada mmoja alimaliza degree yake pale mlimani, badala ya kutembea na CV yake maofisini kuomba kazi, alifanya kazi ya kuuza uji wa ulezi. Anatembeza na chupa yake kubwa ya uji na kuuza uji na ucheshi mzuri. Sasa hivi amefungua saloon yake kwa kutumia kipato cha kuuza uji na mambo yake ni mazuri. Kazi ni kazi, ili mradi ujue kwa siku unaingiza ngapi.
Hahahahah kwamba uji ndio umempa million 7 za kufungulia saluni. Kaa kijanja wewe ogopa sana hizo success stories za watoto wa kike 😀
 
Mkuu wewe ukiomba kazi barua yako hua unaandika kwenda kwa Nani Boss wa Kampuni au HR? Emu tuanzie hapo maana Leo nimekutana na fuvu jipya
mbeya.jpg


Tuanze na hiyo hapo niliyo attach.

Mimi nitaandika kwenda kwa CENTRE MANAGER, wewe utaandika kwenda kwa HR?

Baada ya hapo ndiyo utajua kwamba wewe ni fuvu la aina gani 😁 😁 😁 😁
 
Happy Easter to everyone,

Nimeguswa ku share haya machache kuhusu hili kundi kubwa la watu (Wasomi) ambalo ndo linaongoza kulalamika huku mitandaoni kuwa maisha magumu na wengine wakienda mbali zaidi kuwa serikali yetu haiwajali.

Nimefuatilia kwa ukaribu wasomi wengi, kitu kinachowakwamisha ni wao wenyewe kujiona wao ni tofauti na watu wengine kwenye jamii na wanastahili kupewa heshima kubwa.

Huu mtazamo wenu wasomi ndo unawafanya mnapishana na fursa nyingi kwakua lazima tukubali hakuna serikali duniani iliyoweza kuwaajiri watu wake wote , hivyo basi ukiwa kama msomi na umekosa ajira cha kwanza kabisa kubali kujishusha kuendana na mazingira halisi ya mtaani.

Elimu uliyo nayo isikufanye uzubae tuu jichanganye na watu wa mtaani walioanza ujasiriamali hata kama wanafanya kwa kiwango cha chini, kupitia kujichanganya kwako kutakuongezea maarifa ambayo huna.

Elimu uliyo nayo isikufanye kujiona kuwa wewe ni mtu wa hadhi ya juu, huku huna source yoyote ya kukuingizia kipato. Kama huna means yoyote ya kuingiza kipato basi ujue kuna vingi sana huvijui unapaswa ujifunze.

Elimu uliyo nayo itakusaidia tuu endapo utakubali kubadilika kutokana na mazingira lakini pia kukubali uhalisia wa mambo coz huku mtaani mambo ni tofauti sana na vile wasomi wanavyochukulia pindi wakiwa vyuoni.

Elimu ulionayo ukiongeza na maarifa kidogo tuu utakayoyapata pindi ukijichanganya na watu mtaani itakua na faida sana, kuliko kusubiri ajira.

Elimu uliyo nayo bila kuwa na pesa tambua fika hakuna atakayekupa heshima kama wengi wenu mlivo na mawazo hayo ya kijinga.

Kushinda mitandaoni na kulalamika kuwa ajira ngumu tuu bila kuchukua hatua zozote ni ujinga ambapo ni wa kuacha mara moja.

Tunawategemea sana kuja kuleta ukombozi mtaani kutokana na elimu mlioipata, ila hii hali ya kulaumu tuu serikali inatupa sana mashaka kuwa kuna uwezekano tuna wasomi ambao hawajaelimika.
Mwana huu ni umbea sasa
 
Ujinga wenu ni kuwa mnawaza kuajiriwa tuu, yan hamtaki kufanya chochote kile ,tulitegema taaluma zenu ziwasaidie hata kuanzisha miradi midogo midogo sio lazima muanzie juu
Kuna point gani kwa mtu aliyesomea sheria kulima mboga mboga?

Au mtu aliyesomea uhasibu kufuga kuku?
 
Kuna point gani kwa mtu aliyesomea sheria kulima mboga mboga?

Au mtu aliyesomea uhasibu kufuga kuku?
Nani kakwambia kua ni lazima mwanasheria alime mbogamboga au mhasibu afuge kuku

Hapa tunazungumzia afanye lililo ndani ya uwezo wake
 
Back
Top Bottom