Wataalamu wa Biashara nauliza Comfort Iringa ilikufaje wakati ilikuwa na wateja abiria wa mabasi?

Tatizo la confort hotel ilikuwa ni kuuza vyakula visivyo na ubora,bei juu, na vilivyolala, unauziwa chips zilizolala,halafu hazipashwi, unauziwa chips za viazi vibovu( vimefikia stage ya kuwa mbegu,vinakuwa na ukijani flan hivi halafu haviivi) vyenye uchungu. Nyama ya kuku iliyovunda. Na uchafu wa mazingira. Hata al jazeera ni kwa sababu tu hajapata mpizani,ila akipatikana wa kuweka hotel ya ukweli kama njia ya kaskazin pale anafunga. Liverpool alifunga hivyo hivyo sababu ya huduma mbovu akakosa wateja,sasa hivi alivyoikarabati na kuboresha huduma wateja wamerudi
 
Mama hajui namba ya siri ya ac ya baba ya bank.. Ngoz nyeusi tuna roho mbaya vibaya mno
 
Wataalamu wa Biashara nauliza Comfort Hotel, kitonga Iringa ilikufaje wakati ilikuwa na wateja abiria wa mabasi?
Alipofariki mwenye maono na mmiliki Andeson Mwanyato, ndugu zake waliobaki walishindwa kuendeleza uwekezaji wake mzuri. Hata mabasi yake yote yakaisha. Ila bado ni eneo mwafaka sana kwa biashara kama unaweza kununua na kuliendeleza.
 
Nilikuwa najuana naye sana Anderson Mwanyato niliwahi kumpa ushauri wa kibiashara. Alikuwa msikivu na mtulivu ila alipenda kufanya aonavyo yeye na alikuwa na ujasiri wa kuthubutu.
 
Daraja la Chipite kijiji cha Nangoo, nimepita sana maeneo hayo
 
Shikamoo
 
Kila jambo na zama zake. Kwani Blackberry ilikufaje?
Hazikosekani sababu za kufa, kwenye mtihani ukiulizwa kuanguka kwa ottoman empire ama wamongoli, ama chochote kile utajibu kila kitu na wakati wake?

😂😂
 

Weka rekodi zako sawa mkuu, mwaka 1998 ndio kulikuwa na mvua za El Nino na balaa kubwa lilikuwa ni kuzolewa kwa basi la No Challenge Tanga...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…