Wataalamu wanadai hizi ndiyo sababu za Tsh kuimarika dhidi ya Dola

Wataalamu wanadai hizi ndiyo sababu za Tsh kuimarika dhidi ya Dola

Dola ya Marekani haijashuka thamani kwa Tanzania tu, bali pia kwa nchi nyingine duniani. Nimesoma mahali pia kuwa sababu nyingine ni kupunguzwa/kushushwa kwa viwango riba (interest rates) huko US, na hivyo kusababisha baadhi ya mabwanyenye wa huko kukimbiza baadhi ya akiba na au vitga uchumi vyao kutoka US kwenda nchi nyinginezo. Wataalamu wa mambo ya uchumi wanaweza kutusaidia kutoa ufafanuzi.
Hiyo Marekani na idondoke mpaka ishangae
 
Hii ni short term trend. Ili iendelee zaidi ya miezi 6 inabidi Tanzania iongeze exports significantly, kitu ambacho sioni kikitokea.

In the mid to long term USD itapanda tena tu.
Marekani na iporomoke mpaka iache ushoga,nashangaa BRICS wamepotea ghafla
 
Nimeona huko mtandaoni wataalamu wakielezea sababu za Tsh kuimarika dhidi ya dola.

1. Wanadai kuwa kwa sasa ada zote za utalii zinalipwa kwa Tsh. Kwa hiyo watalii hao wanatakiwa kutumia dola kununua Tsh ili waweze kulipa ada mbalimbali.
Kuna mtu huko anabubujikwa na machozi
 
Hii sio kweli kwa 100%.
Serikali haikufuta ada za utalii kulipwa kwa dola, bali serikali ilifuta utaratibu wa kulazimisha malipo mbali mbali hapa nchini kuwa kwa dola.
Serikali inahitaji mnoo dola kutoka nje ziingie nchini (ili ikienda nje kufanya malipo izitumie) na serikali kwa sasa haitaki kutoa dola zake kuzunguka humu humu nchini hivyo ndio hilo dhumuni la kufanya hivyo.
Mpaka leo hii na saa hii watalii kutoka nje wanalipa kwa dola. Na hilo ni rahisi kwao na habari njema zaidi kwa serikali
Mwisho kabisa, kushuka kwa dola dhidi ya shilingi ni suala la mpito na halina uhusiano wa moja kwa moja na hatua za serikali. Kitaalamu tunasema it is a nature phenomenon of the graph!
Wanadai zamani watalii walikuwa wakilipa ada na gharama zingine kwa dola moja kwa moja kwa makampuni ya utalii, taasisi na mahoteli. Na serikali ilikuwa ikifuata chake kwenye makampuni na mahoteli haya ndiyo ilikuwa inapata dola zake. Hili lilikuwa linasababisha ikose dola nyingi sana(kumbuka kile kikao na wadau wa utalii)

Lakini sasa ni kuwa mtalii akiingia nchini anapaswa kubadilisha dola zake kuwa shillingi(ananunua shillingi) na ada na gharama zote anazolipia analipia kwenye makampuni, taasisi na mahoteli analipa kwa Tsh. Kitendo hiki cha kununua Tsh kimefanya Tsh ihitajike na kupanda thamani.

Nafikiri pia imecontrol mahali ambako watalii hawa hununua hizo Tsh.
 
Dola ya Marekani haijashuka thamani kwa Tanzania tu, bali pia kwa nchi nyingine duniani. Nimesoma mahali pia kuwa sababu nyingine ni kupunguzwa/kushushwa kwa viwango riba (interest rates) huko US, na hivyo kusababisha baadhi ya mabwanyenye wa huko kukimbiza baadhi ya akiba na au vitga uchumi vyao kutoka US kwenda nchi nyinginezo. Wataalamu wa mambo ya uchumi wanaweza kutusaidia kutoa ufafanuzi.
Unakumbuka Ksh ilipanda thamani kwa karibu 25% ndani ya muda mfupi sana huku pesa yetu ikiwa vilevile. Nadhani sababu ya hili ni monetary policies za nchi husika na si sababu ya Feds kushusha riba. Pengine tumeiga mbinu ya Kenya.
 
Benki kuu wameongeza interest rate kwa muda mfupi, hili suala ni la muda mfupi , dollar itapanda watu watashangaa....

Ujanja ujanja tu kuelekea 2025.
Shilingi ikiimarika mbona interest ndio inatakiwa kushushwa?
Shilingi ikishuka ndio inerest inapandishwa ili watu waweke hela benk ili kupunguza mfumuko
 
Mbona dola imeshuka karibu nchi zote duniani? Yani wabongo sijui mnafikiri tunaishi kisiwani
 
Mhuuu na Uganda,Kenya na kwingineko?
Shilingi pia imepanda vs Kenya, kipindi shilingi imeshuka vs Dollar hela ya Kenya ilifika hadi tsh 22 ila sasa hivi ni kama 18. Same kwa Uganda wiki chache zilizopita shilingi moja ya Tz ulipata 1.35 ugx ila sasa hivi unapata 1.54. So ni consistently imekua na nguvu kote.
 
Mbona dola imeshuka karibu nchi zote duniani? Yani wabongo sijui mnafikiri tunaishi kisiwani
Si Kweli ni Tanzania tu, atleast compare to majirani

Screenshot_20241215-113433_Pixel Launcher.png
Screenshot_20241215-113354_Pixel Launcher.png

Ukiangalia hapo Kenya na Uganda utofauti baina ya mwezi wa 11 na 12 hakuna ama ni mdogo sana

Screenshot_20241215-113459_Pixel Launcher.png


Ila kwetu unaona kabisa utofauti dola inashuka vs TSh.
 
Nyie ndio mtaporomoka na kuanguka kwenye ushoga mpaka muombe Marekani wawasaidie. Mbona wanawasaidia sana kwenye umaskini kama mnafikiri wamelaaniwa, nani kati yenu na Marekani aliyelaaniwa. Pia msubiri Dola ikianza kupanda mwakani mpaka kufikia TZS 3800/= ndio mtajua nguvu na akili za Wamarekani.
Hiyo Marekani na idondoke mpaka ishangae

Marekani na iporomoke mpaka iache ushoga,nashangaa BRICS wamepotea ghafla
 
Nyie ndio mtaporomoka na kuanguka kwenye ushoga mpaka muombe Marekani wawasaidie. Mbona wanawasaidia sana kwenye umaskini kama mnafikiri wamelaaniwa, nani kati yenu na Marekani aliyelaaniwa. Pia msubiri Dola ikianza kupanda mwakani mpaka kufikia TZS 3800/= ndio mtajua nguvu na akili za Wamarekani.
Mhhhh,uchawa ni fursa mpya pia
 
Back
Top Bottom