Magonjwa Mtambuka
JF-Expert Member
- Aug 2, 2016
- 32,246
- 31,176
Hapana, lakini nakupa ushauri wa bure tu. Jifunze kuandika na kuongea kwa ufasaha; iwe ni lugha ya Kiswahili au Kiingereza. Si vyema kudonyoa donyoa vijimaneno vya hapa na pale. Utaonekana ni limbukeni tu kwa kufanya hivyo.😂Kwahio kujua Kiswahili ni moja ya requierments za kujiunga JF ?...
Ushauri wa Bure, hapa hatuandiki thesis.., ni muhimu ujumbe ufike... mwisho wa siku issue ni communication, ukianza kufuatilia uwasilishaji wa points za watu kwenye social media (na sio jukwaa la lugha) ni kupoteza muda wako; Pili ukifanya vitu kwa hofu watu wanakuonaje ni dalili za inferiority complex... (wewe fanya kinachokuja kwako kwa urahisi)Hapana, lakini nakupa ushauri wa bure tu. Jifunze kuandika na kuongea kwa ufasaha; iwe ni lugha ya Kiswahili au Kiingereza. Si vyema kudonyoa donyoa vijimaneno vya hapa na pale. Utaonekana ni limbukeni tu kwa kufanya hivyo.😂
Acha uongo. Kuna media inalipa vizuri kama Azam tz?Unakuwa na mtangazaji Mauldi Kitenge, Eddo Kumwembe hawa hawana shule ya Uandishi wa habari ni ujanja wao na kulaghai watu. Baraka Mpenja kaenda shule ila mropokaji na wala sio mtangazaji. Fuatilia goli la Dube alivyotangaza kuna maneno aliropoka kuhusu Dube. Ama fuatilia goli la Aziz Ki alilofunga dhidi ya Simba alivyoropa maneno ya kijinga. Anaropoka baada ya kutangaza maneno ya kiswahili fasaha. Pia wamiliki wa hivi vyombo hawalipi vyema wafanyakazi wao. Mfano pale Azam media pana njaa ya kufa mtu. Na media zingine nyingi tu zina malipo hafifu kwa wafanyakazi wao.
Na wewe nawe ni kama vile hujui vizuri Kiswahili. Yaani unabaki kudokoa dokoa vijimaneno ya Kiingereza alimradi tu uonekane unajua Kiingereza. Unakera kweli kweli na huo ulimbukeni wako.
Hivi unajua hata unachokielezea ?!!, Au ukiweka fullspot unasahau ulichokiandika kabla ?KeyserSoze endelea tu na ulimbukeni wako. Sina shida na hilo kabisa.
Kwahio= kwa hiyoKwahio kujua Kiswahili ni moja ya requierments za kujiunga JF ?
Ukitaka definition ya Ulimbukeni ni hicho ulichoweka hapo juu.....
fullspot = full stop, au unaweza kuandika nukta..Hivi unajua hata unachokielezea ?!!, Au ukiweka fullspot unasahau ulichokiandika kabla ?
Nadhani ni vema ukazipitia fikra zako kichwani mwako kabla haujazitoa katika hadhara...
Inaonekana kichwa chako kina internal conflicts
Kuna mmoja wa RFA huenda alikulia kwenye ubanda,ikiwa ni saa 12:30 asubuhi kwake ni saa 12:00 kamili asubuhi na hana marekebisho.Habari wanaJF?
Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha na maneno mengi. Kwa mujibu wa utafiti binafsi nilioufanya hivi karibuni, usikilizaji wa redio na utazamaji wa TV umepungua sana miongoni mwa wafuatiliaji wa habari. Hili halijatokea kwa bahati mbaya bali ni kwa sababu ya kupungua usahihi wa taarifa na ubora wa watangazaji. Sote ni mashahidi jinsi Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na Voice of Kenya (VoK) zilivyokuwa na watangazaji nguli ambao huchoki kuwasikiliza.
Watangazaji wengi wa redio na TV zinazochipukia kama uyoga hapa nchini wanakera mno kwa utangazaji wa ovyo na unaokosa weledi. Ukisikiliza redio na kutazama TV, hasa hizi zinazoitwa Redio/TV za Kijamii, utahisi kichefuchefu na huwezi kuendelea kusikiliza kwa zaidi ya dakika 5! Wanachotangaza ni zaidi ya utumbo. Na kibaya zaidi, hawa makanjanja hawakupitia kabisa kwenye vyuo vya uandishi wa habari. Inasikitisha mtangazaji kutoongea Kiswahili fasaha unabaki unajiuliza: hivi huyu mtu alienda shule kweli au ameokotwa jalalani? Na kama alienda shule, je, huko alienda kujifunza ujinga au maarifa? (FaizaFoxy, 2015). Yaani hawa viumbe hawawezi kabisa kujieleza kwa Kiswahili na Kiingereza fasaha.
Zamani haikuwa rahisi mtu yeyote kujipenyeza kwenye utangazaji ikiwa hajui Kiswahili na Kiingereza fasaha. Na si hilo tu, mtangazaji anatakiwa kuwa na uhakika wa jambo analolitangaza. Juzi nilipata hasira sana niliposikia mtangazaji wa mpira akiutangazia umma kuwa mmiliki wa sasa wa Klabu ya Chelsea ni Roman Abramovich. Wanajiropokea tu ilmradi tonge liingie kinywani.
Utakuta mtu ana lafudhi mbovu na uelewa mdogo kama mbegu ya hardali lakini bado anang’ang’ania kuwa mtangazaji. Ni aibu kubwa. Yaani pale inapotaikiwa kuweka “r”, yeye anapachika “l”, kwa mfano mpira anatamka mpila. Ni aibu iliyoje! Na pia ni wazuri sana kwenye upotoshaji kwa mfano neno wimbo, hutamka nyimbo……..mfano: Leo nawachezea nyimbo moja ya Diamond inayoitwa Kantangaze. Ovyo kabisa!
Kwa ujumla, nchi hii ina watangazaji wenye uelewa finyu na upeo mdogo wa utangazaji. Natoa wito kwa serikali na vyombo vinavyohusika kudhibiti maudhui ya vyombo vya habari kufanya kazi yao kikamilifu ili kuzuia upotoshaji huu unaofanywa na baadhi ya watangazi makanjanja. Aidha, kiwango cha elimu na weledi wa mtu anayefaa kuwa mtangazaji kipitiwe upya. Watangazaji wasiokidhi vigezo wachujwe na kutupwa nje ya ulingo wa utangazaji. Tumechoshwa na upotoshaji.
Alex Ngusa alifariki? au sijaelewa ulivyoandika?Tag ENZI ZA MWALIM TULIKUA NA WATANGAZAJI KWELIKWELI DEO BURABUZA KIDUDUYE MAREHEM OSTAZI PETER OMARI HAYAT PLENCE BAINA KAMUKULU HAYATI ALEXA NGUSA HOME BOY DIWANI KILUMBA ILIKUA HATARI SANA
Mimi haswa na kerwa na Tv stations/ on line Tvs/ Radio station kupiga soga la watu watatu ama zaidi wakibishania jambo ambalo kika mtu halijui na hana majibu ya usahihi nalo.Habari wanaJF?
Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha na maneno mengi. Kwa mujibu wa utafiti binafsi nilioufanya hivi karibuni, usikilizaji wa redio na utazamaji wa TV umepungua sana miongoni mwa wafuatiliaji wa habari. Hili halijatokea kwa bahati mbaya bali ni kwa sababu ya kupungua usahihi wa taarifa na ubora wa watangazaji. Sote ni mashahidi jinsi Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na Voice of Kenya (VoK) zilivyokuwa na watangazaji nguli ambao huchoki kuwasikiliza.
Watangazaji wengi wa redio na TV zinazochipukia kama uyoga hapa nchini wanakera mno kwa utangazaji wa ovyo na unaokosa weledi. Ukisikiliza redio na kutazama TV, hasa hizi zinazoitwa Redio/TV za Kijamii, utahisi kichefuchefu na huwezi kuendelea kusikiliza kwa zaidi ya dakika 5! Wanachotangaza ni zaidi ya utumbo. Na kibaya zaidi, hawa makanjanja hawakupitia kabisa kwenye vyuo vya uandishi wa habari. Inasikitisha mtangazaji kutoongea Kiswahili fasaha unabaki unajiuliza: hivi huyu mtu alienda shule kweli au ameokotwa jalalani? Na kama alienda shule, je, huko alienda kujifunza ujinga au maarifa? (FaizaFoxy, 2015). Yaani hawa viumbe hawawezi kabisa kujieleza kwa Kiswahili na Kiingereza fasaha.
Zamani haikuwa rahisi mtu yeyote kujipenyeza kwenye utangazaji ikiwa hajui Kiswahili na Kiingereza fasaha. Na si hilo tu, mtangazaji anatakiwa kuwa na uhakika wa jambo analolitangaza. Juzi nilipata hasira sana niliposikia mtangazaji wa mpira akiutangazia umma kuwa mmiliki wa sasa wa Klabu ya Chelsea ni Roman Abramovich. Wanajiropokea tu ilmradi tonge liingie kinywani.
Utakuta mtu ana lafudhi mbovu na uelewa mdogo kama mbegu ya hardali lakini bado anang’ang’ania kuwa mtangazaji. Ni aibu kubwa. Yaani pale inapotaikiwa kuweka “r”, yeye anapachika “l”, kwa mfano mpira anatamka mpila. Ni aibu iliyoje! Na pia ni wazuri sana kwenye upotoshaji kwa mfano neno wimbo, hutamka nyimbo……..mfano: Leo nawachezea nyimbo moja ya Diamond inayoitwa Kantangaze. Ovyo kabisa!
Kwa ujumla, nchi hii ina watangazaji wenye uelewa finyu na upeo mdogo wa utangazaji. Natoa wito kwa serikali na vyombo vinavyohusika kudhibiti maudhui ya vyombo vya habari kufanya kazi yao kikamilifu ili kuzuia upotoshaji huu unaofanywa na baadhi ya watangazi makanjanja. Aidha, kiwango cha elimu na weledi wa mtu anayefaa kuwa mtangazaji kipitiwe upya. Watangazaji wasiokidhi vigezo wachujwe na kutupwa nje ya ulingo wa utangazaji. Tumechoshwa na upotoshaji.
Ludia kusoma mkuu umeambiwa ni DIWANI wa kata ya KILUMBAAlex Ngusa alifariki? au sijaelewa ulivyoandika?
Kwa hiyo uwepo wa mitandao ya jamii ndiyo kunafanya waajiri watangazaji wasio na weledi? Unakuta eti Kingwendu, Stan bakora, Mpoki na wengineo eti wanajadili habari na kuchambua magazeti kweli?? Walisomea journalism lini?Hii inaletwa na Kuwepo kwa mitandao ya kijamii. Karibu habari zote unazipata mitandaoni, Hata ukisema usikilize radio ama tv ni kama kurudia yale yale.
maana simu zinajitosheleza video picha , sauti na maelezo kiujumla.
Aisee kamari nalo ni jangaaa...radio zote zimejaa kamari...ujinga
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaaahKimsingi media industry imeingiliwa na washenzi. Kwa mfano mmiliki wa hii online TV angepewa hata kesi ya uhujumu uchumi ahangaike nayo
View attachment 2411411
Kukemea mambo ambayo hayako sawa kwenye jamii ni jukumu letu sote. Hata kama mimi nina source ya kupata reliable information bado nina wajibu wa Kukemea upotoshwaji wa habari pale unapofanyika kwa sababu athari zake hurudi kwa jamii.Freedom of Speech tukianza kufungia watu kwa kigezo hiki tutafungia wote kwa vigezo vyovyote...
I might disagree of what you say But I will defend to the death your right to say it”
By the way wewe kama unakwenda kwa mdau kama huyo kupata concrete news nadhani tatizo lipo kwako na sio kwa mtoa habari...., What next utachukua ushauri wa ki-afya kutoka kwa Tom and Jerry ?
Kukemea na Kufungia ni vitu viwili tofauti..., Na huko Youtube kumejaa Channels ambazo ni Click Baits na nyingine ni conspiracies mwanzo mwisho, sasa tukianza kufungia vichaa wachache mwisho wa siku tutakuta hata wale ambao tunawaona kwa jicho letu kwamba ni vichaa tutawafungia..., Na wale vichaa wanaokubaliana na sisi tutawaachia...Kukemea mambo ambayo hayako sawa kwenye jamii ni jukumu letu sote. Hata kama mimi nina source ya kupata reliable information bado nina wajibu wa Kukemea upotoshwaji wa habari pale unapofanyika kwa sababu athari zake hurudi kwa jamii.