Watanzania kabla ya kuanza mradi wa Bandari ya Bagamoyo tafuteni Articles za 'Lesson from Sri Lanka Hambantota Port'

We jamaa aisee unazungumzia nchi ambayo aiwezi kushindana na bidhaa hata za Kenya kwenye unit costs.

Kwa ivyo we unadhani hakina Bakhresa na wazalishaji wengine watakaa kimya wakati mshindani wao achezi fair kwa msaada wa serikali huku anaenda dominant soko na bidhaa zake; ilhali na wao wana madeni ya kulipa.

Anyway serikali iliyopita ilifanya ilichoona sahihi kwa maslahi mapana ya nchi; na mama nae atafanya anachoona sahihi.

Muhimu msipotoshe Magufuli alizuia bandari hayo si kweli.
 
Sisi tuna bahati moja. Kuna nchi nyingine zimefanya makosa, zikajikuta zime-surrender vipande vya ardhi China hivyo tumeshajua hawa jamaa siyo watu wazuri. Lakini ajabu naona mama Samia ndiyo yuko mbele kuwakumbatia. Tutakuja kujuta sana.
Acheni kumchafua Rais wetu.
Mama ana nia njema sio wale waovu waliokua wanageuza nchi kuwa kama kundi la boko haram kujifanya kuwa wanatetea rasilimali za umma kumbe ni wapigaji wakubwa.

Urafiki wa China na Tanzania hajauanzisha mama Samia.
Na awamu iliyopita ndiyo iliyokua inawapa kila mrafi hao wageni na ukiona mzawa kapewa jua ni wakuzaliwa.

Mama hana upande alioegemea Bali ameegemea Katiba na sheria za nchi.

Wachina watajenga Bandari yetu na wataiacha wakati ukifika. Nchi hii ni nchi ya kijamaa. Muda wowote tunaitaifisha na kuwaambia wachape lapa endapo watajaribu kuleta usanii.

Hatuwezi kutumia tena matrilioni ya fedha kujenga Bandari kwa kuwatumia hao hao Wachina.
Ni ukichaa wa hali ya juu.
Yaani tutoa tril. 30 tujenge Bandari kwa kuwalipa mainjinia wa Kichina na wataalam wa kichina na malighafi za kichina kama miradi inayoendelea ilivyowajaza wachina. Wakati pesa ni za kwetu. Unachukua pesa za wananchi maskini unawapa wachina ili wajenge bandari ambayo itachukua karne mbili kurudisha faida chini ya management ya wabongo wapiga dili na wezi. Mwishowe inakua ni kama huduma na kuomba ruzuku toka serikalini ili ijiendeshe.
Hapana ,kuna watu wanataka ijengewe kwa pesa za madafu ili wapige pesa na kuajiri watoto wao wasio na sifa huku wananchi wakikosa huduma muhimu za kijamii.

Aje mchina mana pesa ni ya kwake na sisi tunatoa ardhi ambayo ni Mali ya Mungu wote tumeikuta na wote tutaiacha. Mungu ametupa ardhi ina kila kitu lakini roho mbaya za watu zinatufanya tunabaki na ardhi isiyoendelezwa kwa mradi wowote. Wabonge wakipewa hiyo ardhi wataifanyia nini zaidi ya kugawana viwanja na kujenga nyumba za kuishi na kupangishia watanzania wenzao tu huku maisha yakizidi kuwa magumu.
 
Mungu ameshaingilia kati kwa kutuletea Rais sahihi mpenda haki na anayesimamia katiba na sheria za nchi.

Kwa serikali ya akina Sabaya na kundi lake kila mwekezaji alionekana ni mwizi hivyo tulidanganywa na kujazwa ujinga na kupewa maadui wasiojulikana na wasiopo huku wabaya wetu wakiwa waamekalia ofisi za umma na kula bata wakijiita wazalendo.
 
Wewe kwa sasa unapata nini kwa kutokuwepo kwa hiyo bandari?

Au ni basi tu kwa sababu kuna mtu alituongopea kuwa wanataka waikalie miaka 99 wasiulizwe? Ni mkataba gani usio na wataalam wa kuujadili na kuupitisha kwa maslahi ya umma. Kwa nini asingeipeleka hiyo mikataba kule bungeni kama kweli alikua na nia njema ?

Ogopa mtu abayetaka kila mwekezaji awekeze anapotaka yeye hata kama ni mwekezaji wa hasara.

Hivi ni miradi mingapi iliyoanzishwa na inatia hasara taifa lakini iliendelea tu kwa sababu ya kutumika kama kichocheo cha maendeleo mengine?
 
Bandari ya DSM ni kichaka cha mafisadi na joka la kuwatia watanzania umaskini.

Kuagiza mizigo kupitia bandari ya DSM ni gharama kubwa sana. Kuendekeza wezi na kubana wigo wa ajira na kutanua zone ya kiuchumi ni jambo lisilofaa kabisa.
Pwani ya Bagamoyo itajengwa viwanda zaidi ya mitatu. Huoni kuwa tutapanua wigo mkubwa wa kodi kwenye viwanda na ajira?
Yani tubaki na kabandari kamoja tuu katukamue ili kafikie malengo ya kukusanya pesa za mifukoni mwao na za serikali??
Nchi itaendelea kwa kasi ikiwa na wawekezaji na mabilionea wengi sio kashirika kamoja kasiko zalisha zaidi ya kukamua tu pesa za mizigo na kusababisha nchi yetu bidhaa zote zipo juu kuliko hata nchi zisizo na bandari.

Bandari ya DSM waongeze ufanisi na kuweka tozo zenye ahueni sio kupinga bandari ya Bagamoyo.
 
Twiga Tanzania ina 16%, Barrick 84%. Tunagawana 50/50 of economics benefits after Barrick recoupment of capital investments. We have seats at the top table (Board level) kuangalia, kusimamia nakujua kila kinachoendelea. So far wameshatulipa kodi and royalties over $300 millions and on top of that millions in dividends.

Magu aliunda tume kusimamia na ku-negotiate kwa maslahi ya Tanzania. Mchango wetu hapo ni Ardhi yetu makinikia yetu. Na aliweka wazi makubaliano yao.

Ardhi yetu, strategic location (ndio litakuwa lango kufikia soko letu TZ na SADC, EAC). Pia kupitia hapo export hadi Dunia nzima, tax holiday, concession kwenye bill za maji, umeme etc, unafikiri hivi ni vitu kidogo.

Kuna issue ya ushindani, fair competition na viwanda vingine Tanzania.

Bidhaa zinaweza kuwa zinaletwa kutoka China zikaingizwa bila kulipiwa kodi, wakisema wamezalisha hapo kwenye Economic Zone utawapinga vipi wakati huna mamlaka ya kusimamia, kujua vitu vyote vinavyoingia na kutoka na vinavyozalishwa hapo.

Madawa ya kulevya yakiletwa kupitia hiyo bandari, pembe za ndovu na madini yakipitishwa hapo, wanyama wakitoroshwa utajuaje wakati huna mamlaka ya usimamizi.

Kwanini kuna kigugumizi kusema tutaweka vitu vyote wazi.

Mkataba uliokataliwa uwekwe wazi, unaopendekezwa uwekwe wazi, ujadiliwe.

Kuna maswali mengi Usalama wa Taifa na mali zake na watu wake, mkopo unalipajwe, tukishindwa kulipa wanachukua nini? (There is free Lunch, hatuna Shangazi wala mjomba).

Tunahakikishaje kutakuwa na fair competition na viwanda vingine vya ndani, Bandari nyingine za TZ (Dar, Tanga, Mtwara).

Maswali ni mengi sana, majibu hatuyaoni.

Ile tume iliyojadiliana na Barrick, labda wangepewa hii kazi kujadiliana na hawa. Walifanya kazi nzuri sana na income tulipata kutoka day one. Walikuwa wanatu -update everytime what wamefikia kwenye majadiliano. Maboss wao wote walikuja hapa kujadiliana.

Ni sisi ndio tunalikuwa tunaweka masharti sio kupangiwa na wengine masharti ya ajabu.
 
Hiyo kwakweli sijasikia, kama kuna hiyo mipango inaongeza kesi ya Tanga kudai bandari kubwa. Either way Bagamoyo kwa mazingira ya sasa ina supporting infrastructures so kuna strong case kwa mazingira ya leo.
Hizo supporting structure za Bagamoyo dhidi ya Tanga ni zipi
 
Hizo supporting structure za Bagamoyo dhidi ya Tanga ni zipi
Kuna line ya reli ambayo itakuwa under used by cargo kwa dar pekee, so Bagamoyo inaongezea volumes, similar kuna njia ya barabara ambayo inaondoa traffic kuingia katikati ya jiji miundombinu ya barabara tayari ipo, mwekezaji upande wa biashara ya kuzalisha anataka Bagamoyo, wafanyabiashara nchi jirani washazoea Dar.

Kwa sasa hayo maeneo yana miundombinu yenye kuweza kuuwa ndege wawili kwa jiwe moja.

Sisemi bandari ya Tanga aina tija; hizi nchi zetu ni maskini leo lakini zinategemewa kukua kiuchumi, with time hata Bagamoyo itazidiwa Tanzania, Congo na Zambia ni nchi kubwa by size; jumlisha Rwanda na Burundi ipo siku miaka ya mbele itafika zamu ya Tanga tu.
 
"hata mradi ukiwa na hasara sisi hatuhusiki kwenye hiyo hasara" kwa hii statement yako tu naona kwa jinsi gani usivyo na akili na hao wote walio like comment yako..hivi watu weusi mna laana? U think the Chinese are so stupid like your black ass? Watawajengea harafu mkusanye mapato? Hizo bandari zenu za Dar, Tanga na Mtwara zitakuwaje baada ya ujenzi wa hiyo bandari ya bagamoyo? Wawekeze billions of dollars ili wapate hasara? Hao sio wajinga hivyo kama nyie watu weusi, ni hivyo tu.
 
Kwa mantiki hii huo mradi wa bandari ya bagamoyo una mashiko, lakini nchi tumejipangaje kulinda angalau maslahi yetu ya kiusalama.......ukizingatia kwamba tutahitaji kuangalia ikiwa rasilimali zetu zitabaki salama dhidi ya magendo endapo mchina atataka kuendesha hiyo bandari bila mamlaka za nchi kuona jambo lolote linaloendelea.
 
Dar Port inaweza kuwa expanded endapo tutaamua kuhamisha Jeshi la Majini (Navy) kiulinzi nayo ina changamoto zake ila concept ya mradi wa Bagamoyo issue sio ku expand uwezo wa bandari tu bali uwezo wa kuhifadhi mizigo, kuongeza thamani ya bidhaa, kuzalisha bidhaa, kuwa na kutuo cha kufanyia transhipment, na huduma nyinginezo ambazo ni vigumu kufanya hivyo katika eneo la katikati ya Dar es Salaam tayari ni mji uliojengwa, hivyo unahitaji eneo jipya ili uweze kuweka vitu vyote hivyo ambavyo vinaenda sambamba
 
Sio lazima nimuamini au laa, binafsi napata utata cause hakuna aliyewahi kubisha kuhusu hilo. Ukifuatilia Mchina alicho kifanya Sri Lanka na alichokisema mwendazake unapata shida sana mtu wa kumuamini katika hili. Suala la Bagamoyo hata enzi za JK mwenyewe pia lilipata ukakasi kwa baadhi ya watu humu humu jamvini, pekua tu nyuzi za kabla ya mwaka utaona, huna sababu ya kuniita "akili mbovu"
 
Umeuona mkataba wa mradi?
 
Umeuona mkataba wa mradi?
Mimi nadhani ni muhimu watu wakasoma mpango wa maendeleo wa nchi, na pia ni vizuri wakajua kuwa wazo la kujenga bandari ya Bagamoyo sio la wachina ni la mamlaka ya bandari yenyewe (TPA), wachina walikuja kuingia katika hatua za namna gani ujenzi ufanyike kwa kushikiana na private sector, sasa kama wao wachina walikuwa tayari ndio hapo mazungumzo yakaanza na namna mikataba itakavyokuwa ikaanza kujadiliwa.
 
Swala la expansion ya bandari TPA wenyewe wameshafanya feasibility study kuongeza tena it’s not feasible kwa sababu capacity ya meli inazoingia inaongezeka annually it’s reaching a saturation point kwenye uwezo wao wa kasi ya kupakua mizigo. Na tayari wana dry port Bagamoyo ya kutunza mizigo because of space shortages in Dar.

So swala la bandari ya Bagamoyo as far as TPA are concerned it has nothing to do na mipango ya mchina wao pia wana agenda zao zingine. Ujio wa mchina ni kuwaondolea hizo investment tu but they want a win-win situation.

Huko kwenye kuzalisha bidhaa TPA hawana interest wamewapa eneo la size mchina analotaka kufanya huo uwekezaji, sasa kama ana mipango ya belt gani sijui au anashindana na nani duniani TPA couldn’t careless huo uwekezaji afanye mwenyewe tu subject to Tanzanian laws; mchina ataki anataka huo uwekezaji uwe sehemu ya bandari apewe same tax concessions and more.

Ngoja nitafute ile video Kakoko akielezea huo uwekezaji wa viwanda; mchina ndio alikuwa ana hepa siku zote sio serikali.
 
Hujajibu ulichoulizwa na ulichojibu sijauliza.

Umeuona mkataba wa mradi?
 
Kwanini Tusijifunze Kenya na Msumbiji ambako mambo ni mazuri
 
Wewe unawasikiliza kumbe; tatizo watu wanakuja na ngonjera zao ambazo contrary na TPA reasoning kwanini wanahitaji Bagamoyo pia wao wenyewe.
 
Huyu mbunge hajui kujieleza?
au ndio zile 10%
 
Mawazo yako ni ya kivivu na finyu sana. Hivi inaingia akilini kuikabidhi nchi nyingine ijenge na kuendesha sehemu nyeti kama bandari? Unajua madhara yake? Hakika unabebwa na mhemko ya kudhani kuna vitu vya bure. Sisi tuna Bandari tatu na zipo location nzuri sana. Kwa nini tusizipanue zituingizie kipato na badala yake tumpe mgeni ajenge mpya ambayo ataiendesha yeye na kuua hizo zetu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…