Watanzania naombeni mnisamehe kwa hii misimamo yangu ya kisiasa

Watanzania naombeni mnisamehe kwa hii misimamo yangu ya kisiasa

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Kuna kipindi niliamini chama kitakachomkomboa Mtanzania ni Chadema ila nilikuja kubadilisha msimamo wangu nikaamua kushabikia CCM na sababu iliyonifanya niachane na upinzani ni kitendo cha Chadema kumsimamisha Lowasa 2015. Kiukweli niliumia sana roho nikajisemea moyoni haiwezekani kiongozi anaruhusu ndani ya club yake biashara ya madawa ifanywe kuharibu vijana.

Basi ikawa hivyo nikaamua tu kuwa upande wa CCM na kufurahia anguko la CHADEMA japo katika uchaguzi mkuu sikuunga mkono namna uchafuzi uliotokea ule haukua uchaguzi mimi mwenyewe nilikuwa msimamizi msaidizi wa kituo niliyoyaona yanasononesha.

Ila kwa sasa nimekuja kujua CCM ndio wanaotuchelewesha na kutuumiza. Sababu kubwa ni chama cha CCM kimejaa darasa la Saba wa kutosha nenda katika ngazi za wilaya huko utaona viongozi wao ni watu wa namna gani lakini chadema Kuna watu waliosoma cha ajabu hawapewi nafasi.

Kikubwa naomba msamaha kwa yote tusameheane lakini kama ni mipango tuanze sasa hivi ya kuliokoa hili taifa ni heri tufe lakini kieleweke. Kama unaniunga mkono bonyeza like na kisha tupaze sauti popote mlipo muda umewadia kishindo kimefika tusidanganyike tena.
 
Pole Sana kwa Kutangatanga kwa sababu ya Kutokuwa Makini Katika kuujua Ukweli. Sisi Wangine Tuliujua Ukweli Siku Nyingi na Hatukuwahi Kuwashangilia CCM maana Tulijua Mchawi wa Taifa hili ni CCM.

Basi Msamaha umepewa, Kaza boot usirudi Nyuma maana Vita ya Kutafuta Haki ni Ngumu kuliko ile ya Kiuchumi Kama tulivyoaminishwa na utawala ule Katili.
 
Hatuna kinyongo na wewe wali usijione mnyonge tupambane kwa pamoja ukombozi wa taifa hili upo mikononi mwetu
 
Wewe ni wale wanasiasa malkayamalaya Chadema haiwezi kuikomboa nchi wasomi uliowaona Chadema ni kama hao kina mdude kweli are serious? Unachekesha sana mkuu
 
Uliondoka Chadema kwasababu Bilicanas walikuwa wanauza unga?

Kweli una akili ya ndege, sasa mbona hukupeleka ushahidi wako polisi?
 
Ok,

Rudi zako chadema ukaendelee kuwapa nafasi mafisadi papa kugombea urais

Na mkaendeleze na kufungua vijiwe vipya vya kuuza unga maana bills haiwezi rudishwa ila mjiandae kwa anguko kubwa zaidi ya lile la awali
 
Ok,
Rudi zako chadema ukaendelee kuwapa nafasi mafisadi papa kugombea urais
Na mkaendeleze na kufungua vijiwe vipya vya kuuza unga maana bills haiwezi rudishwa ila mjiandae kwa anguko kubwa zaidi ya lile la awali
Mbona unajijibu mwenyewe tena
 
Kesho tena CDM watakuudhi utarudi CCM.

Kweli mnyaturu ni mnyaturu tu🤣

Acha pombe, akili zirudi.

Nakumbuka enzi zangu za utoto, tumechapa sana WALEVI.
 
Back
Top Bottom