mara nyingi nakuaga pande wa upinzani. Lakini hata kama humpedi Magufuli kiasi gani huwezi ukachekelea kuumwa kwake hadharani. Hata kama moyoni kwako unataka iwe hivyo, sio kitu smart kuonyesha hisia hizo kwa umma, ni kosa moja kubwa sana kisiasa.
Ndio maana hata Tundu Lissu alipopigwa risasi Magufuli alitweet kumpa pole, japo naamini serikali yake inahusika, lakini alifanya kinachotakiwa kufanywa na mwanasiasa. Hutakiwi kushangilia ugonjwa wala kifo cha mpinzani wako hadharani.
Walichonishangaza zaidi hawa Wapinzani walikuwa wakichekelea wakati hata mtu mwenyewe haijulikani kama ana afya kweli ama mgonjwa, sasa ukishangilia halafu mtu akajitokeza mzima kabisa utajificha wapi?
Najua ni viongozi wachache wa Upinzani wamefanya hivi, lakini wapinzani wanapaswa kufundishana namna ya ku behave mbele ya public, samaki mmoja akioza watatangaza mmeoza wote, wanaangaliwa na watu wengi, na kila wanachoandika watu wanaki judge.
Hapa wanawafanya CCM kama akina Musiba hivi kuaminika zaidi kuwa Wapinzani wapo kwa ajili ya kumduru magufuli na wanashirikiana na mabeberu kufanya hivyo, yaani wanajipiga risasi ya mguuni kama sio kichwani kabisa.
Wamenisikitisha sana