Watanzania tujiulize busara ya kugomea $450m ya MCC, kisha kukubali $300m toka kwa wezi.

Watanzania tujiulize busara ya kugomea $450m ya MCC, kisha kukubali $300m toka kwa wezi.

Za juu juu tu. Vipi, nimeteleza wapi?
Hizo hizo za juujuu, nikupe 16 percent free shares, I mean FREE SHARES, then tugawane faida 50/50. With no capital injection from your side? Hii nadhani ni ya kwanza kutokea Duniani.

Nadhani tuendelee kushangilia tuu, mengine yatakaa sawa huko mbeleni.
 
Kwani hizi walizotupatia zinatosha kununua NOAH Moja kwa Kila Mtanzania???
 
Hizo hizo za juujuu, nikupe 16 percent free shares, I mean FREE SHARES, then tugawane faida 50/50. With no capital injection from your side? Hii nadhani ni ya kwanza kutokea Duniani.

Nadhani tuendelee kushangilia tuu, mengine yatakaa sawa huko mbeleni.
Tusishangilie sana kwa sababu profit inapatikana baada ya kutoa:

* costs za mining,

* halafu wawalipe investors wote dividends zao (na ACACIA/BARRICK wana majority shares wakati TZ ina 16%)

* halafu kinachobaki ndicho kinachogawiwa 50-50 na serikali.

Sio kikubwa sana lakini ni hatua ya kujivunia.
 
Kuna post ukisoma unajua tu huyu mtu ufahamu wake ni mdogo. Anaweza kuwa na vyeti ila intelectual capacity yake ndoogo. Huyu anafananisha biashara ya madini na msaada. Just imagine !!
 
Mkuu hii ya 50/50 bado naona ni danganya toto,hivi shares 16% faida 50/50 labda kwenye other concentrates siamini hata kidogo
Yote hayo yamekuja kwa sababu ya ile pesa tunayowadai ni nyingi sana. Kama wangetulipa kiasi kile wangelikuwa wanamda mfupi sana wa kusavaiv, ndo maana wakakubali hivyo ("heli ya nusu shari kuliko shali kamili" wanaamini ACASIA)
 
jamani na upande Wa pili nao wamekiri kutoa hiyo hela isiwe mbwembwe tu kama za 37 t za kipindi kile mie accasia wakilipa naombeni Noah yangu
 
Fikra mbovu kabisa!

Ninamuombea Mungu sana Mh Rais afanikiwe, kwani mafanikio yake ndio mafanikio yetu wote na ya hii nchi kwa ujumla wake, hata hivyo ni mategemeo yetu wote hatoweza au kufikiri kubeba fikra zako au kibaya zaidi kuzungukwa na washauri wenye wingwu la fikra zako.

Amen !
Mkuu vipi ulitegemea Serikali iburuzwe MIGA na ICSID?
 
Mkuu hii ya 50/50 bado naona ni danganya toto,hivi shares 16% faida 50/50 labda kwenye other concentrates siamini hata kidogo
Wenye upeo mdogo wa kufikiri wataamini,hii ni danganya toto asee,50/50 ni ndoto.
 
Yaani wewe katika vipengele vyote vile vya makubaliano umeona hiyo $300m tu? Halafu ukiitwa nyumbu au lofa unakasirika. Samahani kama nimetumia lugha isiyopendeza lakini.

Kokolo looote sababu ni shekeli

Mwenye akili ataanza na figure sio blabla
 
Tusishangilie sana kwa sababu profit inapatikana baada ya kutoa:

* costs za mining,

* halafu wawalipe investors wote dividends zao (na ACACIA/BARRICK wana majority shares wakati TZ ina 16%)

* halafu kinachobaki ndicho kinachogawiwa 50-50 na serikali.

Sio kikubwa sana lakini ni hatua ya kujivunia.
Hahahahhahahahah. Boss rule of the game hujaijua. Muda utahukumu
 
Kwanza napenda kupongeza taarifa iliyotolewa leo baada ya majadiliano ya karibia miezi miwili na Barrick. Tumepata tulichopata na makubaliano mengine ambayo itabidi tusubiri kuona faida yake huko mbeleni. Nirejee kwenye mada, wote tunajua mwaka jana tuligomea msaada wa MCC wa dola 450m za bure kwa sababu hatukutaka msaada wa masharti. Ni kweli pesa zile tulizokosa kwa kushindwa tu kutumia busara ya kidiplomasia kwa makosa yetu ya kudharau demokrasia. Kwa bahati siku nazo hazigandi. Tukapata tume mbili zilizoshiba uzalendo zikachunguza wizi wa madini yetu hasa dhahabu. Tume zikafanya kazi kwa uzalendo kabisa na kutuletea data zisizoacha shaka kwa wizi tuliofanyiwa. Taasisi yetu ya mapato ikakokotoa wizi tuliofanyiwa ikakuta tunadai $190b zisizoacha shaka.

Leo hii wengine tunaukumbuka baadhi ya mambo tumepigwa na butwaa kwa kusikia mazungumzo ya wezi wetu wa Barrick yamefikia mwisho mwisho, lakini ni kama maamuzi halisi yameshatolewa. Maamuzi hayo ni pale mwizi wetu alipoona stahili yetu ni $300m tena za uaminifu kwamba yeye sio mwizi, na hizo atazitoa baada ya bodi yao huko London kuridhia! Watanzania tukalipuka kwa shangwe kwamba mwizi kanyoosha mikono. Wengine sisi tukaamua kwenda mbali zaidi na kujiuliza, iweje mwaka tu ulioisha tugomee $450m za bure kisha tuheshimu demokrasia, lakini tukubali $300m toka kwa mwizi tuliye na ushahidi nao mwaka mmoja mbele? Hapa hatunyoosheani vidole, lakini watanzania na waliochukua maamuzi hayo wametumia busara? Je hali hii ya kushindwa kupokea hela za bure kisha tuheshimu demokrasia na kupokea $300m toka kwa mwizi ipi ni maamuzi ya busara? Mawazo yoyote ni sawa kwani hii ndio demokrasia

CC: Paskali Mayalla, Quinine, Yehodaya, Jingalao, Mwigulu Nchemba, Zitto Junior
Mtaelewa tu..c ndo watawala wenu...me ngoja nitafute ugali wangu...

NOTE:: LAKIN AKIPATIKANA MTAWALA MZALENDO NA MUADILIFU. MSIACHE NITAARIFU NIMSAPORT....
 
Hii ndo main point huko kwengine kote umeandika pumba tuu,umeshasema pesa za masharti sisi tumekataa hayo masharti shida ipo wapi??Hizi pesa za ACACIA sio za msaada na wala sio za masharti ni haki yetu.
Wapi wameandika hizo pesa ni haki yenu? Acacia wametoa hizo pesa hili mfunge mdomo.
 
Hivi mkuu huwa unajiuliza kwa kina madhara ya misaada kutoka nchi fedha ya kimataifa?
 
Tujiulize nini sasa wakati huo ndio uwezo wetu wa kufikiri umefikia hapo. Tufanyeje kama Mungu hakutupa uwezo wa kufikiri zaidi ya hapo?
 
Uyu mtoa uzi atakuwa ni wale wa Peacock Hotel
 
Yes, Lissu was very right! Soma sheria ya madini uone ni madini gani ambayo mwelezaji anapaswa ku-declare kutoka kwenye concentrates.
Kamuulize Lissu kama he was very right mbona hawajatushtaki huko MIGA kama alivyosema?
 
Back
Top Bottom