Watanzania tumekosa mtetezi kwenye suala la umeme, sasa tunaangamia

Watanzania tumekosa mtetezi kwenye suala la umeme, sasa tunaangamia

Ndicho nachoweza kusema, machozi ya Watanzania kuhusu kero mbalimbali kwa sasa hayana mtu wa kuyafuta. Sio watawala, sio wapinzani, sio taasisi za kidini Wala yeyote yule. Watanzania tunapigwa bakora za ukosefu wa maji ya uhakika,kupanda kwa gharama za maisha(sukari) kupanda kwa bei za vifurushi vya simu, ukosefu kabisa wa umeme n.k .

kusema kweli kero zote za ukosefu wa maji, kupanda kwa gharama za maisha na uhuni tunaofanyiwa kwenye mitandao ya simu ni kama Watanzania tumekubaliana nayo. Ila hili la umeme kwa kweli hapana.

jamani umeme umekua kero na unatuumiza sana sisi Watanzania wa chini hakika tunaumia tunaumia tunaumia haswa!!!!

Jambo la kusikitisha ni kwamba naona viongozi sio wa upinzani Wala watawala wanaoguswa na hili tatizo, nchi iko gizani karibia mwaka mzima sasa lkn watu wako kimya kana kwamba hakuna kitu chochote kinacholisumbua taifa.

Viongozi wa upinzani nawambieni ktk jambo ambalo inabidi mlivalie njuga ni hili la umeme hakika litapa credit kubwa sana kuelekea mwaka wa uchaguzi 2025.

Watanzania hawana hamu Tena na huyu mama, sio vijijini wa mjini hakika nawambieni. Biashara haziendi watu wanapata hasara kweli kweli! Samaki wanaharibikia kwenye mafriji, nyama zinaoza mabuchani, wauza maziwa nadhani mnanielewa vzr vile mnapata hasara!

Wapi wanangu wa kuchomelea (welding) hasara mnayopata Sina haja ya kuwasimulia, mafundi aluminium, viwanda vidogo vidogo na vikubwa, watu wa saloon (Berber shop), mama ntilie nk. nk....!!
aisee hakika tunalia machozi ya samaki.

Sometime najiuliza hivi kweli viongozi wetu wanakaa kwa amani kbs maofisini kwao ili Hal, Watanzania wenzao wanateseka kiasi hiki na umeme?? Wasivyo na mishipa ya aibu Bado wanapita kudai Kodi kwenye biashara za saloon na mabucha ya samaki na biashara nyingine zinazo athiliwa Moja kwa Moja na ukosefu wa umeme, jamani chonde chonde mtatuuaaaaa.

Mwisho :sasa nimeuona umuhimu wa upinzani kwa usitawi wa nchi, kumbe upinzani ni wamuhimu sana hasa kwenye vyombo vya maamuzi tusichukulie poa! Tunahitaji upinzani dhabiti ktk nchi yetu. Leo hii mwaka unaenda kukata nchi iko gizani lkn husikii mbunge yeyote akisemea swala la umeme, husikii diwani yeyote akisemea swala umeme, hatusikii mwenyekiti Wala kigoda wote kimyaaa!! Kazi kubwa walioambiwa ni kusifu kisichokuepo.

Lkn naamini wapinzani wangekua kwenye vyombo vya maamuzi makelele Yao yangewashitua watawala wangetafuta namna ya kulishughulikia swala hili na Watanzania tungepata afueni.

Kumbuleni mpaka sasa hakuna mwenye jibu ni lini mgao (Mimi nauita ukose wa umeme kbs) tutaondokana nao.

Poleni waganga njaa wenzegu kwa bakora za mgongo hakika chozi letu ni lasamaki.

By kinyozi wa saloni mtoni mtongani.
Kwenye maandamano ulikuwepo ?
 
...ukinunua sola, au ukafunga motor mbili zinazotegemeana, utapata infinity electric charge(umeme usio na kikomo). Utasahau mambo ya TANESCO, nakwambia watakusanya nguzo wauze mbao
Ni kweli usemalo mkuu lkn je ni Watanzania wangapi wenye uwezo wa kununua hizo solar?? Hao wauzaji wa solar nao wamepandisha bei karibia mara Tano ya bei ya awali baada ya kuona Kuna shida ya umeme.. bei ya jenireta kwa sasa ndo usiseme.

Kweli Watanzania tunateseka kwenye nchi yetu aisee, kumbe zile takwimu za kuzidiwa furaha na somalia ni kweli bana..
 
Ni kweli usemalo mkuu lkn je ni Watanzania wangapi wenye uwezo wa kununua hizo solar?? Hao wauzaji wa solar nao wamepandisha bei karibia mara Tano ya bei ya awali baada ya kuona Kuna shida ya umeme.. bei ya jenireta kwa sasa ndo usiseme.

Kweli Watanzania tunateseka kwenye nchi yetu aisee, kumbe zile takwimu za kuzidiwa furaha na somalia ni kweli bana..
Usiseme nchi yetu. Sema nchi yao ( wanasiasa) wanaotengeneza haya matatizo.
 
Umejichanganya mkuu! Wapinzani wanapigania;
  • Uraia pacha wa watoto wao
  • Ruzuku, inaingia mifukoni mwao
  • Nafasi za mamlaka/madaraka

Uwe muungwana tu kusema, aliwahi kuwepo mtu aliyewahi kukerwa na hizo kero na akaonesha nia ya dhati kuzitatua, SIO WAPINZANI.

Unajua kuwa sukari imepanda, kisa mvua? Wapinzani wamefanya nini?

Unajua kuwa umeme ni shida, unaambiwa matengenezo, mara mvua hakuna, unakubaliana nayo hayo? Wapinzani wamefanya nini?

Unajua kuwa mamlaka za maji zimefeli vibaya, wapinzani wako kimya!

Unayo taarifa, nauli zimepanda, wao kimya?

Unajua kuwa hatuna dawa, hatuna chakula cha akiba? Bashe anakanya twende, wao wanafanya nini?

Ni mengi mno ya hovyo nchi hii, CCM wanatengeneza matatizo kwaajili ya maslahi yao...wapinzani wanapambania maslahi yao.

Niambie, maandamano ya kwanza kabisa waliyokusudia kufanya, dhima yake ilikuwa nini?
Nakubaliana kwa uchache na mawazo Yako. Lkn point yangu kubwa ni kwamba kitendo Cha serikali kukosa ukosoaji wa maana hasa kwenye vyombo vya maamuzi wanajisahau!!!! Hata kama wapinzani Wana maslahi Yao mengine lkn mm naamini wangelikua bungeni na sehemu nyingine za maamuzi lazima wangelipigia kelele sana swala hili. Huu mgao hata kipindi cha kikwete haukua hivi bana
 
Hivi tuliambiwa kikomo cha shida ya umeme ni lini vile, naomba nikumbushwe.
Tulidanganywa miezi 6 lkn sasa mwaka unaenda kukatika na hakuna uelekeo wowote ni lini mgao utaisha. Wanafanya kutugeuzia maneno tu.

Kipindi cha kiangazi wakesema shida ni mvua nyanzo vimekauka ndio maana umeme hakuna, mungu si athumani kashusha mvua ya kutosha maji Kila mahali he!! Wakageuka Tena oohh! Mvua zimezidi ndio maana hakuna umeme!! Mungu akasema sio kesi ngoja nipunguze mvua Bado umeme hakuna. Kwa style hii furaha utaitoa wapi wewe mtanzania mwenzangu??
 
Pengine kuna mikataba na wauza soral sasa ili wauze serikali isitoe umeme.maana unaambiwa mtambi umewashwa harafu keshi umeme bado haupo.
Watanzania tugomee kulipa Kodi! Unakuja kunidai Kodi Mimi kinyozi wa saloon hiyo pesa ya kukulipeni naitolea wapi????
 
Nakwambia ni balaa watu wanamapele ya joto kama wamemwagiwa upupu!! Joto Kali na hakuna umeme wa kuwasha hata ki feni.
 
Gharama zote za nini hizo?
Unajua nimekuja kugundua shida ya umeme/ ukosefu wa umeme tusilaumu shirika la Tanesco, shida iko kwa viongozi wetu wa kisiasa hasa kiongozi mkuu. Ukituliza kichwa vzr utanielewa. Mimi nahisi Tanesco wanafanya kazi kwa maelekezo ya mtu au watu flani. Watanzania tujiulize kwa Nini shida ya umeme inakuepo au kutokuepo kutegemea na kiongozi anaengoza nchi???

Kwa Nini kipindi cha magu hakukua na mgao then now mgao ni wakutisha ilihali shirika ni lile lile???

Mzee magu alifanya Nini kuhakikisha Kuna kuwa na umeme wa uhakika ambacho huyu mama hawezi kukifanya?? Tujiulize kwa pamoja
 
Back
Top Bottom