Watanzania tumekosa mtetezi kwenye suala la umeme, sasa tunaangamia

Watanzania tumekosa mtetezi kwenye suala la umeme, sasa tunaangamia

Sijasikia bado tatizo sugu la umeme na maji ninaletwa kwenye jukwaa la kusikiliza kero za wananchi la Mh Makonda.
au tatizo halipo sehemu anazopita? au watanzania hawajui ni tatizo lao kubwa linalo wakabili?
 
Hata hizo kodi za majengo walizozipitishia kwenye kwenye luku tutazilipaje sasa
Kwa mfano umenunua umeme Unaanza kutengeneza bidhaa zako katikati ya uzalishaji ghafla umeme kwao, bidhaa zinaharibika hasara juu ya hasara, aisee! Inatia hasira
 
Naomba chadema na vyama vyote vya upinzani wakae kimya!


Mtanzania sio wa kutetea kabisa


Acha tuteseke Hadi tukome
 
...ukinunua sola, au ukafunga motor mbili zinazotegemeana, utapata infinity electric charge(umeme usio na kikomo). Utasahau mambo ya TANESCO, nakwambia watakusanya nguzo wauze mao
La Sola linaeleweka, hili la motor mbili unafanya fanyaje mkuu, naomba uzoefu wako please.
 
Kero hizo zitaisha mpaka pale watanzania wenyewe sio upinzani wala watawala namaanisha watanzania wenyewe hususa WATANGANYIKA WENYEWE watoke majumbani waingie barabarani na kupinga haya mabaya yanayoendelea bila woga. Asante.
Kwa hiyo unavyotoka ndani mwako na kukutana na wenzako barabarani hayo tayari ni maandamano?

Hauwezi kufanya mambo hayo bila agenda, organizer au mastermind bhana.

Wanaoweza kushawishi ni wasomi, makanisa/madhebu ya dini pamoja na wanasiasa.

Lakini Sasa wote hao washalambishwa asali hakuna wa kuorganize kitu kama hicho.
 
Umejichanganya mkuu! Wapinzani wanapigania;
  • Uraia pacha wa watoto wao
  • Ruzuku, inaingia mifukoni mwao
  • Nafasi za mamlaka/madaraka

Uwe muungwana tu kusema, aliwahi kuwepo mtu aliyewahi kukerwa na hizo kero na akaonesha nia ya dhati kuzitatua, SIO WAPINZANI.

Unajua kuwa sukari imepanda, kisa mvua? Wapinzani wamefanya nini?

Unajua kuwa umeme ni shida, unaambiwa matengenezo, mara mvua hakuna, unakubaliana nayo hayo? Wapinzani wamefanya nini?

Unajua kuwa mamlaka za maji zimefeli vibaya, wapinzani wako kimya!

Unayo taarifa, nauli zimepanda, wao kimya?

Unajua kuwa hatuna dawa, hatuna chakula cha akiba? Bashe anakanya twende, wao wanafanya nini?

Ni mengi mno ya hovyo nchi hii, CCM wanatengeneza matatizo kwaajili ya maslahi yao...wapinzani wanapambania maslahi yao.

Niambie, maandamano ya kwanza kabisa waliyokusudia kufanya, dhima yake ilikuwa nini?
Unataka wakusemee kila kitu wakati huo wewe umekaa kwako.Hoja tu ya nchi kua na katiba mpya ambayo ni bora inajibu kero zote unazoziona hawajazisemea.panua hiyo akili utaona nchi ilipokwama ni wapi badala ya kulaumu wasio husika wakati huo wakijitokeza kusema unawananga.
 
Kwa hiyo unavyotoka ndani mwako na kukutana na wenzako barabarani hayo tayari ni maandamano?

Hauwezi kufanya mambo hayo bila agenda, organizer au mastermind bhana.

Wanaoweza kushawishi ni wasomi, makanisa/madhebu ya dini pamoja na wanasiasa.

Lakini Sasa wote hao washalambishwa asali hakuna wa kuorganize kitu kama hicho.
Hali haijawa mbaya sana, maji yakifika shingoni akili itakuja yenyewe. Tuendelee kusubiri.
 
Unataka wakusemee kila kitu wakati huo wewe umekaa kwako.Hoja tu ya nchi kua na katiba mpya ambayo ni bora inajibu kero zote unazoziona hawajazisemea.panua hiyo akili utaona nchi ilipokwama ni wapi badala ya kulaumu wasio husika wakati huo wakijitokeza kusema unawananga.
Ume-panick bingwa, kuwa Chadema sio kosa wala hupaswi kuji-defense kiasi hiki!

Nani kakuambia Katiba mpya inatoa majibu ya matatizo ya watanzania walio wengi?
- Rather inatatua kero za Chadema kukosa priviledges za kukwapua kama sisiemu.

Kenya wana Katiba mpya, kawaulize inawasaidiaje!
 
...ukinunua sola, au ukafunga motor mbili zinazotegemeana, utapata infinity electric charge(umeme usio na kikomo). Utasahau mambo ya TANESCO, nakwambia watakusanya nguzo wauze mbao
Gharama ni kiasi gani?
 
Hivi shida ni nini jamani?kuna kitu kinaendelea upande wa umeme,kuna mchezo mchafu,maana ,kwaninj kipindi cha kiangazi mgao,kipindi cha mvua mgao,sababu wanazotoa ni sababu za kishetani,haziingi akilini,wanataka wafanye hii ndo iwe style,msipoongea na kuwakumbusha hali itakuwa hivi maisha yoote,watuambie sababu zenye mashiko ili tuwaamini
Lengo lao wanataka watuzoeshe kama walivyotuzoesha matatizo mengine! Hawa ni wakuwakemea kama mapepo yanavyokemewa.
 
Back
Top Bottom