Watanzania tumsaidie kumtajia viongozi wasiofaa Rais anapokwenda kuisuka upya Serikali

Watanzania tumsaidie kumtajia viongozi wasiofaa Rais anapokwenda kuisuka upya Serikali

Naunga mkono hoja ya Emmanuel Misalaba kwa 100%
1. J. Makamba.
2. Madilu system.
3. Ridh Moko.
4. Nape
Hawa wote Mama fyeka kabisa, hawatakusaidia kwa lolote.
hawa wote wanampaka Bimkubwa mafuta kwa mgongo wa chupa, wanakwamisha mipango ya ujenzi wa miundombinu, wanamdharau Bimkubwa sababu ni Rais mwanamke kutoka visiwani kusiko na elimu, wanamng'ong'a sana, ni wanafki , ni wazandiki wanamuona hatoshi wanautaka urais wake , wanatamani hata leo ajiuzulu wakalie kiti, wanaanzisha mambo ya kumgombanisha bimkubwa na wapiga kura wake, wanakata umeme makusudi ili kuudhi raia wamchukie Bimkubwa na kuiba pesa za matengenezo ambazo zinawekwa benki za kampeni ya urais, wanazunguka mikoani na mitungi na kuelezea tozo kumbe lengo ni kujijenga kisiasa, hawa ndo ile kikulacho kinguoni mwako mvunja nchi mwananchi, hawa ni nyoka wanaofugwa ikulu@@@
 
Naunga mkono hoja ya Emmanuel Misalaba kwa 100%
1. J. Makamba.
2. Madilu system.
3. Ridh Moko.
4. Nape
Hawa wote Mama fyeka kabisa, hawatakusaidia kwa lolote.
Eti Madilu System [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
You are very wrong about this lady!, hebu msikilize hapa




P
Mkuu Pascal kwani sisi tunahitaji Mawaziri waongeaji maneno matupu?
Tunataka watu wa action,siyo porojo!
Kijaji hapana,labda jinsia imembeba ila kiutendaji hamna kitu!
Kwa kifupi ata anayewateua na yeye uwezo wa kuongoza taifa lililojaa vibaka la Tanzania bado sana.
Tungekuwa watu serious na CCM serious kama ANC ya South Africa huyu Mama angekuwa out ila kwakuwa sisi watanzania ni mabingwa wa unafiki wacha twende tu.

Hii Biashara ya kukopa Ili ulipe deni jinginge lililoiva,siyo finance pyramid scheme,yaani unakopa mkopo mkubwa Ili ujenge madarasa badala ya kukopa tuwekeze kwenye kilimo cha kisasa Ili tulishe bara la Africa na pesa inayopatikana ndiyo tuboreshe miundombinu yote nchini!
 
Aondoe wote, tunataka majina mapya kabisa, hivi kwani nchi hii imeishiwa watu?
Utashangaa kama wengine ila ndio hivyo
Kuna mwingine eti amekataa kuhama baada ya kuombwa x3
Na bado yupo kazini na wa kumtoa hamna
Wamezoeana sana wamekuwa kama ndugu na washkaji mpaka wanakera

Hebu angalia hili na wapo wengi kama hawa
Screenshot_20221224_163133_Instagram.jpg
 
angeniuliza siku ya leo ningemjibu hivi: Tunavyosherehekea kuzaliwa Yesu hatusherehekei kama sherehe inamaana tuanze kufanya mema kama tulikuwa tunaiba tuwazinzi tuwalevi tuwaongo tuwanafki hatuheshimiani n.k basi tubadilike tutende wema zaidi, mambo yetu yabadilike yawe kwa uzuri zaidi. Undugulization ktk nafasi za teuzi na nafasi za kazi mbalimbali serikalini inatakiwa zikome kabisa...kama viongozi wengi ni wezi, waongo, wanafki n.k alafu wakitaka watoke madarakani wanawarithisha watoto wao maana yake tunalea dhambi katika taifa..dhambi hiyo haiwezi kuisha, uizi hauwezi kuisha, uongo hautaisha, uzinzi n.k havitakwisha kwa maana wanarithishana yaani damu ni ile ile..damu ya uizi uongo ni ile ile....ANGEKUWA ANATEUA DAMU MPYA KABISA KATIKA TEUZI ZAKE..ZISIWE NA UNDUGU IWE KAMA LIMEZALIWA TAIFA JIPYA KABISA..BWANA YESU AANZE NALO..kwenye watanzania milioni 60 huwezi kukosa watu elfu 10 wa kukusaidia kufanya kazi kwa uadilifu uaminifu na ukamilifu. Kwasasa serikali yetu haijazaliwa upya kama tunavyosherehekea hivi leo...walioko serikalini wengi wamekalili maandiko tu ya kusema "tunawatakieni heri na sikukuu njema watanzania wote" ila moyoni kwao kumejaa UBINAFSI, UONGO, UNAFKI, UIZI, UZINZI, KUTOHESHIMU, UBAGUZI, ULEVI N.K

Heri ya siku ya leo na Mungu awatengeneze ninyi na vizazi vyenu muwe wenye kufaa kila mahali na kila mulitendalo ameen!
 
Hawa makosa yao ni yepi ili tuyajue wote
Januari Makamba kosa lake ni issue ya umeme, anawaweka kwenye wakati mgumu sana wafanyabishara wa kawaida hasa watu wenye kuendesha maisha kwa kutegemea saloon za kike na kiume, watu wa welding, watu wa juice mbalimbali, watu wenye kufyatua tofali, wazalishaji wa barafu nk nk.
Makamba amekuwa na sababu kila iitwapo leo, uwezo wake umeishia pale.

Nape nauye ameshindwa kuplay upande wa wananchi, yuko upande wa wamiliki wa mitandao, leo mabando bei iko juu na huduma zao ni mbovu.

Mwingulu Nchemba amekosa ubunifu kwenye wizara ya fedha, anakuja na vitu vya kuumiza zaidi raia wa kawaida, Tozo mbalimbali, anashindwa kutafuta vyanzo madhubuti kwa ajili ya maendeleo ya nchi.
Hawa makosa yao ni yepi ili tuyajue wote
 
Ni kweli kabisa huyu mama hayupo upande wa raia walio wengi, jeshi limweke kando apewe mwenye uwezo na uzalendo na nchi hii
Kwa jinsi sirikali ilivyoshindwa kutatua changamoto za wananchi,

Nashauri akae pembeni Ili aje mwingine kuisuka Serikali mpya.

Mwaka mpya na mambo mapya.

Ni ushauri tu lakini!!!
 
Waziri wa Afya kwa kutoanzisha University teaching hospital nchini.
 
msukaji tu hafai
basi vile hatuna uwezo wa kumwondoa

ondoa mwigulu, simbachawene, mhagama, na yule mama mweupe muhaya waliosema kaazaa na mwenda zake
 
Back
Top Bottom