Mkuu nakumbuka hii imetokana na sheria mpya ya madini kama ulivyosema ingawa sina hakika kama tulifikia majadiliano na makampuni ya gesi, naona nguvu nyingi zilielekezwa kwenye madini mengine kama dhahabu na Almasi.
Mkuu
Hakimu Mfawidhi , sheria ilisema extractive industry yote!, chochote kinachochimbwa kwenye ardhi ya Tanzania, 16% ni mali ya Watanzania ambao ndio wenye ardhi hiyo. Kwangu tatizo la sheria hii ni sheria mpya, wakati inanatungwa, tayari tulikuwa na mikataba ya zamani ya umiliki wa asilimia 100% chini ya 100% kwa mwekezaji.
Baada ya Bunge letu kutunga sheria mpya ya madini, niliuliza
Wanabodi, Kwanza naunga mkono marekebisho ya sheria hizi kufanyika, kwa sababu yanafanyika kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa na maslahi ya Watanzania badala ya maslahi ya wawekezaji, japo siungi mkono miswada hii kuletwa kwa hati ya dharura kwa sababu tayari kuna mikataba mingi iliyopo...
Wiki iliyopita, nimezungumza na Waziri Dotto Biteko, amekiri kuwa serikali ina negotiate na wawekezaji na wote wamekubali kutekeleza sheria hii mpya ya 16% free carried shares
Jambo la pili ni kwamba hizo 16% free carried shares ni class B shares ambazo kimsingi hazina uzito mkubwa sana kwenye kampuni.
Tuendelee kujipa matumaini ila ukweli ni kwamba we are fucked up big time.
Elimu ya shares inahitajika sana Tanzania. Hizo class B shares ni shares kamili zina hadhi sawa na class A shares, the only thing ambacho hazina ni fixed and non transferable, yaani haziwezi kuongezeka wala kuuzwa. Huku kutokujua tofauti ya class A shares na class B, sikulaumu wewe, hata wachumi wetu wa UDSM akiwemo
Zitto , hizi class b shares alikuwa hazijui, na alipandisha bandiko hili
Zitto: Makubaliano ya Serikali na Barrick Gold changa la macho
na mimi ambaye sio mchumi bali muelimishaji umma, nilijitolea kumuelimisha hapa.
Wanabodi, Huu ni muswada wa makala ya gazeti. Nimepata fursa kuendeleza zile makala zangu za "Kwa Maslahi Ya Taifa", ambazo ni makala elimishi katika nyanja za kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa lengo la kulisaidia taifa letu lisonge mbele. Makala ya leo inazungumzia kazi ya vyama vya upinzani...
Na kwa faida ya wale wasio na time to follow links, naomba nilirudie lile darasa
Zitto amesema:Tanzania kupewa Hisa 16% za daraja B lakini Watanzania kunyimwa umiliki wa 30% kupitia Soko la Hisa la DSE
Ni kweli kuwa Serikali itapewa hisa za bure 16% kwenye Kampuni tanzu zote za Acacia hapa nchini kama tulivyoambiwa na Serikali. Lakini hisa hizo ni za Daraja la B ambazo ni hisa dhaifu kulinganisha na zile za Daraja la kwanza. Hisa hizo haziruhusiwi kuuzwa, hazina kura kwa masuala fulani fulani ya Kampuni na huwezi hata kuziweka kama dhamana ya mikopo. Hata mgawo wa gawio hisa hizi hupata baada ya wale wa daraja A kulipwa kwa ukamilifu.
Licha ya makubaliano haya ya hovyo na yasiyo na tija, Serikali yetu imetoa ‘waiver’ (msamaha) kwa Barrick kutoorodhesha hisa kwenye Soko la Hisa la Tanzania. Sheria ya Madini ya mwaka 2010 (Wakati wa Waziri William Ngeleja) na Kanuni zake iliweka sharti kwamba ni lazima makampuni ya madini yauze 30% ya hisa kwa Watanzania kwenye soko la Hisa la Tanzania.
Makubaliano ya Mei 2019 kati ya Barrick na Serikali ya Tanzania yametoa msamaha kwa Barrick kutekeleza sharti hilo la kisheria. Uamuzi huu unavunja sheria za nchi, ni hujuma kwa Watanzania kumiliki maliasili zao na ni ukosefu wa maarifa ya kiuchumi kwa kiwango kisichomithilika wala kuvumilika.
P
Mimi Nimejibu: Hili la hisa za daraja B ni kweli lakini sii kweli kuwa Watanzania tumenyimwa umiliki wa 30% kupitia DSE!.
Hizi hisa aslimia 16 za Tanzania, ni free carried shares, tumepewa bure, na kote free carried shares huwa haziuzwi ila sii kweli kuwa hazina voting rights. Pia sii kweli kuwa Watanzania tumenyimwa umiliki wa 30% kupitia DSE!.
Naomba hapa ikumbukwe, shares zinazouzwa ni shares za Acacia zinazo trade kwenye London Stock Exchange tuu, hata yale mambo ya PUSU ni mambo yao, sijasikia lolote kuhusu shares za Acacia zinazo trade kwenye DSE, hivyo business ya hisa za Acacia ndani ya DSE zinaendelea as usual.Hata baada ya sale kukamilika, hivyo kampuni mpya italazimika kuuza 30% ya hisa zake kwenye DSE na Watanzania wenye fedha, watakuwa free kununua hisa hizo kwenye soko.
Tukija kwenye voting rights, sii kweli kuwa Tanzania hatuna voting rights, bali ni kawaida kwa free shares zote hazina voting rights ya pro rata ya share to shares bali tuna voting rights za block shares. Sisi Tanzania wenye free carried shares za 16%, serikali yetu iteteua mjumbe mmoja wa bodi ambaye ni Mtanzania, ataingia na kuwa mjumbe wa bodi ya hiyo kampuni mpya, kwa zile asilimia 16% za shares zetu na ndani ya kikao cha bodi, atakuwa na voting righs za kupiga kura 1 as a block vote kuwakilisha zile shares 14, wakati wajumbe wengine wa bodi, watakaowakilisha zile subscribed shares za asilimia 84%, wanatakuwa na voting rights ya votes 84 kwa uwiano wa share to shares votes pro rata according to shares subscription. Hivyo ndani ya bodi ya hiyo kampuni Mtanzania atakayeingia humo, atakuwa anapiga kura moja kuwakilisha the block ya zile shares zetu 16 za bure, na katika mgao wa faida, sii kweli kuwa tutapata mgao baada ya wale wengine, huu ni uongo!, Tanzania tunagaiwa mgao sawa kabisa wa faida kwa mujibu wa shares hizo.
Kwa wasio jua kuhusu shares za group A na group B shares za group A ni shares za watu walio invest kwa kutoa fedha zao kununua shares, yaani subscribed shares, na shares group B ni shares za heshima, shares za hisani zinazotolewa bure, shares hizi za hisani haziruhusiwi kuuzwa, wala kuwa disposed or transferred na zina block votes rights. Hili hufanyika kwa makampuni kuwapa hisa za heshima land owners, mfano UAE, hakuna foreigner anayeruhusiwa kumiliki ardhi, ardhi yote ni ya wazawa, hivyo investor akija lazima aingie ubia na wazawa mzawa anatoa land, investo ana jenga, kama alivyofanya Rugemalila kwenye IPTL alitoa ardhi yake na kupewa 30 m% ya shares, IPTL ikaikwa kwa PAP, Ruhemalila akalipwa shares zake, akagawa fedha zake, sasa anateswa bure bila kosa lolote!.