Pre GE2025 Watanzania tunataka kura zetu zihesabiwe wazi wazi

Pre GE2025 Watanzania tunataka kura zetu zihesabiwe wazi wazi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Babu Wassira anahutubia watu na kuwaambia kwamba Watanzania wanataka huduma, siyo Katiba Mpya.
Je, ataweza kutamka hadharani kwamba Watanzania hawataki Kura zao zihesabiwe kwa uwazi?
Ana akili siyo km babu yako ambaye hana mchango unaojulikana ktk hili Taifa
 
Wakishaiba kura wanaenda makanisani na misikitini bila aibu.
Na huko Makanisani na Misikitini wanaenda kutoa "mabaki" yaliyobaki baada ya rushwa kama Sadaka!
Wanadiriki kumpelekea Muumba mabaki!
Tupaze sauti zetu.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Uko sahihi Vessel.
Ndiyo sababu ni muhimu sana kuoaza sauti, ndani na nje ya mipaka yetu kwamba TUNATAKA KURA ZETU ZIHESHIMIKE.
Ili Kura zetu ZIHESHIMIKE, tunataka zihesabiwe kwa Haki na kwa Uwazi.
Kwa Sheria hizi hizi na Kanuni za Uchaguzi hizi hizi.
Nyie nyumbu siasa zenu zinaishiaga humu JF
 
Na kwanini mtu asitake uwazi,yeye ni nani?
Mimi nasemaje ikibidi kila chama wakati wa kura kiwe na upande wake tuone hawa ni ccm na hawa ni Chadema ama Act
Tupaze sauti ili wayasikie hayo uliyoandika.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
CCM cama tawala hakitaki kwasabb kitashindwa mapema asubuhi.
Kwa kuwa Kura zinahesabiwa mafichoni, aliyeshindwa anapata wasaa wa kugeuza matokeo.
Kura zikihesabiwa kwa Uwazi, hawataweza kubadilisha matokeo.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
  • Thanks
Reactions: G4N
We ndio watanzania? Watanzania wana wawakilishi wao wa kuwasemea, tafuta fursa ya kwenda kuwawakilisha hao watanzania kwanza
Mimi na wewe, na yeye na yule ndio Watanzania.
Watanzania tusio Wanachama wa Vyama vya Siasa, tunawakilishwa na nani?
Hupendi sauti zetu zisikike?
Zamani kabla ya 'Social Media' tusingepata pa kusemea.
Sasa hivi tunasema na tunasikika.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Ana akili siyo km babu yako ambaye hana mchango unaojulikana ktk hili Taifa
Kiburi cha kumkashifu Babu yangu kwamba hana mchango katika Taifa hili kinaletwa na TABIA YA KUDHARAU WATANZANIA ambao Kura zao ndizo zinawapeleka Wabunge Mjengoni na Rais Ikulu.
Kura zetu zikihesabiwa hadharani, kwa uwazi, Viongozi wote watawaheshimu Watanzania wote, akiwemo Babu yangu.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Nyie nyumbu siasa zenu zinaishiaga humu JF
Uko sahihi kutukana kwa sababu umejiaminisha kwamba Wapiga Kura wasio na Vyama, ambao wanakaa kimya, akili zao ni sawa na Nyumbu wa Mbuga ya Serengeti.
Sasa tunataka tuamke.
Tunaanza kupaza sauti zetu, mpaka tuheshimike.
Tuombwe radhi kwa kutuita Nyumbu.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Nimesoma kwa makini ilichoandika.
Bandiko lako limeegemea upande wa Mfumo wa hivi Vyama vyetu vya Kisiasa.
Na hicho ndicho wanachotamka Watawala.
Kwamba, Wananchi wa kawaida, ambao ndio Wapiga Kura, WAJITENGE NA MADAI YA VYAMA VYA SIASA, ili kesho na kesho kutwa Babu Wassira aende kwenye Majukwaa na kuwaambia watu kwamba hayo ni "mambo ya Waoinzani".
Hoja yangu mimi ni kuhusu SISI WAPIGA KURA, tena wengi wetu, (majority), tusio Wanachama wa Chama chochote cha Siasa.
Nimemskia Mchambuzi wa Siasa na Ujasusi, ndugu yetu Evarist Chahali, akisema kwamba Asilimia 80 ya Wapiga Kura, siyo Wanachama wa Chama chochote cha Siasa.
Kundi hilo ndilo tunaotakiwa kupaza sauti zetu.
Kwenye Vituo vya Kupiga Kura, CHADEMA wanakuwa na Wakala.
CCM wanakuwa na Wakala.
Sisi tusio na Wakala, tena ambao ndio MAJORITY, haki yetu inalindwa na nani?
Mlinzi pekee wa Haki yetu ni KURA ZETU KUHESABIWA KWA UWAZI, na zitangazwe kuwa rasmi.
Tupaze sauti zetu.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
Mkuu acha kujitoa ufahamu, huna chama halafu unaenda kuchagua wagombea wa vyama tu?! Kungekuwa na mgombea binafsi ungekuwa na hoja. Pambana upate mgombea binafsi ili uwe nje ya huu uchaguzi wa kihuni wa kuchagua wagombea wa vyama. Hao mawakala wa vyama vya upinzani huweza kufanywa lolote na vyombo vya dola na wasifanye lolote. Rudi hapa nchini uje uone hizo nadharia zako kama zinafanya kazi.
 
Mkuu Smart911,
Wametuchukulia powa kwa muda mrefu sana mpaka wamejisahau.
Tukiamua kupaza sauti zetu, zikaenea Tanzania nzima, mpaka zikavuka Mipaka ya Nchi yetu, watasikiliza.
Zama hizi za Social Media, ndiyo wakati wa wasio na sauti.
Tupaze sauti zetu.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
Tatizo tume ya kutangaza matokeo wote ni makada wa chama tawala...
 
Japhet gombe,
Kuna usemi kwamba, "Wenye uelewa lakini wakaacha kupiga Kura, wanatawaliwa na wasio na uelewa, waliopiga Kura".
Huu ni usemi sahihi sana.
Na Watawala wanatumia mwanya huo kujazia Masanduku ya Kura za wasiojitokeza kuweka "Alama ya ✓" kwenye Majina yao.
Tafsiri hapa ni kwamba, usipoenda kupiga Kura, umeruhusu Kura yako ipigwe na usiyemtaka.
Tusiruhusu hali hali.
Wala tusikubali kukatishwa Tamasha na hawa WEZI WA KURA ZETU.
Tupaze sauti.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
Uende usiende wao watajaza tu afadhali uwaachie tu
 
Njia pekee ya Watanzania kuheshimiwa na Wawakilishi wetu ni kuhakikisha kwamba Kura zetu zinahesabiwa katika mazingira ya uwazi kwenye kila Kituo cha Kupigia Kura, na matokeo hayo yawe rasmi.

Tabia ya kufukuza Wapiga Kura kwenye Vituo vya Kupiga Kura ikomeshwe ili Mshindi halali ajulikane.
Hili halihitaji Azimio la Bunge wala Mswada wowote wa Sheria.

Wananchi tukiamua na kushinikiza, hili linawezekana kufanyika kwenye Uchaguzi Mkuu Novemba mwaka huu 2025
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
CCM wakisikia hayo maneno wanatetemeka sana.
 
Mkuu acha kujitoa ufahamu, huna chama halafu unaenda kuchagua wagombea wa vyama tu?! Kungekuwa na mgombea binafsi ungekuwa na hoja. Pambana upate mgombea binafsi ili uwe nje ya huu uchaguzi wa kihuni wa kuchagua wagombea wa vyama. Hao mawakala wa vyama vya upinzani huweza kufanywa lolote na vyombo vya dola na wasifanye lolote. Rudi hapa nchini uje uone hizo nadharia zako kama zinafanya kazi.
Maneno yako ni mazito.
Lakini yana dalili za kukata tamaa.
Wagombea ni Vyama.
Wapiga Kura ni sisi sote.
Tatizo letu Nchini, walioko Madarakani hawataki Tume Huru, hawataki Katiba Mpya, na hawaoni aibu kujinasibu na hali hiyo.
Sauti ya Wapiga Kura inao uwezo wa kufikisha madai haya mpaka Nje ya Nchi, na kwenye ulingo wa Kimataifa, shinikizo linaweza kuwarudia hawa Watawala wetu.
Kupaza kwetu sauti, kutaenda sambamba na jitihada za Vyama vinavyodai Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi.
Sauti za Wapiga Kura zitakuwa CHACHU kwenye jitihada zilizopo za kudai mabadiliko.
Kumbuka Mtawala aliyepo Madarakani haoni aibu kuwaengua Wagombea wa Vyama vingine na kubakiza wale wa Chama chake tu.
Kundi pekee ambalo haliwezi kuenguliwa ni sisi Wapiga Kura.
Tupaze sauti.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Tatizo tume ya kutangaza matokeo wote ni makada wa chama tawala...
Tatizo kubwa zaidi ni kwamba Wapiga Kura wanaridhika anapotangazwa Mgombea ambaye hakuchaguliwa kihalali.
Kura zikihesabiwa kwa uwazi, huyo anayetangaza Matokeo atakwama KUBATILISHA ushindi wa aliyeshinda.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Uende usiende wao watajaza tu afadhali uwaachie tu
Ukiwaachia ni sawa na kuacha Mlango wazi ili Mwizi aje KUIBA kiulaini.
Tufunge Milango kisawasawa, ili Mwizi akija, apambane kuuvunja.
Anaweza kukamatwa kabla hajatimiza azma yake ya kishetani.
Tupige Kura.
Na Kura zetu ZIHESHIMIKE.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Back
Top Bottom