Pre GE2025 Watanzania tunataka kura zetu zihesabiwe wazi wazi

Pre GE2025 Watanzania tunataka kura zetu zihesabiwe wazi wazi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Asante!zipigwe hadharani,zitumbukizwe kwenye maboksi yanayoonyesha ndani,zihesabiwe hadharani,zitangazwe hadharani na mshindi atangazwe mbele ya kadamnazi ya walipiga kura,tuachane na mabungutu soksini.
Sahihi kabisa 'kitowowoti'.
Wapiga Kura tumejisahau kwa muda mrefu sana juu ya umuhimu na uzito wa Kura ya kila mmoja wetu.
Sasa tuamke.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Mkuu, CCM wamezoea kula vibudu, kwa uzoefu huo vya kuchinja kamwe hawataviweza. Kuokoteza mizoga ndiyo ibada na jadi yao.
Ukimya wetu umewafanya waamini kwamba kula vibudu ni haki yao.
Sasa tuwaambie, tena kwa kupaza sauti, kwamba tunataka Kura zetu ZIHESHIMIKE.
Na namna ya kuziheshimisha ni kuhesabiwa kwa Uwazi.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Kura zihesabiwe hadharani pia matokeo yatangazwe hadharani baada ya kupata mgombea aruhusu kura zichomwe hakuna kuondoka nazo kuondoka nazo Ndiyo kuziiba kwenyewe, kikikiki nilisema tutapata suluhisho tu na suluhisho Ndilo hilo

Zoezi hili litapunguza kesi za wagombea kwenda mahakamani

Sikuhizi taarifa zinaingizwa kwenye mfumo wa kidigitali hakuna mbamba, yaani mfumo utaona matokeo yote ya siku hiyo
Tupaze sauti mpaka kieleweke.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Njia pekee ya Watanzania kuheshimiwa na Wawakilishi wetu ni kuhakikisha kwamba Kura zetu zinahesabiwa katika mazingira ya uwazi kwenye kila Kituo cha Kupigia Kura, na matokeo hayo yawe rasmi.

Tabia ya kufukuza Wapiga Kura kwenye Vituo vya Kupiga Kura ikomeshwe ili Mshindi halali ajulikane.
Hili halihitaji Azimio la Bunge wala Mswada wowote wa Sheria.

Wananchi tukiamua na kushinikiza, hili linawezekana kufanyika kwenye Uchaguzi Mkuu Novemba mwaka huu 2025
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
Labda raia wawe na silaha hasa za moto, ifahamike uporaji wa chaguzi zetu unasimamiwa na vyombo vya dola ambavyo vinamiliki silaha za moto.

Ifahamike ccm haina uwezo tena wa kushinda kwenye uchaguzi halali. Hivyo tusitarajue chaguzi za haki tena bila machaguko kwanza, ama mapinduzi ya kijeshi.
 
Unaweza isvyo sahihi,

Kwamba kura fake zihesabiwe Kwa uwazi?

Hukujifunza uchaguzi wa Serikali za mitaa?

Rudi andika UPYA kwamba,

Tunataka Tume huru na Katiba mpya kabla ya Uchaguzi wa October,

Tupate Sanduku la kura lisilonajisiwa.

Ndipo tupige kura na zihesabiwe Kwa uwazi.

Na bila Tume huru ya Uchaguzi, uchaguzi utayeyuka.

Sijui umeelewa?
 
Njia pekee ya Watanzania kuheshimiwa na Wawakilishi wetu ni kuhakikisha kwamba Kura zetu zinahesabiwa katika mazingira ya uwazi kwenye kila Kituo cha Kupigia Kura, na matokeo hayo yawe rasmi.

Tabia ya kufukuza Wapiga Kura kwenye Vituo vya Kupiga Kura ikomeshwe ili Mshindi halali ajulikane.
Hili halihitaji Azimio la Bunge wala Mswada wowote wa Sheria.

Wananchi tukiamua na kushinikiza, hili linawezekana kufanyika kwenye Uchaguzi Mkuu Novemba mwaka huu 2025
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
Sawa zitahesabiwa
 
Njia pekee ya Watanzania kuheshimiwa na Wawakilishi wetu ni kuhakikisha kwamba Kura zetu zinahesabiwa katika mazingira ya uwazi kwenye kila Kituo cha Kupigia Kura, na matokeo hayo yawe rasmi.

Tabia ya kufukuza Wapiga Kura kwenye Vituo vya Kupiga Kura ikomeshwe ili Mshindi halali ajulikane.
Hili halihitaji Azimio la Bunge wala Mswada wowote wa Sheria.

Wananchi tukiamua na kushinikiza, hili linawezekana kufanyika kwenye Uchaguzi Mkuu Novemba mwaka huu 2025
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
Hao wananchi wa kushinikiza chama dola hawapo Tanzania
 
Njia pekee ya Watanzania kuheshimiwa na Wawakilishi wetu ni kuhakikisha kwamba Kura zetu zinahesabiwa katika mazingira ya uwazi kwenye kila Kituo cha Kupigia Kura, na matokeo hayo yawe rasmi.

Tabia ya kufukuza Wapiga Kura kwenye Vituo vya Kupiga Kura ikomeshwe ili Mshindi halali ajulikane.
Hili halihitaji Azimio la Bunge wala Mswada wowote wa Sheria.

Wananchi tukiamua na kushinikiza, hili linawezekana kufanyika kwenye Uchaguzi Mkuu Novemba mwaka huu 2025
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
Tanzania kwani kunakuaga na uchaguzi?Tangu lini. Mimi nadhani uchaguzi wangu wa mwisho ni 2020 sitegemei kupoteza mda wangu tena kwa vitu visivyo na maana.
 
Labda raia wawe na silaha hasa za moto, ifahamike uporaji wa chaguzi zetu unasimamiwa na vyombo vya dola ambavyo vinamiliki silaha za moto.

Ifahamike ccm haina uwezo tena wa kushinda kwenye uchaguzi halali. Hivyo tusitarajue chaguzi za haki tena bila machaguko kwanza, ama mapinduzi ya kijeshi.
Tindo, uko sahihi sana.
Uwakilishi unaopatikana kwa mbinu badala ya Kura halali, ni uporaji na ni kinyume cha Katiba iliyopo na Kanuni za Uchaguzi zilizopo.
Kwa kuwa Kura zinatakiwa ziwe halali, Wapiga Kura tumechangia sana kuleta tabia hizi mbaya za Chama Tawala kwa kukaa kimya.
Kila wanachofaa, sisi tumekuwa kimya.
Mwishowe wanajiona wako sahihi.
Hatuhitaji Silaha za moto.
Tunahitaji kupaza sauti, tusikike.
Wanaotumia Silaha za moto, Kwa watu ambao hawana hata mawe mikononi wana lengo la kututisha.
Wanalenga kututisha ili tutishike, tuogope kusema.
Kimsingi, wanajijua kuwa wana hatia.
Sisi tupaze sauti.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Unaweza isvyo sahihi,

Kwamba kura fake zihesabiwe Kwa uwazi?

Hukujifunza uchaguzi wa Serikali za mitaa?

Rudi andika UPYA kwamba,

Tunataka Tume huru na Katiba mpya kabla ya Uchaguzi wa October,

Tupate Sanduku la kura lisilonajisiwa.

Ndipo tupige kura na zihesabiwe Kwa uwazi.

Na bila Tume huru ya Uchaguzi, uchaguzi utayeyuka.

Sijui umeelewa?
Rabbon, mimi na wewe, yaani sisi wote, tuko sahihi.
Kupaza sauti ni njia sahihi.
Tena njia ambayo Babu Wassira hawezi kuwadanganya Wapiga Kura waipuuze, kama alivyowaambia Watanzania wenzetu kule Musoma, siku walipompokea.
Aliwaambia kuwa Watanzania wanataka MAENDELEO, siyo Katiba Mpya na Wasanii wa CCM wakamshangilia.
Je, anaweza kusimama hadharani na kutamka kwamba Watanzania hawataki KURA ZAO ZIHESABIWE KWA UWAZI?
Katiba Mpya na Tume Huru ndiyo suluhisho Kuu.
Ili kulifikia, kwa hawa Watawala ambao wanajua kwamba Wapiga Kura hawawataki, upo umuhimu wa kutumia kila nyenzo tuliyonayo.
Nyenzo ambayo hawawezi kutunyang'anya ni SAUTI ZETU.
Tupaze sauti.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Ni ukweli mtupu
Badala ya kuimarisha Elimu, Huduma za Afya, Maji na Miundombinu, Kodi zetu zinatumika kununua Silaha na Magari ya Maji ya Washawasha kuja kutudhuru.
Watawala wanapata Uwakilishi na Urais kwa KUIBA Kura ndiyo sababu wanatudharau sisi tunaotakiwa kuwaweka Madarakani.
Sasa tuamke.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI
 
Tanzania kwani kunakuaga na uchaguzi?Tangu lini. Mimi nadhani uchaguzi wangu wa mwisho ni 2020 sitegemei kupoteza mda wangu tena kwa vitu visivyo na maana.
Japhet gombe,
Kuna usemi kwamba, "Wenye uelewa lakini wakaacha kupiga Kura, wanatawaliwa na wasio na uelewa, waliopiga Kura".
Huu ni usemi sahihi sana.
Na Watawala wanatumia mwanya huo kujazia Masanduku ya Kura za wasiojitokeza kuweka "Alama ya ✓" kwenye Majina yao.
Tafsiri hapa ni kwamba, usipoenda kupiga Kura, umeruhusu Kura yako ipigwe na usiyemtaka.
Tusiruhusu hali hali.
Wala tusikubali kukatishwa Tamasha na hawa WEZI WA KURA ZETU.
Tupaze sauti.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
 
Back
Top Bottom