nicholasmari
JF-Expert Member
- Dec 28, 2024
- 630
- 583
Ana akili siyo km babu yako ambaye hana mchango unaojulikana ktk hili TaifaBabu Wassira anahutubia watu na kuwaambia kwamba Watanzania wanataka huduma, siyo Katiba Mpya.
Je, ataweza kutamka hadharani kwamba Watanzania hawataki Kura zao zihesabiwe kwa uwazi?
Na huko Makanisani na Misikitini wanaenda kutoa "mabaki" yaliyobaki baada ya rushwa kama Sadaka!Wakishaiba kura wanaenda makanisani na misikitini bila aibu.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUUSawa pazeni
Nyie nyumbu siasa zenu zinaishiaga humu JFUko sahihi Vessel.
Ndiyo sababu ni muhimu sana kuoaza sauti, ndani na nje ya mipaka yetu kwamba TUNATAKA KURA ZETU ZIHESHIMIKE.
Ili Kura zetu ZIHESHIMIKE, tunataka zihesabiwe kwa Haki na kwa Uwazi.
Kwa Sheria hizi hizi na Kanuni za Uchaguzi hizi hizi.
Tupaze sauti ili wayasikie hayo uliyoandika.Na kwanini mtu asitake uwazi,yeye ni nani?
Mimi nasemaje ikibidi kila chama wakati wa kura kiwe na upande wake tuone hawa ni ccm na hawa ni Chadema ama Act
Kwa kuwa Kura zinahesabiwa mafichoni, aliyeshindwa anapata wasaa wa kugeuza matokeo.CCM cama tawala hakitaki kwasabb kitashindwa mapema asubuhi.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUUUnasema sawaπ€£.
Mimi na wewe, na yeye na yule ndio Watanzania.We ndio watanzania? Watanzania wana wawakilishi wao wa kuwasemea, tafuta fursa ya kwenda kuwawakilisha hao watanzania kwanza
Kiburi cha kumkashifu Babu yangu kwamba hana mchango katika Taifa hili kinaletwa na TABIA YA KUDHARAU WATANZANIA ambao Kura zao ndizo zinawapeleka Wabunge Mjengoni na Rais Ikulu.Ana akili siyo km babu yako ambaye hana mchango unaojulikana ktk hili Taifa
Uko sahihi kutukana kwa sababu umejiaminisha kwamba Wapiga Kura wasio na Vyama, ambao wanakaa kimya, akili zao ni sawa na Nyumbu wa Mbuga ya Serengeti.Nyie nyumbu siasa zenu zinaishiaga humu JF
Mkuu acha kujitoa ufahamu, huna chama halafu unaenda kuchagua wagombea wa vyama tu?! Kungekuwa na mgombea binafsi ungekuwa na hoja. Pambana upate mgombea binafsi ili uwe nje ya huu uchaguzi wa kihuni wa kuchagua wagombea wa vyama. Hao mawakala wa vyama vya upinzani huweza kufanywa lolote na vyombo vya dola na wasifanye lolote. Rudi hapa nchini uje uone hizo nadharia zako kama zinafanya kazi.Nimesoma kwa makini ilichoandika.
Bandiko lako limeegemea upande wa Mfumo wa hivi Vyama vyetu vya Kisiasa.
Na hicho ndicho wanachotamka Watawala.
Kwamba, Wananchi wa kawaida, ambao ndio Wapiga Kura, WAJITENGE NA MADAI YA VYAMA VYA SIASA, ili kesho na kesho kutwa Babu Wassira aende kwenye Majukwaa na kuwaambia watu kwamba hayo ni "mambo ya Waoinzani".
Hoja yangu mimi ni kuhusu SISI WAPIGA KURA, tena wengi wetu, (majority), tusio Wanachama wa Chama chochote cha Siasa.
Nimemskia Mchambuzi wa Siasa na Ujasusi, ndugu yetu Evarist Chahali, akisema kwamba Asilimia 80 ya Wapiga Kura, siyo Wanachama wa Chama chochote cha Siasa.
Kundi hilo ndilo tunaotakiwa kupaza sauti zetu.
Kwenye Vituo vya Kupiga Kura, CHADEMA wanakuwa na Wakala.
CCM wanakuwa na Wakala.
Sisi tusio na Wakala, tena ambao ndio MAJORITY, haki yetu inalindwa na nani?
Mlinzi pekee wa Haki yetu ni KURA ZETU KUHESABIWA KWA UWAZI, na zitangazwe kuwa rasmi.
Tupaze sauti zetu.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
Tatizo tume ya kutangaza matokeo wote ni makada wa chama tawala...Mkuu Smart911,
Wametuchukulia powa kwa muda mrefu sana mpaka wamejisahau.
Tukiamua kupaza sauti zetu, zikaenea Tanzania nzima, mpaka zikavuka Mipaka ya Nchi yetu, watasikiliza.
Zama hizi za Social Media, ndiyo wakati wa wasio na sauti.
Tupaze sauti zetu.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
Uende usiende wao watajaza tu afadhali uwaachie tuJaphet gombe,
Kuna usemi kwamba, "Wenye uelewa lakini wakaacha kupiga Kura, wanatawaliwa na wasio na uelewa, waliopiga Kura".
Huu ni usemi sahihi sana.
Na Watawala wanatumia mwanya huo kujazia Masanduku ya Kura za wasiojitokeza kuweka "Alama ya β" kwenye Majina yao.
Tafsiri hapa ni kwamba, usipoenda kupiga Kura, umeruhusu Kura yako ipigwe na usiyemtaka.
Tusiruhusu hali hali.
Wala tusikubali kukatishwa Tamasha na hawa WEZI WA KURA ZETU.
Tupaze sauti.
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
CCM wakisikia hayo maneno wanatetemeka sana.Njia pekee ya Watanzania kuheshimiwa na Wawakilishi wetu ni kuhakikisha kwamba Kura zetu zinahesabiwa katika mazingira ya uwazi kwenye kila Kituo cha Kupigia Kura, na matokeo hayo yawe rasmi.
Tabia ya kufukuza Wapiga Kura kwenye Vituo vya Kupiga Kura ikomeshwe ili Mshindi halali ajulikane.
Hili halihitaji Azimio la Bunge wala Mswada wowote wa Sheria.
Wananchi tukiamua na kushinikiza, hili linawezekana kufanyika kwenye Uchaguzi Mkuu Novemba mwaka huu 2025
#KURA ZIHESABIWE KWA UWAZI UCHAGUZI MKUU
Maneno yako ni mazito.Mkuu acha kujitoa ufahamu, huna chama halafu unaenda kuchagua wagombea wa vyama tu?! Kungekuwa na mgombea binafsi ungekuwa na hoja. Pambana upate mgombea binafsi ili uwe nje ya huu uchaguzi wa kihuni wa kuchagua wagombea wa vyama. Hao mawakala wa vyama vya upinzani huweza kufanywa lolote na vyombo vya dola na wasifanye lolote. Rudi hapa nchini uje uone hizo nadharia zako kama zinafanya kazi.
Tatizo kubwa zaidi ni kwamba Wapiga Kura wanaridhika anapotangazwa Mgombea ambaye hakuchaguliwa kihalali.Tatizo tume ya kutangaza matokeo wote ni makada wa chama tawala...
Ukiwaachia ni sawa na kuacha Mlango wazi ili Mwizi aje KUIBA kiulaini.Uende usiende wao watajaza tu afadhali uwaachie tu
Hao Watanzania wenyewe ni mimi na wewe.Hao watanzania wenyewe sasa π
Tupaze sauti zaidi na zaidi, ili watetemeke sana.CCM wakisikia hayo maneno wanatetemeka sana.