Watanzania tusipomshukuru Nyerere kwa hili tutapata laana

Watanzania tusipomshukuru Nyerere kwa hili tutapata laana

Ila kwa Tanzania hali imekuwa tofauti. Pamoja na utofauti wa itikadi zetu za kisiasa, kidini, kabila nk. Lakini linapokuja swala la kitaifa tunakuwa kitu kimoja. Leo hii mtanzania akipata tatizo lolote huku nje tutamchangia kwa sababu ya utanzania wake, na sio kwa ajili ya dini yake, chama chake, kabila lake au mkoa wake. Tunaamini sisi wote ni wamoja, tunaoishi katika nyumba moja, ya baba mmoja na mama mmoja. Kwa wenzetu ukileta taarifa za mmoja wao kama anaumwa au kafariki, utasikia
Mkuu 'Dudumizi', najua wewe siyo mgeni sana humu JF, na ninakumbuka vyema michango yako humu Jukwaani.

Ila sielewi hasa ni nini msukumo uliokufanya uweke mada hii hapa, ambayo kwa kiasi kikubwa na kwa bahati mbaya sana ni kama imekwishapitwa na wakati.

Unayoyaeleza kwenye andiko lako gumu (kutokana na uwasilishaji wake wa kiuandishi), ni mambo ambayo yalikuwepo miaka michache iliyopita. Siku hizi tuna makundi mbalimbali, kila kundi likipigania maslahi yake zaidi kuliko utaifa alioufanyia kazi kubwa Mwalimu Nyerere.

Leo hii tunayo makundi kama ua UCCM na wenzao; kuna wanaoamini zaidi udini wao kuliko uTanzania wao.
Siku hizi ni sifa kujitambua kuwa wewe ni Msukuma, na unaona raha kabisa kuzungumza lugha yako hata kama kuna wasioelewa chochote juu ya lugha hiyo.

Sasa hivi tupo kwenye shughuli kubwa ya "Kuifungua nchi."
Kuifungua nchi nako kunaonekana kuwa kama ni kutafuta njia za kuwapata watu wenye uwezo wa kuunda kundi lao lenye uwezo wa kuwa tofauti na makundi mengine. Tutatumia nguvu nyingi kuliunda kundi hili kwa gharama kubwa dhidi ya makundi mengine.

Hii ni mifano michache tu inayoweza kukuonyesha kwamba kazi kubwa aliyoifanya Mwalimu Nyerere, tena kwa mafanikio makubwa, sasa hivi ni kama kuna juhudi kubwa ya kuibomoa kazi hiyo.
 
Kabla hajawa Rais Tanganyika haikuwa na tatizo la ukabila wala udini lakini aliposhika madaraka alitengeneza tatizo la udini, waislamu walianza kuminywa kisiri siri.
Walianza kuminywa kivipi mkuu? Hebu tufafanulie.
 
Mkuu 'Dudumizi', najua wewe siyo mgeni sana humu JF, na ninakumbuka vyema michango yako humu Jukwaani.

Ila sielewi hasa ni nini msukumo uliokufanya uweke mada hii hapa, ambayo kwa kiasi kikubwa na kwa bahati mbaya sana ni kama imekwishapitwa na wakati.

Unayoyaeleza kwenye andiko lako gumu (kutokana na uwasilishaji wake wa kiuandishi), ni mambo ambayo yalikuwepo miaka michache iliyopita. Siku hizi tuna makundi mbalimbali, kila kundi likipigania maslahi yake zaidi kuliko utaifa alioufanyia kazi kubwa Mwalimu Nyerere.

Leo hii tunayo makundi kama ua UCCM na wenzao; kuna wanaoamini zaidi udini wao kuliko uTanzania wao.
Siku hizi ni sifa kujitambua kuwa wewe ni Msukuma, na unaona raha kabisa kuzungumza lugha yako hata kama kuna wasioelewa chochote juu ya lugha hiyo.

Sasa hivi tupo kwenye shughuli kubwa ya "Kuifungua nchi."
Kuifungua nchi nako kunaonekana kuwa kama ni kutafuta njia za kuwapata watu wenye uwezo wa kuunda kundi lao lenye uwezo wa kuwa tofauti na makundi mengine. Tutatumia nguvu nyingi kuliunda kundi hili kwa gharama kubwa dhidi ya makundi mengine.

Hii ni mifano michache tu inayoweza kukuonyesha kwamba kazi kubwa aliyoifanya Mwalimu Nyerere, tena kwa mafanikio makubwa, sasa hivi ni kama kuna juhudi kubwa ya kuibomoa kazi hiyo.
Mkuu Kalamu1 , kwanza napenda kutumia nafasi hii kukushukur kwa kufuatilia michango yangu na ya wana JF wenzetu mbali mbali. Kwa hakika haya ya ubaguzi unayoyasema mengi yanafanyika ndani ya mipaka yetu, na sio nje ya mipaka yetu. Sikatai kwamba hata nje bado kuna makundi mbali mbali ya uchama kama vile ccm wana mashina yao mengi nje ya nchi, ambayo yanaendesha shughuli za kichama kwa watanzania wanaoishi katika nchi hizo.

Halikadhalika na Chadema, Cuf na vyama vingine navyo vina mashina yao mbali mbali huku nje kwa ajili ya masilahi yao na ya vyama vyao kama ilivyo kwa ccm. Ila linapokuja swala la utaifa, mfano kuna mtanzania amepigwa risasi akafari na baadae kuhitajika michango kwa ajili ya kuusafirisha mwili wake, basi wengi huchangia kwa kigezo cha kumchangia mtanzania mwenzetu, na sio kuchanga kwa vile ni mnyatulu mwenzetu, mzaramo mwenzetu, muislamu mwenzetu, mkristo mwenzetu nk.

Kuna nchi zina ubaguzi wa ndani na nje. Yani raia wanabaguana wakiwa ndani ya nchi na nje ya nchi pia. Mfano unakuta mcongo amefariki inapokuja taarifa kwa wacongo wenzie utaona wanaanza kuuliza vipi aliekufa ni msema lingala au mswahili. Ukisema tu ni msema lingala, basi utasikia wasema kiswahili wanajibu kama ni msema lingala basi atazikwa na wangala wenzake sisi huo msiba hautuhusu.

Kwahiyo mkuu pamoja na kwamba kuna changamoto mbali mbali zinazojitokeza katika nchi yetu, lakini bado ile misingi ya umoja na utaifa haijabomoka, sijui labda kwa huko mbeleni kama watanzania hatujakuwa macho kukemea ubaguzi wa aina yoyote.
 
SAWA>
Lakini kumbuka swali hilo sio polisi pekee wanaolitumia.
Ukienda kwenye nyumba za wageni, utatakiwa kujaza kabila.
Sioni faida yoyote inayotokana na kujitambulisha kwa mtu kwa kabila mahali popote.
Sijui kama kwenye Sensa kuna sehemu inayoulizia kabila la mtu anayehesabiwa.

Kama haina lazima ya kujihesabu kwa dini, kwa nini kabila iwe sawa!
Nafikiri hapo kwenye kabila wangetoa na badala yake wangekuwa wanauliza utaifa, au namba ya kitambulisho cha uraia.
 
Kwahiyo mkuu pamoja na kwamba kuna changamoto mbali mbali zinazojitokeza katika nchi yetu, lakini bado ile misingi ya umoja na utaifa haijabomoka, sijui labda kwa huko mbeleni kama watanzania hatujakuwa macho kukemea ubaguzi wa aina yoyote
Hizi unazoziita "changamoto", ndiyo chachu (mbegu) mbaya kabisa inayotupeleka huko, tena kwa haraka sana, ambako tulidhani kuwa sisi hatupo tena.

Aliyoyafanya Mwalimu katika eneo hili yalitakiwa kuendelezwa (kupaliliwa) kwa makini zaidi na viongozi wote waliokuja baada yake, lakini sasa utaona kuwa kuna baadhi yao wanaong'oa hata mizizi ya mbegu hiyo muhimu.
Tulishafikia mahali ambapo kujua au kujitambulisha kwa mtu kwa kabila lake ilikwishakuwa haina maana yoyote.
 
Hizi unazoziita "changamoto", ndiyo chachu (mbegu) mbaya kabisa inayotupeleka huko, tena kwa haraka sana, ambako tulidhani kuwa sisi hatupo tena.

Aliyoyafanya Mwalimu katika eneo hili yalitakiwa kuendelezwa (kupaliliwa) kwa makini zaidi na viongozi wote waliokuja baada yake, lakini sasa utaona kuwa kuna baadhi yao wanaong'oa hata mizizi ya mbegu hiyo muhimu.
Tulishafikia mahali ambapo kujua au kujitambulisha kwa mtu kwa kabila lake ilikwishakuwa haina maana yoyote.
Ya nimekuelewa mkuu. Nafikiri ni vizuri sisi wananchi kama raia halali wa nchi hii tupambane na wale wanaojaribu kuiharibu misingi hii bora kabisa iliyoachwa na baba yetu wa taifa.
 
Alikuwa akiwabagua katika madaraka na wengine kuwekwa ndani kwa visingizio mbalimbali.
Ok mkuu.. ila mbona hata wakristo wapo waliokosa kuwekwa katika uongozi. Wapo pia waliofungwa, na wengine kukimbia nchi kama vile kina Oscar Kambona nk.
 
Habari zenu wana JF wenzangu. Ama baada ya salam, ningependa nielekee kwenye mada husika.

Ndugu watanzania na wana JF wenzangu, katika pita pita yangu ya kutafuta ugali wangu, nimefanikiwa kukutana na watu mbali mbali waliotoka katika nchi mbali mbali za Africa na nje ya Africa.

Hakika kukutana nao watu hao kumenifanya nifahamu mambo mbali mbali yanayohusu nchi zao na tamaduni zao.

Katika kufahamu huko ndipo nilipokuja kuona upendo wa kweli aliokuwa nao baba yetu wa Taifa mwl J.K. Nyerere kwa sisi watoto wake au wananchi wake.

Nchi hizi nyingi unakuta hazina utaifa. Kwa mfano kuna wacongo ambao lugha yao kuu ni lingala tu, wangala hawa wakikutana na wacongo wanaoongea kiswahili huwa hawapatani kabisa, kiasi kwamba unaweza ukafikiri kuwa watu hao ni wa nchi mbili tofauti.

Yani mcongo anae ongea kiswahili yupo radhi kumsaidia mtanzania, mkenya au muongea kiswahili yeyote mwenzake kuliko kumsaidia muongea lingala.

Hivyo hivyo na kwa ndugu zao wangala ambao huwaona wenzao waongea kiswahili kuwa sio wacongomani original, wangala huamini kwamba waongea kiswahili ni migrants waliongia congo miaka mingi iliyopita wakitokea katika nchi kama vile Tanzania, Burundi, Rwanda nk.

Tukija kwa upande wa Zimbabwe pia kuna ubaguzi katika ya makabila makubwa mawili yenye kuongea lugha tofauti, yani washona (shona) na wandebele (ndebele).

Pia hawa wamekuwa hawana umoja hata chembe. Unakuta mfano mshona labda anapewa deal la kutafuta wafanya kazi na boss wake, mshona atahangaika kutafuta washona wenzake na akiwakosa basi bora deal hilo ampe mtu yeyote kutoka katika nchi nyingine kuliko kumpa mzimbabwe mwenzake wa kabila la ndebele hata kama wanapanga katika mjengo mmoja.

Na hii ipo hata kwa wandebele ambao hupeana kazi wenyewe kwa wenyewe, huku wakiwaacha ndugu zao washona kwenye mataa. Washona anaamini kuwa wandebele ni migrants walio ingia Zimbabwe kutoka Afrika kusini miaka mingi iliyopita.

Kadhalika hata kwa jirani zetu kama vile Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda tumeweza kuona migawanyiko hiyo ambayo huendelea mpaka nje ya mipaka ya nchi zao. Ila kwa Tanzania hali imekuwa tofauti.

Pamoja na utofauti wa itikadi zetu za kisiasa, kidini, kabila nk. Lakini linapokuja swala la kitaifa tunakuwa kitu kimoja. Leo hii mtanzania akipata tatizo lolote huku nje tutamchangia kwa sababu ya utanzania wake, na sio kwa ajili ya dini yake, chama chake, kabila lake au mkoa wake.

Tunaamini sisi wote ni wamoja, tunaoishi katika nyumba moja, ya baba mmoja na mama mmoja.

Kwa wenzetu ukileta taarifa za mmoja wao kama anaumwa au kafariki, utasikia wanauliza.. kwanza huyo kijana aliekufa, kupata tatizo au kuumwa ni muhutu au mtusi, ni muongea lingala au kiswahili, ni mshona au ndebele, ni mkikuyu au mjaluo nk.

So kwa hili la baba wa taifa kutujenga na kutufanya watanzania wote tuwe kitu kimoja katika utaifa, ni la kupongezwa sana. Japo kwa sasa kuna baadhi ya changamoto ndogo ndogo zimekuwa zikijitokeza, lakini ule msingi wa utaifa bado upo.

Nani kama Nyerere? Asanteni sana kwa kunisoma. Picha ya chini kabisa baba wa taifa mwl J. Nyerere akikumbatiana kwa furaha na mh J. Kikwete. RIP baba wa Taifa letu
Piga Vita udini na ukabila unagawa watu
 
Habari zenu wana JF wenzangu. Ama baada ya salam, ningependa nielekee kwenye mada husika.

Ndugu watanzania na wana JF wenzangu, katika pita pita yangu ya kutafuta ugali wangu, nimefanikiwa kukutana na watu mbali mbali waliotoka katika nchi mbali mbali za Africa na nje ya Africa.

Hakika kukutana nao watu hao kumenifanya nifahamu mambo mbali mbali yanayohusu nchi zao na tamaduni zao.

Katika kufahamu huko ndipo nilipokuja kuona upendo wa kweli aliokuwa nao baba yetu wa Taifa mwl J.K. Nyerere kwa sisi watoto wake au wananchi wake.

Nchi hizi nyingi unakuta hazina utaifa. Kwa mfano kuna wacongo ambao lugha yao kuu ni lingala tu, wangala hawa wakikutana na wacongo wanaoongea kiswahili huwa hawapatani kabisa, kiasi kwamba unaweza ukafikiri kuwa watu hao ni wa nchi mbili tofauti.

Yani mcongo anae ongea kiswahili yupo radhi kumsaidia mtanzania, mkenya au muongea kiswahili yeyote mwenzake kuliko kumsaidia muongea lingala.

Hivyo hivyo na kwa ndugu zao wangala ambao huwaona wenzao waongea kiswahili kuwa sio wacongomani original, wangala huamini kwamba waongea kiswahili ni migrants waliongia congo miaka mingi iliyopita wakitokea katika nchi kama vile Tanzania, Burundi, Rwanda nk.

Tukija kwa upande wa Zimbabwe pia kuna ubaguzi katika ya makabila makubwa mawili yenye kuongea lugha tofauti, yani washona (shona) na wandebele (ndebele).

Pia hawa wamekuwa hawana umoja hata chembe. Unakuta mfano mshona labda anapewa deal la kutafuta wafanya kazi na boss wake, mshona atahangaika kutafuta washona wenzake na akiwakosa basi bora deal hilo ampe mtu yeyote kutoka katika nchi nyingine kuliko kumpa mzimbabwe mwenzake wa kabila la ndebele hata kama wanapanga katika mjengo mmoja.

Na hii ipo hata kwa wandebele ambao hupeana kazi wenyewe kwa wenyewe, huku wakiwaacha ndugu zao washona kwenye mataa. Washona anaamini kuwa wandebele ni migrants walio ingia Zimbabwe kutoka Afrika kusini miaka mingi iliyopita.

Kadhalika hata kwa jirani zetu kama vile Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda tumeweza kuona migawanyiko hiyo ambayo huendelea mpaka nje ya mipaka ya nchi zao. Ila kwa Tanzania hali imekuwa tofauti.

Pamoja na utofauti wa itikadi zetu za kisiasa, kidini, kabila nk. Lakini linapokuja swala la kitaifa tunakuwa kitu kimoja. Leo hii mtanzania akipata tatizo lolote huku nje tutamchangia kwa sababu ya utanzania wake, na sio kwa ajili ya dini yake, chama chake, kabila lake au mkoa wake.

Tunaamini sisi wote ni wamoja, tunaoishi katika nyumba moja, ya baba mmoja na mama mmoja.

Kwa wenzetu ukileta taarifa za mmoja wao kama anaumwa au kafariki, utasikia wanauliza.. kwanza huyo kijana aliekufa, kupata tatizo au kuumwa ni muhutu au mtusi, ni muongea lingala au kiswahili, ni mshona au ndebele, ni mkikuyu au mjaluo nk.

So kwa hili la baba wa taifa kutujenga na kutufanya watanzania wote tuwe kitu kimoja katika utaifa, ni la kupongezwa sana. Japo kwa sasa kuna baadhi ya changamoto ndogo ndogo zimekuwa zikijitokeza, lakini ule msingi wa utaifa bado upo.

Nani kama Nyerere? Asanteni sana kwa kunisoma. Picha ya chini kabisa baba wa taifa mwl J. Nyerere akikumbatiana kwa furaha na mh J. Kikwete. RIP baba wa Taifa letu
Piga Vita udini na ukabila una gawa watu
 
Mwendazake na Mpemba wametusahaulisha ya Mwalimu na sasa wameturudisha huko kwenye kuulizana Makabila.

Nimeshangaa sana Juzi, Trafiki kuniuliza: Kwani wewe kabila gani? Aisee!! Nlimind na amenifikirisha mpaka saahizi!!?
Tena mwendazake ndio alikuwa akipiga kampeni kwa kilugha na kujivunia kabila lake kila mara,,
 
Nafikiri hapo kwenye kabila wangetoa na badala yake wangekuwa wanauliza utaifa, au namba ya kitambulisho cha uraia.
Hilo takwa la hoteli kujaza kabila ni takwa la Polisi/ Uhamiaji. Haja ya kubadili ujinga huu iko pale pale. Polisi walirithi kwa Mkoloni. Mie ambaye mama na baba huwa ni makabila tofauti huwa napiga kamari nijaze kabila lipi kila ninapohitajika. Wabunge wetu wao ni kushangilia bajeti basi; hili hawalioni. Sasa hivi wapenzi wa makabila tofauti kuoana imeenea mno kwetu Tanzania, pia sifa ya huyo huyo Baba wa Taifa; kwa hiyo ni kero kweli kweli watoto wao kuwauliza kabila!

Sent from my ONEPLUS A5000 using JamiiForums mobile app
 
..Tanganyika haikuwa na tatizo la ukabila kabla ya uhuru.

..Kwa hiyo Mwalimu Nyerere alienzi na kutunza hali ya undugu na maelewano iliyokuwepo.

..Lugha ya Kiswahili nayo ilikuwa imesambaa maeneo mengi ya Tanganyika.

..Kwasababu Kiswahili kilikuwa kikieleweka na Watanganyika waliowengi ilikuwa rahisi kwa Tanu kueneza ujumbe wa kudai uhuru nchi nzima.

..Mwalimu alifanya juhudi kubwa kueneza ELIMU kwa Watanzania wote bila ubaguzi.

..Mwalimu pia alichukua maamuzi ya kuandikisha Watanzania wote ktk majeshi yetu.

..Wakoloni walikuwa wakiandikisha makabila fulani majeshini, Mwalimu aliondoa utaratibu huo.
 
Back
Top Bottom