Watanzania tusipomshukuru Nyerere kwa hili tutapata laana

Watanzania tusipomshukuru Nyerere kwa hili tutapata laana

Hilo swala lilikuepo tangu zamani, yeye amelikuta. Ndio maana hata watemi, machifu walikuwa na ushirikiano. Hata yeye alikaribishwa mjini na wenyeji kwa upendo, kwa hiyo umoja huo upo kabla yake
 
Kabla hajawa Rais Tanganyika haikuwa na tatizo la ukabila wala udini lakini aliposhika madaraka alitengeneza tatizo la udini, waislamu walianza kuminywa kisiri siri.
Una shida ww.Umenikumbusha ya prof Kigoma Malima kutaka kujiunga Chuo Kikuu lazima uwe Abdallah ama Ashura.
 
Nyerere hiki kitu alikikuta alichofanya yeye ni kudumisha hali hiyo. Yumkini Nyerere alipata shida na changamoto kudumisha hali hiyo
Huku pwani tulikuwa tukikutana kwenye vijiwe vya kahawa haulizwi mtu kabila wala Asili yake

Ukiingia interior utakuta
The largest colonial resistance war in Africa => Majimaji War ilihusisha makumi kadhaa ya makabila hii inaonyesha jinsi gani Machifu wa Makabila yetu walivyokuwa wamoja

Wakati tunaanzisha taasisi za kupigania uhuru wa nchi AA => TAA=> TANU halikadhalika mambo yalikuwa hivyo hivyo.Nyerere + Rupia + Kahama waliweza tangamana na akina Sykes + Mshume Kiate + Mwapachu + Titi + Aziz Ali + Takadiri + Mtemvu + Mufti Hassan bin Amir + Tewa Said na kutengeneza taasisi iliyo na nguvu kubwa

Mambo yalibadilika baada ya kupata Uhuru, tukaanza kusikia baadhi ya Mashirika ya Uma yakanasibishwa na kabila fulani
eti kuanzia Mfyagiaji mpaka Meneja Mkuu ni wa kabila fulani
Tukaanza kushuhudia watu wa dini fulani wakirundikana kwenye taasisi muhimu zote zilizobeba hatima ya nchi kwa uwiano wa 75:25 mpaka 80:20
Tukaanza kushuhudia ktk elimu watoto wa dini fulani wakifaulu/kufeli ktk uwiano uliyoonyeshwa hapo juu

Wakatabahu
 
KWELI TUPU. INAYONISHANGAZA KWA MIAKA YA HIVI KARIBUNI NI KUCHIPUKA KWA UBAGUZI WA KIVYAMA VYA SIASA? NI HATARI KUBWA! INATAKIWA KUREKEBISHWA HARAKA. NAPENDEKEZA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA. WANASIASA VIONGOZI WA VYAMA WASHINDANE KWA UWAZI NA HAKI. WASHINDANE KWA HOJA, PIA WAWE NA TUME YAO HURU YA KUSHUGHULIKIA MASLAHI YAO
 
Inabidi sisi wenyewe kama watanzania, tukiona swala linapelekwa nje ya mstari tupambane ili lirudishwe katika misingi yake.

CCM imeifikisha hii nchi mahali hakuna hoja za watanzania, bali kuna hoja za CCM, na hoja za wapinzani. Sioni ni wapi tunasimama kama watanzania kwenye hoja zetu. Labda mahali tulipo pamoja japo ni kwa maumivu, ni mfumuko wa bei.
 
Habari zenu wana JF wenzangu. Ama baada ya salam, ningependa nielekee kwenye mada husika.

Ndugu watanzania na wana JF wenzangu, katika pita pita yangu ya kutafuta ugali wangu, nimefanikiwa kukutana na watu mbali mbali waliotoka katika nchi mbali mbali za Africa na nje ya Africa.

Hakika kukutana nao watu hao kumenifanya nifahamu mambo mbali mbali yanayohusu nchi zao na tamaduni zao.

Katika kufahamu huko ndipo nilipokuja kuona upendo wa kweli aliokuwa nao baba yetu wa Taifa mwl J.K. Nyerere kwa sisi watoto wake au wananchi wake.

Nchi hizi nyingi unakuta hazina utaifa. Kwa mfano kuna wacongo ambao lugha yao kuu ni lingala tu, wangala hawa wakikutana na wacongo wanaoongea kiswahili huwa hawapatani kabisa, kiasi kwamba unaweza ukafikiri kuwa watu hao ni wa nchi mbili tofauti.

Yani mcongo anae ongea kiswahili yupo radhi kumsaidia mtanzania, mkenya au muongea kiswahili yeyote mwenzake kuliko kumsaidia muongea lingala.

Hivyo hivyo na kwa ndugu zao wangala ambao huwaona wenzao waongea kiswahili kuwa sio wacongomani original, wangala huamini kwamba waongea kiswahili ni migrants waliongia congo miaka mingi iliyopita wakitokea katika nchi kama vile Tanzania, Burundi, Rwanda nk.

Tukija kwa upande wa Zimbabwe pia kuna ubaguzi katika ya makabila makubwa mawili yenye kuongea lugha tofauti, yani washona (shona) na wandebele (ndebele).

Pia hawa wamekuwa hawana umoja hata chembe. Unakuta mfano mshona labda anapewa deal la kutafuta wafanya kazi na boss wake, mshona atahangaika kutafuta washona wenzake na akiwakosa basi bora deal hilo ampe mtu yeyote kutoka katika nchi nyingine kuliko kumpa mzimbabwe mwenzake wa kabila la ndebele hata kama wanapanga katika mjengo mmoja.

Na hii ipo hata kwa wandebele ambao hupeana kazi wenyewe kwa wenyewe, huku wakiwaacha ndugu zao washona kwenye mataa. Washona anaamini kuwa wandebele ni migrants walio ingia Zimbabwe kutoka Afrika kusini miaka mingi iliyopita.

Kadhalika hata kwa jirani zetu kama vile Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda tumeweza kuona migawanyiko hiyo ambayo huendelea mpaka nje ya mipaka ya nchi zao. Ila kwa Tanzania hali imekuwa tofauti.

Pamoja na utofauti wa itikadi zetu za kisiasa, kidini, kabila nk. Lakini linapokuja swala la kitaifa tunakuwa kitu kimoja. Leo hii mtanzania akipata tatizo lolote huku nje tutamchangia kwa sababu ya utanzania wake, na sio kwa ajili ya dini yake, chama chake, kabila lake au mkoa wake.

Tunaamini sisi wote ni wamoja, tunaoishi katika nyumba moja, ya baba mmoja na mama mmoja.

Kwa wenzetu ukileta taarifa za mmoja wao kama anaumwa au kafariki, utasikia wanauliza.. kwanza huyo kijana aliekufa, kupata tatizo au kuumwa ni muhutu au mtusi, ni muongea lingala au kiswahili, ni mshona au ndebele, ni mkikuyu au mjaluo nk.

So kwa hili la baba wa taifa kutujenga na kutufanya watanzania wote tuwe kitu kimoja katika utaifa, ni la kupongezwa sana. Japo kwa sasa kuna baadhi ya changamoto ndogo ndogo zimekuwa zikijitokeza, lakini ule msingi wa utaifa bado upo.

Nani kama Nyerere? Asanteni sana kwa kunisoma. Picha ya chini kabisa baba wa taifa mwl J. Nyerere akikumbatiana kwa furaha na mh J. Kikwete. RIP baba wa Taifa letu

Kama taifa lina umoja kwa nini Nyerere alipeleka jeshi Zanzibar na mpaka leo limebaki? Umoja wa kulazimishana na mtutu wa bunduki na vifaru.
 
Baba wa Taifa angekuwepo kipindi hiki Angenyonga watu wengi sana! Kuna Taasisi kubwa na makampuni bado zinaendekeza hayo mambo kwa Usiri mkubwa sana.....Huwezi kulijua hilo km Hujabaguliwa.
 
Hilo takwa la hoteli kujaza kabila ni takwa la Polisi/ Uhamiaji. Haja ya kubadili ujinga huu iko pale pale. Polisi walirithi kwa Mkoloni. Mie ambaye mama na baba huwa ni makabila tofauti huwa napiga kamari nijaze kabila lipi kila ninapohitajika. Wabunge wetu wao ni kushangilia bajeti basi; hili hawalioni. Sasa hivi wapenzi wa makabila tofauti kuoana imeenea mno kwetu Tanzania, pia sifa ya huyo huyo Baba wa Taifa; kwa hiyo ni kero kweli kweli watoto wao kuwauliza kabila!

Sent from my ONEPLUS A5000 using JamiiForums mobile app
Haya mambo ya kuulizana makabila kwa kweli hayana msingi wowote. Ni bora kwenye mahoteli wawe wanauliza ID namba au kwa mgeni aulizwe passport namba.
 
Baba wa Taifa angekuwepo kipindi hiki Angenyonga watu wengi sana! Kuna Taasisi kubwa na makampuni bado zinaendekeza hayo mambo kwa Usiri mkubwa sana.....Huwezi kulijua hilo km Hujabaguliwa.
Baba wa taifa aliacha misingi bora sana. Inabidi tuilinde na kuisimamia ipasavyo ili misingi hiyo isije kubomoka.
 
Hilo swala lilikuepo tangu zamani, yeye amelikuta. Ndio maana hata watemi, machifu walikuwa na ushirikiano. Hata yeye alikaribishwa mjini na wenyeji kwa upendo, kwa hiyo umoja huo upo kabla yake
Mkuu BrownRange inawezekana kweli hilo swala lilikuwepo kabla yake. Lakini na yeye aliposhika madaraka alilisimamia kwa nguvu zake zote, na alikemea wale waliotaka kujaribu kutengeneza ubaguzi kupitia makabila nk.
 
Nyerere hiki kitu alikikuta alichofanya yeye ni kudumisha hali hiyo. Yumkini Nyerere alipata shida na changamoto kudumisha hali hiyo
Huku pwani tulikuwa tukikutana kwenye vijiwe vya kahawa haulizwi mtu kabila wala Asili yake

Ukiingia interior utakuta
The largest colonial resistance war in Africa => Majimaji War ilihusisha makumi kadhaa ya makabila hii inaonyesha jinsi gani Machifu wa Makabila yetu walivyokuwa wamoja

Wakati tunaanzisha taasisi za kupigania uhuru wa nchi AA => TAA=> TANU halikadhalika mambo yalikuwa hivyo hivyo.Nyerere + Rupia + Kahama waliweza tangamana na akina Sykes + Mshume Kiate + Mwapachu + Titi + Aziz Ali + Takadiri + Mtemvu + Mufti Hassan bin Amir + Tewa Said na kutengeneza taasisi iliyo na nguvu kubwa

Mambo yalibadilika baada ya kupata Uhuru, tukaanza kusikia baadhi ya Mashirika ya Uma yakanasibishwa na kabila fulani
eti kuanzia Mfyagiaji mpaka Meneja Mkuu ni wa kabila fulani
Tukaanza kushuhudia watu wa dini fulani wakirundikana kwenye taasisi muhimu zote zilizobeba hatima ya nchi kwa uwiano wa 75:25 mpaka 80:20
Tukaanza kushuhudia ktk elimu watoto wa dini fulani wakifaulu/kufeli ktk uwiano uliyoonyeshwa hapo juu

Wakatabahu
Nashukuru sana mkuu Adilinanduguze , kama ni hivyo basi kuna ulazima wa kurudia katika umoja wetu ule ule uliokuwepo kabla ya uhuru.
 
Habari zenu wana JF wenzangu. Ama baada ya salam, ningependa nielekee kwenye mada husika.

Ndugu watanzania na wana JF wenzangu, katika pita pita yangu ya kutafuta ugali wangu, nimefanikiwa kukutana na watu mbali mbali waliotoka katika nchi mbali mbali za Africa na nje ya Africa.

Hakika kukutana nao watu hao kumenifanya nifahamu mambo mbali mbali yanayohusu nchi zao na tamaduni zao.

Katika kufahamu huko ndipo nilipokuja kuona upendo wa kweli aliokuwa nao baba yetu wa Taifa mwl J.K. Nyerere kwa sisi watoto wake au wananchi wake.

Nchi hizi nyingi unakuta hazina utaifa. Kwa mfano kuna wacongo ambao lugha yao kuu ni lingala tu, wangala hawa wakikutana na wacongo wanaoongea kiswahili huwa hawapatani kabisa, kiasi kwamba unaweza ukafikiri kuwa watu hao ni wa nchi mbili tofauti.

Yani mcongo anae ongea kiswahili yupo radhi kumsaidia mtanzania, mkenya au muongea kiswahili yeyote mwenzake kuliko kumsaidia muongea lingala.

Hivyo hivyo na kwa ndugu zao wangala ambao huwaona wenzao waongea kiswahili kuwa sio wacongomani original, wangala huamini kwamba waongea kiswahili ni migrants waliongia congo miaka mingi iliyopita wakitokea katika nchi kama vile Tanzania, Burundi, Rwanda nk.

Tukija kwa upande wa Zimbabwe pia kuna ubaguzi katika ya makabila makubwa mawili yenye kuongea lugha tofauti, yani washona (shona) na wandebele (ndebele).

Pia hawa wamekuwa hawana umoja hata chembe. Unakuta mfano mshona labda anapewa deal la kutafuta wafanya kazi na boss wake, mshona atahangaika kutafuta washona wenzake na akiwakosa basi bora deal hilo ampe mtu yeyote kutoka katika nchi nyingine kuliko kumpa mzimbabwe mwenzake wa kabila la ndebele hata kama wanapanga katika mjengo mmoja.

Na hii ipo hata kwa wandebele ambao hupeana kazi wenyewe kwa wenyewe, huku wakiwaacha ndugu zao washona kwenye mataa. Washona anaamini kuwa wandebele ni migrants walio ingia Zimbabwe kutoka Afrika kusini miaka mingi iliyopita.

Kadhalika hata kwa jirani zetu kama vile Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda tumeweza kuona migawanyiko hiyo ambayo huendelea mpaka nje ya mipaka ya nchi zao. Ila kwa Tanzania hali imekuwa tofauti.

Pamoja na utofauti wa itikadi zetu za kisiasa, kidini, kabila nk. Lakini linapokuja swala la kitaifa tunakuwa kitu kimoja. Leo hii mtanzania akipata tatizo lolote huku nje tutamchangia kwa sababu ya utanzania wake, na sio kwa ajili ya dini yake, chama chake, kabila lake au mkoa wake.

Tunaamini sisi wote ni wamoja, tunaoishi katika nyumba moja, ya baba mmoja na mama mmoja.

Kwa wenzetu ukileta taarifa za mmoja wao kama anaumwa au kafariki, utasikia wanauliza.. kwanza huyo kijana aliekufa, kupata tatizo au kuumwa ni muhutu au mtusi, ni muongea lingala au kiswahili, ni mshona au ndebele, ni mkikuyu au mjaluo nk.

So kwa hili la baba wa taifa kutujenga na kutufanya watanzania wote tuwe kitu kimoja katika utaifa, ni la kupongezwa sana. Japo kwa sasa kuna baadhi ya changamoto ndogo ndogo zimekuwa zikijitokeza, lakini ule msingi wa utaifa bado upo.

Nani kama Nyerere? Asanteni sana kwa kunisoma. Picha ya chini kabisa baba wa taifa mwl J. Nyerere akikumbatiana kwa furaha na mh J. Kikwete. RIP baba wa Taifa letu

Yaani tumshukuru Laanatullahi Nyerere aliyesababisha kuuwawa watu kwa maelfu Zanzibar baada ya kuivamia kwa msaada wa Wakoloni Waingereza waliomweka madarakani baada kupinduliwa ? Mnyama huyu ndiye aliyeipoteza dola yetu ya Zanzibar kwa kukubali kuwatumikia Mabwana zake waliomweka madarakani
 
Back
Top Bottom