Watanzania tusiwe wanafiki, Tozo ni muhimu kwa upana wake

Watanzania tusiwe wanafiki, Tozo ni muhimu kwa upana wake

Kuna Mtanzania alikuambia hataki kulipa kodi! Au kukatwa hizo tozo? Watu wanalalamikia matumizi yake, yaliyojaa ubadhirifu mkubwa na ufisadi wa kutisha!

Lakini pia watu wanalalamikia namna wahamasishaji wenyewe wa hizo kodi/tozo kuwa mstari wa nyuma kwa kukwepa kulipa, huku wanyonge na watu wa kawaida wakiwajibishwa ipasavyo!

Mfano mzuri ni Kesi ya Mbunge wa Ukonga Jerry Silaa kulalamikia mishahara ya Wabunge kutokukatwa kodi, Mshahara wa Rais nao tunasikia haukatwi kodi, nk. Hiki kitu ndicho kinacho amsha hisia hasi kwa raia.

Ili kodi na tozo zilipwe kwa urahisi, viongozi wawe mfano wa kuigwa kwa kulipa hizo kodi, lakini pia kuzitumia kwa matumizi sahihi! Na siyo kuzitapanya, kama ilivyo sasa.
Kwahiyo Wabunge hawatumi Miamala !? Au wameo wapo Excluded. Yaani Wamepeleka namba Zao zitolewe Kwenye Makato
 
Hamkulalamika hivyo wakati wa Magufuli, kuwa fedha wanazonyang'anya wafanya biashara zinaenda wapi?
Arusha Beureu De Change zimeporwa na vyombo vya serikali, hela ilienda wapi?
Ndio maana nasema tusiwe wanafiki.
Hii tabia ya kila kitu kurejea kwa mwendazake ni ya kipuuzi kwa sababu haiwezi kumrejesha mtu aliyetangulia mbele za haki. Pili hata mti wa mnazi una akili nyingi kukuzidi wewe kwa sababu unatambua ya kwamba ikija tufani na upepo mkali unainama kuupisha na upepo ukipita mnazi unarudi wima kuendelea na maisha.
 
Kwahiyo Wabunge hawatumi Miamala !? Au wameo wapo Excluded. Yaani Wamepeleka namba Zao zitolewe Kwenye Makato
Nimejumuisha KODI na TOZO kwenye maelezo yangu. Wabunge na Rais wana kesi ya kutolipa Kodi stahiki.

Natambua fika Tozo zinahusu makundi yote! Lakini bado, maumivu mengi yako kwa raia wa kawaida, wanaifanya miamala kila siku ukilinganisha na hao Wabunge.
 
Unafiki unatumaliza Watanzania.
Kodi zilizokuwa zikitozwa na serikali ya Awamu ya Tano kwa wafanyabiashara na wajasiria mali, wengi waliitikia wakisema mafisadi hao au wahujumu uchumi.

Kipindi cha Awamu ya Tano uonezi mwingi wa kupora, kunyang'anya, kubambika kodi na hata watu kuwekwa ndani na kufunguliwa kesi za uongo za uhujumu uchumi zilikuwepo tena nyingi sana.

Lengo lake kupata fedha kwa udi na uvuma kwa miradi ya SGR na Stiglaz Umeme na mingine mingi.

Kuna wananchi walishangilia sana uonezi uliofanywa.
Wapo viongozi walio kundi hili, Waziri Mpango wakati huo hakosekani humo.

Sasa Awamu ya Sita imerekebisha hilo ili KODI IWE KWA WATANZANIA WOTE.

Na hili linatekelezwa kwa kupitia TOZO za miamala ambazo zinamgusa kila mtu.

Hapo ndio unaona unafiki wa watu.
Hawapendi kuchangia kodi kwa maendeleo, wao wanafikiri kundi fulani tu ndio litoe kodi ili wao waneemeke.

Mshindwe, lipeni kodi Watanzania.
Watanzania wengi tunapenda vinavyoelea ,hatutaki kinda.
 
Nimejumuisha KODI na TOZO kwenye maelezo yangu. Wabunge na Rais wana kesi ya kutolipa Kodi stahiki.

Natambua fika Tozo zinahusu makundi yote! Lakini bado, maumivu mengi yako kwa raia wa kawaida, wanaifanya miamala kila siku ukilinganisha na hao Wabunge.
Ndio maana tunasisitizwa Tuchague Viongozi Sahihi. Naona Jambo Hili Tutajifunza Baadae kwenye Uchaguzi
 
Unafiki unatumaliza Watanzania.
Kodi zilizokuwa zikitozwa na serikali ya Awamu ya Tano kwa wafanyabiashara na wajasiria mali, wengi waliitikia wakisema mafisadi hao au wahujumu uchumi.

Kipindi cha Awamu ya Tano uonezi mwingi wa kupora, kunyang'anya, kubambika kodi na hata watu kuwekwa ndani na kufunguliwa kesi za uongo za uhujumu uchumi zilikuwepo tena nyingi sana.

Lengo lake kupata fedha kwa udi na uvuma kwa miradi ya SGR na Stiglaz Umeme na mingine mingi.

Kuna wananchi walishangilia sana uonezi uliofanywa.
Wapo viongozi walio kundi hili, Waziri Mpango wakati huo hakosekani humo.

Sasa Awamu ya Sita imerekebisha hilo ili KODI IWE KWA WATANZANIA WOTE.

Na hili linatekelezwa kwa kupitia TOZO za miamala ambazo zinamgusa kila mtu.

Hapo ndio unaona unafiki wa watu.
Hawapendi kuchangia kodi kwa maendeleo, wao wanafikiri kundi fulani tu ndio litoe kodi ili wao waneemeke.

Mshindwe, lipeni kodi Watanzania.
Tozo ni muhimu je hicho kiwango kitaleta tija? mimi nadhani kiwango bado siyo rafiki ,sera ili ili ifanikiwe ni lazima iwe shirikishi 'ineffective public policies always fail'
 
Mabwenyenye wa nchi hii wanaishi maisha ya kufuru alafu wanataka watu maskini wakatwe tozo, mwalimu, daktari anaishi kwa kutegemea mshahara wale ila wakuu wa wilaya/mikoa, wabunge, MARAS, MADAS na nk... Wanahudumiwa kila kitu na serikali nje ya mshahara wao, kwa no wasiishi kwa kutumia ujira wao? Wana uspecial gani wao? Uzalendo wa kweli ulipaswa kuanzia kwa hawa na hiki ndo kinawavunja moyo watanzania
 
Mabwenyenye wa nchi hii wanaishi maisha ya kufuru alafu wanataka watu maskini wakatwe tozo, mwalimu, daktari anaishi kwa kutegemea mshahara wale ila wakuu wa wilaya/mikoa, wabunge, MARAS, MADAS na nk... Wanahudumiwa kila kitu na serikali nje ya mshahara wao, kwa no wasiishi kwa kutumia ujira wao? Wana uspecial gani wao? Uzalendo wa kweli ulipaswa kuanzia kwa hawa na hiki ndo kinawavunja moyo watanzania
Huu ndio ujinga mliopandikizwa na wajinga wenzenu.
Sasa hao unaona ndio matajiri wako wangspi nchini dhidi ya nyie mliokubali kuitwa kijinga ati "wanyinge"?
Ukitawaliwa kiakili utabaki nyuma dsima.
Lipa tozo bana!
 
Unajua beureu ziliporwaa pesa kwa ajili gani?? Kama hujui kitu bora unyamaze ufiche ujinga wako! Wale watu wa beureu walikuwa wanaficha dola ili zipungue mitaani kisa dola ipandee..rais akaona wanasaliti nchi wakafanyiwa hivyo..sasa ww punguani unakurupuka huko fyoko fyoko hujui chochote..subir hizo tozo uone kama kuna jipyaa litakalofanywaa na hao wapuuzi.. akili yako itakaa sawaa..ila kwa kuwa ww n kipofuu hutajua hilo umekosa ilmu dunia..unaelimu yako ya hukooo
Ujinga huo kamuhadithie babu yako kijijini.
 
Ishu sio tozo, ishu ni transparency!

Tumeambiwa ni tozo za uzalendo which means ni pesa yetu wananchi basi tunaomba isichezewe na kwa kuhakikisha hilo kuwe na real time system ambayo ni kama portal mwananchi anaweza kuangalia on a daily imeingia shillingi ngapi kwenye kapu na taarifa za kutolewa pesa ziwe wazi kwamba kiasi gani kimetolewa kwenye mfuko huo na kinaenda kujenga shule au barabara gani kama tulivyokubaliana.

Sio watu wanajichotea hela tu kwa siri humo na kufanya mambo yao kwa jasho la wananchi! Haifai na wala haikubaliki na kutokana na mazoea ya ufisadi wa viongozi wa chama tawala for years hatuna imani na usalama wa tozo na ndio maana tunalalamika kukatwa michango hio!
Ndio maana nasema mkuki kwa nguruwe, kwa binadamu mchungu!
Hiyo transoarency ilikuweoo Awamu ya tano?
Mtu kachota tril 1.5 na kamfukuza CAG aliyehoji, mlikuwa wapi
?
 
Ndio maana nasema mkuki kwa nguruwe, kwa binadamu mchungu!
Hiyo transoarency ilikuweoo Awamu ya tano?
Mtu kachota tril 1.5 na kamfukuza CAG aliyehoji, mlikuwa wapi
?
Awamu ya tano hakukuwa na Tozo mind you na kwa mambo ambayo yamefanyika kama una akili timamu huwezi kuanza kuhoji ikiwa unaona miundombinu inajengwa kwa kasi yani mambo yanafanyika na kuna dira ya kiongozi aliyepo madarakani inayofanya kazi. Yapo mabaya yake pia ila hakukuwa na huu ushenzi wa kupora wananchi fedha zao kwa mgongo wa uzalendo!

Nikikuuliza msimamo wa kiongozi wa sasa ni upi unaweza elezea japo kwa machache?
 
Tozo ni muhimu je hicho kiwango kitaleta tija? mimi nadhani kiwango bado siyo rafiki ,sera ili ili ifanikiwe ni lazima iwe shirikishi 'ineffective public policies always fail'
Tusijidanganye.
Iitwe TOZO au KODI yote ni mamoja.
Hiyo hela inaingia serikalini kufanya yale yaliyotazamiwa.
Miradi ya SGR na Stiglaz Umeme yote inahitaji hiyo tozo na kodi.
Kwamba ni kwa kiwango kipi itabaki kuwa issue, swala hapan i kwamba yale yalioanzwa kujengwa kimaendeleo ni lazima yakamilike iwe kwa kodi au tozo.
 
Awamu ya tano hakukuwa na Tozo mind you na kwa mambo ambayo yamefanyika kama una akili timamu huwezi kuanza kuhoji ikiwa unaona miundombinu inajengwa kwa kasi yani mambo yanafanyika na kuna dira ya kiongozi aliyepo madarakani inayofanya kazi.

Nikikuuliza msimamo wa kiongozi wa sasa ni upi unaweza elezea japo kwa machache?
Wewe kwa sababu ulikuwa hukamuliwi ndio maana unalia sasa.
Nyie ndo haswa lengo la hii mada.
Wanafiki mliokuwa hamguswi na Magufuli, kila kikicha mnamshangilia kama hmna akili nzuri.
Sasa mmeguswa.
Lipeni tozo bana.
 
Tatzo tozo nyingi na kama una lain tatu ukifanya muamala wanakukata pote na kila ukifanya muamala unakatwa kwanini wasiweke hata 500 kila tozo bado kampuni za simu wakukate,ila acha akili itukae maana sisi maskin ndio hupenda ccm
 
Back
Top Bottom