Watanzania tusiwe wanafiki, Tozo ni muhimu kwa upana wake

Watanzania tusiwe wanafiki, Tozo ni muhimu kwa upana wake

Wewe kwa sababu ulikuwa hukamuliwi ndio maana unalia sasa.
Nyie ndo haswa lengo la hii mada.
Wanafiki mliokuwa hamguswi na Magufuli, kila kikicha mnamshangilia kama hmna akili nzuri.
Sasa mmeguswa.
Lipeni tozo bana.
Aliekwambia nilikuwa sikamuliwi ni nani? Mie siafiki uporaji wa fedha za wananchi ikiwa tunalipa kodi za majengo mpaka kwenye pipi!
 
Kuna Mtanzania alikuambia hataki kulipa kodi! Au kukatwa hizo tozo? Watu wanalalamikia matumizi yake, yaliyojaa ubadhirifu mkubwa na ufisadi wa kutisha!

Lakini pia watu wanalalamikia namna wahamasishaji wenyewe wa hizo kodi/tozo kuwa mstari wa nyuma kwa kukwepa kulipa, huku wanyonge na watu wa kawaida wakiwajibishwa ipasavyo!

Mfano mzuri ni Kesi ya Mbunge wa Ukonga Jerry Silaa kulalamikia mishahara ya Wabunge kutokukatwa kodi, Mshahara wa Rais nao tunasikia haukatwi kodi, nk. Hiki kitu ndicho kinacho amsha hisia hasi kwa raia.

Ili kodi na tozo zilipwe kwa urahisi, viongozi wawe mfano wa kuigwa kwa kulipa hizo kodi, lakini pia kuzitumia kwa matumizi sahihi! Na siyo kuzitapanya, kama ilivyo sasa.
Usichoelewa matumizi ya tozo ni nini? Madarasa 500 na zahanati zaidi ya 220 kwa makusanyo ya mwezi mmoja tu, hii ni fahari. Tukajikongoja kwa mwaka mmoja tu tatizo la madarasa na zahanati zitakwisha na tutahamia kwenye tatizo jingine. Kweli huelewi hayo!

Umeambiwa watoto wengi wa darasa la saba waliofanya mtihani wao hivi punde kufaulu kwa wingi (matokeo ya elimu bure) na hapatatosha mashuleni, hivyo ongezeko la madara ndio muarubaini wa tatizo- usichoelewa ni nini?

Akina mama waja wazito hujifungulia barabarani kuitafuta zahanati iliyo kilomita 50, sasa wanasogezewa zahanati karibu na nyumbani- nalo hilo hulielewi- Mmmmm nanamashaka!
 
H
Tatzo tozo nyingi na kama una lain tatu ukifanya muamala wanakukata pote na kila ukifanya muamala unakatwa kwanini wasiweke hata 500 kila tozo bado kampuni za simu wakukate,ila acha akili itukae maana sisi maskin ndio hupenda ccm
Hahahahahah hamna anayeipenda ila ni basi tu ujasiri wa kuvumilia kipigo cha ma afande ndio wananchi wenzangu hawana 😅
 
Usichoelewa matumizi ya tozo ni nini? Madarasa 500 na zahanati zaidi ya 220 kwa makusanyo ya mwezi mmoja tu, hii ni fahari. Tukajikongoja kwa mwaka mmoja tu tatizo la madarasa na zahanati zitakwisha na tutahamia kwenye tatizo jingine. Kweli huelewi hayo!

Umeambiwa watoto wengi wa darasa la saba waliofanya mtihani wao hivi punde kufaulu kwa wingi (matokeo ya elimu bure) na hapatatosha mashuleni, hivyo ongezeko la madara ndio muarubaini wa tatizo- usichoelewa ni nini?

Akina mama waja wazito hujifungulia barabarani kuitafuta zahanati iliyo kilomita 50, sasa wanasogezewa zahanati karibu na nyumbani- nalo hilo hulielewi- Mmmmm nanamashaka!
Mashaka ulitakiwa uwe nayo toka mwanzo tu sababu hayo madarasa, zahanati na mahospitali aliyojengaga Jakaya alijenga kwa tozo zipi?

Hizi lami na madaraja aliyoyajenga mkapa na mwenziwe Magufuli waliyajenga kwa tozo zipi?

Kwamba kipato cha nchi kimepungua kiasi kwamba lazma tuanze kupora wananchi fedha zao kwa mgongo wa uzalendo? Uliona wapi uzalendo unalazimisha raia kufanya jambo bila ridhaa yake?

The state imeshindwa kutumia resources zake kwa tija na kuunda sera nzuri ili kuleta maendeleo yani inasikitisha mpaka tumeanza kupora fedha kwa mtu mmoja mmoja. Aibu kwa kweli yani kwa Gov kusafiria nyota ya makampuni ya simu kujipatia tozo kwa kufanya double taxing
 
Usichoelewa matumizi ya tozo ni nini? Madarasa 500 na zahanati zaidi ya 220 kwa makusanyo ya mwezi mmoja tu, hii ni fahari. Tukajikongoja kwa mwaka mmoja tu tatizo la madarasa na zahanati zitakwisha na tutahamia kwenye tatizo jingine. Kweli huelewi hayo!

Umeambiwa watoto wengi wa darasa la saba waliofanya mtihani wao hivi punde kufaulu kwa wingi (matokeo ya elimu bure) na hapatatosha mashuleni, hivyo ongezeko la madara ndio muarubaini wa tatizo- usichoelewa ni nini?

Akina mama waja wazito hujifungulia barabarani kuitafuta zahanati iliyo kilomita 50, sasa wanasogezewa zahanati karibu na nyumbani- nalo hilo hulielewi- Mmmmm nanamashaka!
Miaka zaidi ya 60 ya uhuru, bado stori ni zile zile! Madarasa, madawati! Huku watawala wachache wakiishi maisha ya peponi!

Halafu unaniuliza nisicho elewa ni nini!! Ni kuona miaka zaidi ya 60, tukiwa tumejaliwa kila aina ya raslimali, lakini bado serikali inawakamua wananchi wake maskini, huku kikundi cha watu wachache tu kikizifaidi hizo raslimali.

I wish tungekua na Mtawala kama Muammar Gaddaf! Ambaye aliitumia vilivyo raslimali ya mafuta, kuboresha maisha ya wananchi wenzake wa Libya.
 
Unafiki unatumaliza Watanzania.

Kodi zilizokuwa zikitozwa na serikali ya Awamu ya Tano kwa wafanyabiashara na wajasiria mali, wengi waliitikia wakisema mafisadi hao au wahujumu uchumi.

Kipindi cha Awamu ya Tano uonezi mwingi wa kupora, kunyang'anya, kubambika kodi na hata watu kuwekwa ndani na kufunguliwa kesi za uongo za uhujumu uchumi zilikuwepo tena nyingi sana.

Lengo lake kupata fedha kwa udi na uvuma kwa miradi ya SGR na Stiglaz Umeme na mingine mingi.

Kuna wananchi walishangilia sana uonezi uliofanywa.

Wapo viongozi walio kundi hili, Waziri Mpango wakati huo hakosekani humo.

Sasa Awamu ya Sita imerekebisha hilo ili KODI IWE KWA WATANZANIA WOTE.

Na hili linatekelezwa kwa kupitia TOZO za miamala ambazo zinamgusa kila mtu.

Hapo ndio unaona unafiki wa watu.

Hawapendi kuchangia kodi kwa maendeleo, wao wanafikiri kundi fulani tu ndio litoe kodi ili wao waneemeke.

Mshindwe, lipeni kodi Watanzania.
Niliwaambia ccm bila ya magufuli ni mafii ya bata
Usitufanya wapumbavu kumbuka samia aliponda polisi kukusanya mapato kupitia makosa ya barabarani hadi sasa hivi ajali za barabarani zimerudi kwa wingi tunasikia kila siku mabasi yanaua sasa kwanini unaacha kukusanya mapato ya mamillion kupitia makosa kama hayo unaweka tozo ya kinafiki ambayo ni kodi juu ya kodi ,kwanini asipandishe kodi kwenye pombe ,sisi tunajua kiongozi mpumbavu na kiongozi mwenye akili hizi ni zama za
MAFISADI LEGACY DHIDI YA MAGUFULI LEGACY
 
Hamkulalamika hivyo wakati wa Magufuli, kuwa fedha wanazonyang'anya wafanya biashara zinaenda wapi?

Arusha Beureu De Change zimeporwa na vyombo vya serikali, hela ilienda wapi?

Ndio maana nasema tusiwe wanafiki.
Hao ni wezi watz hatutaki hata kuwasikia mafisadi mpwa wakubwa ,kitu ninacho kuambia ni lazima MAGUFULI LEGACY ishinde hii ya mama yenu ya MAFISADI LEGACY
 
Kuna Mtanzania alikuambia hataki kulipa kodi! Au kukatwa hizo tozo? Watu wanalalamikia matumizi yake, yaliyojaa ubadhirifu mkubwa na ufisadi wa kutisha!

Lakini pia watu wanalalamikia namna wahamasishaji wenyewe wa hizo kodi/tozo kuwa mstari wa nyuma kwa kukwepa kulipa, huku wanyonge na watu wa kawaida wakiwajibishwa ipasavyo!

Mfano mzuri ni Kesi ya Mbunge wa Ukonga Jerry Silaa kulalamikia mishahara ya Wabunge kutokukatwa kodi, Mshahara wa Rais nao tunasikia haukatwi kodi, nk. Hiki kitu ndicho kinacho amsha hisia hasi kwa raia.

Ili kodi na tozo zilipwe kwa urahisi, viongozi wawe mfano wa kuigwa kwa kulipa hizo kodi, lakini pia kuzitumia kwa matumizi sahihi! Na siyo kuzitapanya, kama ilivyo sasa.
Kwamba hiyo mbunge kulalamika kuwa mishahara yao ikatwe Kodi nayo ni ufisadi?
 
Watanzania wengi tunapenda vinavyoelea ,hatutaki kinda.
Kuunda manaake ni nini? Uliwahi sikia lini Marekani kuna tozo za uzalendo au Canada toka kuasisiwa kwake? We have Bogus leaders na ndio maana tunaonekana vituko tu.

Tumeshakubalianaga kilimo ni uti wa mgongo wa taifa ila mbolea bei juu, masoko ya uhakika hakuna! System ya stakabadhi tu usimamizi ni changamoto such a minor system.

Leteni basi wanaoyaweza hata kwa kuwakodisha wafanye mambo ni aibu sana karne ya 21 kwa taifa kutegemea mbeleko ya IMF na world Bank nchi ina madini kibao, wanyama kibao tu na uoto mwingi wa asili!

Tuleteeni wanaoweza tujifunze kwao tunasema wachina rafiki zetu ila tumekuwa daraja la wao kufanikiwa kwa kutufanya soko lao badala nasie tuombe ujanja wa kiteknolojia tuanze kuzalisha vitu vya kuuziana humu humu africa but made in Tz! Tumeamua kuwapa na bandari kabisa ili wajaze takataka zao toka China hapa nchini. Natabiri tutakuwa masikini mara 20 zaidi ya hapa tulipo ni swala la muda tu!
 
Sasa hizi tozo mnazokamua si ni sawa na kurudisha kodi ya kichwa vima nyie, kwa nini mnakata VAT sasa kwenye huduma na bidhaa ambazo kila mwananchi anapofanya manunuzi na kulipia bidhaa mbalimbali analipa, na zile PAYE mnazokata wafanyakazi bado haziwatoshi.

Unataka kuaminisha watu kipindi cha Magu wafanyabiashara pekee ndo walikuwa wanalipa kodi. Kimsingi hakuna mfanyabiashara anye lipa kodi zaidi ya kuwasilisha yale makato ya VAT ambayo ni mwananchi aliyelipa. Kawambie waliokutuma hii imegonga mwamba.
Mkuu,wafanya biashara wanalipa kodi nyingi tu Corporate tax,Personal income tax,Withhoding.hata hyo VAT unayosema wanakatwa wananchi bado kuna mzigo mkubwa unalala kwa wafanya biashara sababu si wote waliosajiliwa VAT na wakati mwingine wanalazimika kuchaji price sawa na wasiosajiliwa sababu ya ushindani.hyo PAYE inayolipwa na wafanyakazi wa serikali haiwezi kufanya miradi peke yake,kumbuka wafanyakazi wa serikali hawazidi hata laki tatu na wengi wana mishahara midogo kama walim na police,so unategemea hvyo vilaki wanavyokatwa ndo vifanye miradi mikubwa?
 
Hao ni wezi watz hatutaki hata kuwasikia mafisadi mpwa wakubwa ,kitu ninacho kuambia ni lazima MAGUFULI LEGACY ishinde hii ya mama yenu ya MAFISADI LEGACY
Ninyi mlikuwa hanlipinkodi zoxote, sasa karibu kuchangia maendekeo ya Taifa.
Kwenu kila aliyefanya biashara ni fisadi.
 
Miaka zaidi ya 60 ya uhuru, bado stori ni zile zile! Madarasa, madawati! Huku watawala wachache wakiishi maisha ya peponi!

Halafu unaniuliza nisicho elewa ni nini!! Ni kuona miaka zaidi ya 60, tukiwa tumejaliwa kila aina ya raslimali, lakini bado serikali inawakamua wananchi wake maskini, huku kikundi cha watu wachache tu kikizifaidi hizo raslimali.

I wish tungekua na Mtawala kama Muammar Gaddaf! Ambaye aliitumia vilivyo raslimali ya mafuta, kuboresha maisha ya wananchi wenzake wa Libya.
Hata mimi zamani nilifikiri kuwa kwa kuwa na viwanda vingi(vya silaha za kijeshi, usindikaji chakula, magari nk) Marekani haitozi kodi wananchi wake. Nilikuwa wrong!

Miaka 60! Ni kweli, lakini tatizo lililokuwepo ni watu wachache waliokuwa wanalipa kodi kwa maendeleo ya wananchi wote. Mkoloni alikuwa na kodi ya kichwa, Nyerere akaifuta. Mkapa baada ya kuona mambo magumu akairudisha - Ukusanyaji wake ukawa ni adha kwa wananchi. Haikudumu sana ikafutwa. Magufuli akajaribu kuwabana sana matajiri - Biashara nyingi zikafa na lawama nyingi zikatawala. Mama kaja na tozo za kistaarabu na kizalendo na zitazowahusisha watanzania wote toka apatae sh 2000 mpaka mwenye bilioni. Kwa mtindo wa Mama tutapata wachangiaji wa maendeleo kama milioni 40 bila shuruti/kwa hiari yako mwenyewe.

Kwa miaka 60 hatujaacha kuzaa, tena mpaka uzazi wa majira tukaukataa - Eeh kuzaa tunazaa lakini kuchangia wachangie matajiri tu, wapi na wapi. Tulikuwa milioni 20 walipa kodi hao hao leo milioni 60 walipa kodi wale wale na tunataka tuione Tanzania nyingine- Mmmm, hiyo hata Gwajima na miujiza yake hawezi.
 
Kuunda manaake ni nini? Uliwahi sikia lini Marekani kuna tozo za uzalendo au Canada toka kuasisiwa kwake? We have Bogus leaders na ndio maana tunaonekana vituko tu.

Tumeshakubalianaga kilimo ni uti wa mgongo wa taifa ila mbolea bei juu, masoko ya uhakika hakuna! System ya stakabadhi tu usimamizi ni changamoto such a minor system.

Leteni basi wanaoyaweza hata kwa kuwakodisha wafanye mambo ni aibu sana karne ya 21 kwa taifa kutegemea mbeleko ya IMF na world Bank nchi ina madini kibao, wanyama kibao tu na uoto mwingi wa asili!

Tuleteeni wanaoweza tujifunze kwao tunasema wachina rafiki zetu ila tumekuwa daraja la wao kufanikiwa kwa kutufanya soko lao badala nasie tuombe ujanja wa kiteknolojia tuanze kuzalisha vitu vya kuuziana humu humu africa but made in Tz! Tumeamua kuwapa na bandari kabisa ili wajaze takataka zao toka China hapa nchini. Natabiri tutakuwa masikini mara 20 zaidi ya hapa tulipo ni swala la muda tu!
Wewe hujakaa nchi za
huwezi ukawa na akili timamu. unajua ratural esources zilizopo kwnye hii, unajua population ya hii nchi ni kubwa kuliko nchi yoyoye E. Africa.
Hayo ndo mawazo ya mtu ambaye si mvivu tu bali mjinga pia.
Hizo natural resuorces unazozisema si unaziona?
Kazivune ulipe tozo!
 
Unafiki unatumaliza Watanzania.

Kodi zilizokuwa zikitozwa na serikali ya Awamu ya Tano kwa wafanyabiashara na wajasiria mali, wengi waliitikia wakisema mafisadi hao au wahujumu uchumi.

Kipindi cha Awamu ya Tano uonezi mwingi wa kupora, kunyang'anya, kubambika kodi na hata watu kuwekwa ndani na kufunguliwa kesi za uongo za uhujumu uchumi zilikuwepo tena nyingi sana.

Lengo lake kupata fedha kwa udi na uvuma kwa miradi ya SGR na Stiglaz Umeme na mingine mingi.

Kuna wananchi walishangilia sana uonezi uliofanywa.

Wapo viongozi walio kundi hili, Waziri Mpango wakati huo hakosekani humo.

Sasa Awamu ya Sita imerekebisha hilo ili KODI IWE KWA WATANZANIA WOTE.

Na hili linatekelezwa kwa kupitia TOZO za miamala ambazo zinamgusa kila mtu.

Hapo ndio unaona unafiki wa watu.

Hawapendi kuchangia kodi kwa maendeleo, wao wanafikiri kundi fulani tu ndio litoe kodi ili wao waneemeke.

Mshindwe, lipeni kodi Watanzania.
Awamu ya tano taratibu za kodi zilifuatwa ila wale wazoefu wa kukwepa walipatikana. Tozo hatupingi bali kiwango ndoo kero.
 
Swala ni kiasi gani........sio kwamba kusiwepo Tozo haiwezekani Tozo ikawa kubwa kuliko charge ya mwenye mtandao wakati serikali haijaewekeza chochote pale.
 
Ishu sio tozo, ishu ni transparency!

Tumeambiwa ni tozo za uzalendo which means ni pesa yetu wananchi basi tunaomba isichezewe na kwa kuhakikisha hilo kuwe na real time system ambayo ni kama portal mwananchi anaweza kuangalia on a daily imeingia shillingi ngapi kwenye kapu na taarifa za kutolewa pesa ziwe wazi kwamba kiasi gani kimetolewa kwenye mfuko huo na kinaenda kujenga shule au barabara gani kama tulivyokubaliana.

Sio watu wanajichotea hela tu kwa siri humo na kufanya mambo yao kwa jasho la wananchi! Haifai na wala haikubaliki na kutokana na mazoea ya ufisadi wa viongozi wa chama tawala for years hatuna imani na usalama wa tozo na ndio maana tunalalamika kukatwa michango hio!
Kabisa hizi hela zingetumika kwauwazi na usawa wananchi tungeelewa sasa hivi tuaona tunajambaziwa tu
 
Unafiki unatumaliza Watanzania.

Kodi zilizokuwa zikitozwa na serikali ya Awamu ya Tano kwa wafanyabiashara na wajasiria mali, wengi waliitikia wakisema mafisadi hao au wahujumu uchumi.

Kipindi cha Awamu ya Tano uonezi mwingi wa kupora, kunyang'anya, kubambika kodi na hata watu kuwekwa ndani na kufunguliwa kesi za uongo za uhujumu uchumi zilikuwepo tena nyingi sana.

Lengo lake kupata fedha kwa udi na uvuma kwa miradi ya SGR na Stiglaz Umeme na mingine mingi.

Kuna wananchi walishangilia sana uonezi uliofanywa.

Wapo viongozi walio kundi hili, Waziri Mpango wakati huo hakosekani humo.

Sasa Awamu ya Sita imerekebisha hilo ili KODI IWE KWA WATANZANIA WOTE.

Na hili linatekelezwa kwa kupitia TOZO za miamala ambazo zinamgusa kila mtu.

Hapo ndio unaona unafiki wa watu.

Hawapendi kuchangia kodi kwa maendeleo, wao wanafikiri kundi fulani tu ndio litoe kodi ili wao waneemeke.

Mshindwe, lipeni kodi Watanzania.
Ukweli mchungu ila wote tunapaswa kulipa kodi. Tukishalipa tuwabane viongozi waache kuchezea kodi zetu kwa kufanya mambo ya anasa. Haya mambo ya kuendesha V8 kila upande na bila sababu za msingi yakomeshwe. Mbona mikutano mingine inaweza kufanyika virtually? Kwanini wanaenda na kutoka Dodoma kama wanaenda sinza mjini kila week?
Tubadilike ili tujenge nchi yetu kwa hiki kipato kidogo kilichopo
 
Back
Top Bottom