Watanzania uvivu wa kusoma mambo utatuponza,tusome katiba pendekezwa jamani.

Watanzania uvivu wa kusoma mambo utatuponza,tusome katiba pendekezwa jamani.

Watanzania sisi wavivu wa kusoma kwa kweli.
Hiyo katiba hata hao walio na access sijui kama wataisoma.
Tushaambia kura ni ndio tena tumeshapata kisingizio copy zipo chache?mtoa mada labda serekali itoe motisha.
 
Unaposema kitu ambacho hukipendi toa mifano hai ili ujibiwe kwa ufasaha, ni wapi hapo ambapo unasema haijajali wananchi? wananchi gani hao? Au ukitaka matakwa yako binafsi? Kwa taarifa yako hii katiba inayopendekezwa imejali makundi mbalimbali na ukweli wa suala hili unapatikana katika katiba inayopendekezwa katika sura ya tano ibara ya 56 (haki za makundi madogo katika jamii), pia soma ibara ya 46 haki za wakulima, wafugaji, wavuvi na wachimba madini (watumiaji wa ardhi), kwa maneno hayo naamini nitakuwa nimekusaidia kukujibu na kukutoa wasiwasi kuhusu wananchi.

Mhhh hapo ndio uwezo wako wa kufikiri ulipofikia unaweza kutuambia kwa nini walitoa zile tunu za taifa na ile ya madaraka ya rais ukinisaidia hapo nitaisoma zaidi ya hapo siihitaji.
 
mhhh hapo ndio uwezo wako wa kufikiri ulipofikia unaweza kutuambia kwa nini walitoa zile tunu za taifa na ile ya madaraka ya rais ukinisaidia hapo nitaisoma zaidi ya hapo siihitaji.

tunu za taifa ktk katiba inayopendekezwa hazijafutwa na mambo ya madaraka ya rais yako kama yalivyoandikwa katika katiba hii, labda nikusaide kitu kimoja, soma katiba inayopendekezwa hasa hasa katika sura ya kwanza ibara ya 5 utaziona hizo tunu za taifa ambazo zimetajwa zikiwemo lugha ya kiswahili, muungano, utu na udugu, amani na utulivu.
 
mhhh hapo ndio uwezo wako wa kufikiri ulipofikia unaweza kutuambia kwa nini walitoa zile tunu za taifa na ile ya madaraka ya rais ukinisaidia hapo nitaisoma zaidi ya hapo siihitaji.

tunu za taifa ktk katiba inayopendekezwa hazijafutwa kijana zipo ktk sura ya kwanza ibara ya 5, tunu hizo ni lugha ya kiswahili, muungano, utu na udugu, amani na utulivu, lakini pia kuhusu suala la madaraka ya rais hayajafutwa yako vizuri katika sura ya nane ibara ya 81, nenda kasome katiba hii sasa ktk hayo maeneo ili uyaelewe vema.
 
Kwa bahati mbaya walio wengi hawana haja ya kuisoma kwani hawaikubali. Toka mambo ya msingi toka rasimu ya Warioba kuondolewa walio wengi hawaikubali. Kwa hiyo nyinyi mnaoikubali endeleeni nayo huko mbeleni tutaandika upya katiba ya watu wote na sio hiyo iliyotungwa na kundi la watawala.
Umesema ukweli ambao unawauma sana hao wapiga deal
 
umesema ukweli ambao unawauma sana hao wapiga deal

mwakaboko na tindo mtaongea sana mpaka mchanike midomo yenu, ukweli wa katiba hii kila mmoja anaujua nyie mnabisha tuu kufurahisha midomo yenu na watu wengine, watanzania hawawaelewi lolote juu ya hilo na watawapinga cku ya kupiga kura, poleni sana kubalini ukweli tuu sisi wote ni watanzania tuwe wazalendo kwa nchi yetu.
 
Wadau isomeni kwanza...mimi pia nilikuwa na mtazamo huu huu ila nimeipitia kipengele kimoja hadi kingine...kuna baadhi sikubaliani navyo kwa mtazamo wangu ila tuisome kwanza ndio tuamue....

Kura yangu ni HAPANA.
 

tunu za taifa ktk katiba inayopendekezwa hazijafutwa kijana zipo ktk sura ya kwanza ibara ya 5, tunu hizo ni lugha ya kiswahili, muungano, utu na udugu, amani na utulivu, lakini pia kuhusu suala la madaraka ya rais hayajafutwa yako vizuri katika sura ya nane ibara ya 81, nenda kasome katiba hii sasa ktk hayo maeneo ili uyaelewe vema.

Naona unajitahidi kuipigia debe umepewa ngapi?Tumekwambia hatuitaki hivyo hatuba haja ya kuisoma!
 
kwa muda mrefu nimekuwa nikijiuliza kwa watanzania wenzangu, kwa sasa kila mtu kwa anaweza kutunufaika na maendeleo ya technolojia ya mawasiliano bila kujalisha yupo mjini ama vijijini,kwa sasa ni rahisi hata kwa watu ambao hawana elimu ya kawaida, unamkuta yumo fb,wasap na pia kuangalia taarifa zingine kupitia simu! Katika siku za hivi karibuni watu wengi wamekuwa wakilalamikia kutopata nakala za katiba,lakini mie kengele leo imegonga kichwani nikaona watu walivyo na ueledi mkubwa wa matumizi ya mitandao ya kijamii na katiba pendekezwa jitihada kidogo tu mtu waweza ipata kupitia mitandao hiyo.sasa je swali la kujiuliza kwamba kama si ushabiki wa kisiasa tu,kweli mtu ukipania kuisoma huwezi kuisoma kweli? Ama tukisikia kauli za kisiasa tunapandia hapo hapo,sidhani kama tunaweza kwenda kwa mfumo huu,nijuavyo mie watanzania waliowengi hawana utamanaduni wa kusomo mrundikano wa maandishi hilo hakuna hata mmoja anagusia,ila kusema nakala hazijasambazwa zile za hard copy,hiyo ndo inakuwa habari ya mjini. Mie nadhani kutokana na umhimu wa katiba katika mstakabali wa nchi kwa siku zijazo kila mtu angepumnzika kidogo tu kuchat na kuingia online kuisoma katika inayopendekezwa,na si kuishia malalamiko ambayo nahisi ni ya wachache kwamba hawawezi kupata nakala ya katiba pendekezwa, ila wengine ni kama hatutaki tu kuifikia katiba hiyo kwa ya kimitandao.nawasilisha jamvini mawazo tete haya
wewe umesikia kengele za mazombi ukiwa usingizini hna lolote, hiyo sio hoja ya kuleta jamvini kuwa walio wengi hawana utamaduni wa kusoma mrundikano wa maandishi ha ha ha ha ha ha kweli mzembe utamjua tu,acha uvivu wa kufikiri kama huwezi kusoma ni wewe mwenyewe usiwaunganishe huma watz wenzio tuko smart.
 
kwa bahati mbaya walio wengi hawana haja ya kuisoma kwani hawaikubali. Toka mambo ya msingi toka rasimu ya warioba kuondolewa walio wengi hawaikubali. Kwa hiyo nyinyi mnaoikubali endeleeni nayo huko mbeleni tutaandika upya katiba ya watu wote na sio hiyo iliyotungwa na kundi la watawala.


nenda kalale wapishe wenye hoja wachangie huelewi maudhui yake na hata ukielewa haitakusaidia wewe si raia wa tanzania.
 
Back
Top Bottom