Watanzania walioko Ukraine watakiwa kurudi Tanzania

Watanzania walioko Ukraine watakiwa kurudi Tanzania

Bima mbele ya kutunguliwa..😀

Kuna BIMA ya majanga ; vita inaingizwa humo!!! Lakini Bongo hawana utamaduni wa kujikinga na majanga ndio maana hata masoko yakiungua watu wanafilisika!! Sio utani kuna wakati ndege za ATC zilikuwa zinaruka bila BIMA!! Unbelievable!!!
 
China yupo na mimi hadi mda huu, france,Japan,Germany na UK hawawezi kuwapiga China,Iran na Korea. Vita hii ndio mwisho wa USA kwenye uso wa dunia. Rafiki yang Van amenihakikishia hilo ila kwa sasa hajibu sms zangu ila nitawaletea update maana nachat nae
Kuna kitu kinaitwa balance of terror, ukielewa hii concept utajua Russia na marekani hawawezi pigana
 
Kuna BIMA ya majanga ; vita inaingizwa humo!!! Lakini Bongo hawana utamaduni wa kujikinga na majanga ndio maana hata masoko yakiungua watu wanafilisika!! Sio utani kuna wakati ndege za ATC zilikuwa zinaruka bila BIMA!! Unbelievable!!!
Hata Kama Kuna bima uhai wa mtu haulipwi huwezi sogelea hatari.
 
Hata Kama Kuna bima uhai wa mtu haulipwi huwezi sogelea hatari.

BIMA sio mbadala wa uhai wa mtu bali ni kipoza machungu tu!!! Je kuendesha gari sio hatari? Watu hukata BIMA kama kinga just in case hiyo hatari inajitokeza.
 
Ucdhani Russia ni mwepesi hvyo ndugu tangu enzi na enzi America hajawah kuipiga moja kwa moja

Nadhani hakulisikia onyo la Biden kwa Wamarekani waliokuwa Ukraine, kwamba wangesubiri mpaka vita vianze, Marekani isingekuwa na uwezo wowote wa kufanya evacuation ya raia wake. Kwamba kujaribu kufanya hivyo, ingekuwa kuanzisha World War III.
 
Kushabikia vita isiyo na sababu na kumuita Mvamizi ni Mwamba ni kushangilia ushetani.

Ushetani ni kumkaribisha adui wa jirani yako/ndugu yako sebuleni kwako. Matokeo ya kutosikiliza hoja za wakubwa huwa na adhabu kubwa
 
I might not agree with your assestment of the situation considering,you made the assestment prior to Russia de-militarizing Ukraine overnight..
...
Screenshot_20220225-062700~2.jpg
 
PUTIN: AFRIKA HAITOKAA IWE HURU

"Afrika haitokaa iwe HURU. Waafrika wanawaamini Wazungu, Wamarekani na Wachina zaidi kuliko wanavyojiamini wao wenyewe....hawajiamini wao wenyewe hata kidogo.

Mzungu au mtu mweupe anafanya makosa Afrika tena makosa ya jinai ila hakuna hatua za kisheria zitakazochukuliwa dhidi yake kwa sababu mamlaka za Afrika zinatutazama sisi weupe kama miungu, jambo ambalo liko mbali sana na ukweli.

Mtu mweusi (Mwafrika) anaweza kuteswa, kunyanyaswa na hata kuuawa kinyama Ulaya lakini hakuna mamlaka yoyote ya Afrika inayoweza kuuliza wala kuhoji.

Waafrika wamejikubali na kuamini kuwa wao ni watu DHAIFU wasio na tumaini haswa linapokuja suala la kupambana na Wazungu, Wamarekani na Wachina. Mzungu, Mmarekani au Mchina anaweza kumdhalilisha, kumtukana, kumpiga na hata kumuua Mwafrika katika ardhi ya Afrika tena kwenye nchi yake au nje ya Afrika na Viongozi wa Afrika wataliona hilo na kila mmoja atajiweka kana kwamba hakuona wala kusikia.

Adui wa Mwafrika ni Mwafrika. Mwafrika mpe silaha, pesa au ahadi ya madaraka madogo tu kwa sharti moja tu la kumuua Mwafrika mwenzake, atamuua kinyama kuliko ulivyotarajia. Adui wa Mwafrika sio mzungu, sio Mmarekani wala sio mchina. Adui wa Mwafrika ni AKILI na fikra zake na ndio maana leo Wazungu, Wamarekani, Waarabu na Wachina wameitawala tena Afrika kwa kutumia dini, Elimu, uchumi, teknolojia, siasa na utamaduni.

Waafrika ni watu wanaochukiana na wasioaminiana na ndio maana Afrika haiwezi kuungana na haitokaa iungane kuwa na dola imara. Chuki ya wenyewe kwa wenyewe na utengano ndio inayowapa wakoloni wao nguvu ya kuendelea kunyonya rasilimali za Afrika."

Je unakubaliana na Rais Vladmir Putin?
Je ni kipi unaweza kuongeza kuhusu Afrika?

Quote
 
Habari za jioni wana Jamii Forums, kwa kweli nimeona suala la ndugu Watanzania walioko Ukraine kutakiwa kurudi Tanzania na wengine kutolewa na mataifa yao sababu kubwa ni nini? Putin anahusikaje? Tujuzane.

Maestro de Quimica!!OPView attachment 2129084
"Juhudi binafsi" hii nchi ni ya mijibwa tu! Hivi watu wapo kujirusha na kusafiri na midege ya kukodi kwa kisingizio cha kutembeza mabakuli wakati watoto wetu wanajificha chini ya miamba kukwepa makombora ya Rusia! Tumeshindwa hata kutumia asilimia 0.001 ya matumizi mabovu kuwaleta wanetu nyumbani jamani! CCM mlaaniwe hadi kizazi cha nne!!
 
Ngoma ikiwambwa sana hupasuka. Putin yuko vizuri sana lakini nahisi sifa zinampanda kichwani sasa. Akiivamia Ukraine itakuwa keshwapa chance kubwa mahasimu wake hasa USA kummaliza kabisa.

Kupitia mtafaruku huu, USA atapata support kutoka kwa washirika wake hivyo kutimiza ndoto yake ya siku nyingi ya kuidunda Russia.

USA alishajua kuwa peke yake haiwezi Russia, lakini sasa atapata support ya wengine.
hupo upo sahihi lakini ni mtu mmoja anayweza aidha kufanya marekani waingie au watulie,
 
View attachment 2129683

Inasikitisha sana waafrika tunadharaulika sana……na viongozi wetu hili naona hawalioni …bado wanapiga magoti kwao wakiamini ukombozi wetu utatoka kwao.

Hivi najiuliza haya madeni tutayalipa na nini km rasilimali kubwa zetu washachukua wanazimiliki….utalii ni mdogo sana, we consume what we do not produce…na tunachozalisha tunauziana wenyewe kwa wenyewe…
Sasa huyu kunyaland na yeye kaingiliaje ugomvi wa vigogo? mambo mengine ni kupiga kimya tu watayamaliza wenyewe kwa wenyewe.....
 
Wapelekewe Airbus nchi ya jirani ili iwachukue huko. Itue Romania ama Poland maana anga la Ukraine imefungwa.
 
Nilidhani ubalozi ungewafanyia taratibu za kuwasafirisha kumbe wanawashauri? Duuuh... Kila mtu ana pesa ya haraka km anatoka na daladala Kariakoo kwenda Mbagala?

Hao wazazi ukute walishalipa ada wanasubiri likizo mwisho wa mwaka huko ndipo mtoto arudi, sahivi ghafla tu hakuna kuwafanyia juhudi za ziada?

Twafwaaa..
Ni tabu kwel mkuu
 
Yule aliyemuomba Madame aombe vita na Rwanda achukuliwe apelekwe Ukraine.

Ili kutengeneza fair ground akiwa huko akabidhiwe guruneti moja, bastola moja na AK 47 moja.

Kwakua yeye anaamini vita ni kama kwenye muvi hata chakula asigewe tunaamini atakua anawapora maadaui.
Nadhani sasa mnaelewa nini maana ya "TUMIA KURA YAKO VIZURI" unachagua kiongozi, anagombana na kiongozi mwenzake, mnalipuliwa wewe na ndugu zako na kura zenu na mifugo yenu[emoji2375]
 
Back
Top Bottom