Russia hakuitawala Africa sio kwa kupenda. Kwanza haikuwepo Urusi Kama Urusi. Na nchi zilizokuwepo maeneo hayo miaka ya 1800 zilikuwa dhaifu Sana. Zilizopigana Mara kwa mara na zisizoweza kutoka nje kuja Afrika kutawala.
Kumbuka ata Marekani haikuitawala Africa.
Sawa na Italy iliambulia eritria tu baada ya kuchelewa kwake.
So Urusi haikuja kuikomboa Afrika Bali kupigania maslahi yake dhidi ya mabepari Afrika. Na imehusika na kuwa karibu na madikteta na tawala za kijeshi akiwa ndio muuzaji mkuu wa slaa kwa Afrika kwa Sasa.
Eti imehusika kuwa karibu na madikteta na tawala za kijeshi. Watu wanapolishwa maneno na watu wa magharibi. Ebu taja hao madikteta na tawala za kijeshi Africa ambazo Russia au Urusi amekuwa nazo karibu. Ingekuwa hivyo Urusi ingekuwa karibu na Dictotor Idd Amin Dada, cha ajabu Urusi ilisaidia Tanzania.
Marekani haikuitawala Africa lakini imekuwa chanzo cha migogoro na kuiba rasilimali za Africa ikishirikiana na wadau wake. Kwanini Marekani haimalizi migogoro ya DRC? Kwa nini marekani iliunga mkono Serikali ya kibaguzi dhidi ya Waafrika?
Unahitaji kujua baada ya ukoloni wa kuitawala Africa physical kuondolewa mbinu nyingine ilikuwa ni ukoloni mamboleo ambau umeendelea kutumika na mataifa makubwa hasa Marekani. Na huu ukoloni ni mbaya kuliko ule wa mwanzo.
nikujulishe tu, Italy iliitawala Ethiopia kwa almost miaka isiyopungua sita. Na waliimarisha miundo mbinu mingi tu kama reli, viwanja vya ndege, barabara, kuna majengo mengi hadi leo ya waitalia. Mpaka walipokuja kushindwa vita na kuondoka. Japo nashangaa Ethiopia wanapenda kusema kuwa hawajatawaliwa. Wakati Italia ilikaa na wakawa na mamlaka kamili. Baada ya waitalia kuondolewa, Ethiopia ilikuwa under British protectorate, na wakati huo Mfalme Haile selaise alikuwa wingereza alikoenda kuomba msaada wa kuondoa wa Italia.
Waethiopia usheherekea hiyo siku kila mwaka walivyojikomboa, na imefanyika tu wiki iliyopita. Cha hajabu wanajisifia hawajatawaliwa! Mie uwa nawaeleza nchi ambayo haikutawaliwa pekee ni Liberia. Cha ajabu wanadai ni wao tu hawakutawaliwa, huu ni uongo. Muitali kaja kaa kaimarisha utawala, utadai hajakutawala? Wanadai kulikuwa na resistance hivi ni nchi gani Africa haikuwa na resistance?
Hii uwa naifananisha na Zanzibar kudai mapinduzi yaliongozwa na Abeid Amani karume, na kutomtambua John Okero. Ukweli na historia kupindishwa.
Ok, Marekani ndiyo aneongoza kwa mikakati ya kimapinduzi katika nchi kadhaa Africa, wakishirikiana na Ufaransa wala si Rassia. Marekani ukienda kinyume na maslahi yake anakuita dicteta mara hakuna demokrasia, mfano walivyomgeuka Mugabe kisa kurejesha ardhi kwa weusi.
Urusi ilipigania ukombozi wa nchi mbalimbali Africa, na hasa Africa ya kusini ikipinga ubaguzi. Kumbuka Marekani ilikuwa side ya Makaburu. Sasa ni wapi Urusi imetetea madikiteta ebu wataje? Urusi ilikuwa against kinachofanyika DRC, wakati marekani wakimuweka dikteta Mabutu Seseseko wakishirikiana na wabeligiji.
Urusi ililaani kuuwawa kwa Gadaffi, japo Gadaffi alikuwa mshirika wa Marekani toka miaka na miaka. Hakuwa mshirika wa Urusi. Marekani ikamgeuka Gadaffi kwa maslahi yao.
Umesikia wapi Urusi au Russia imeingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine kama si Marekani. Chukua muda utafakari. Vyombo vinavyotumika kunyonya nchi zinazoendelea viko chini ya nani kama si Marekani? IMF na World Bank? Tafakari?