Watanzania wapo kwenye njia panda baina ya Kiswahili na Kingereza

Hizi zako ni stimu za copper, acha kununua sukari ya kwota kwota na nusu nusu kilo wewe mkikuyu.
Wacha kufanya makosa ya kuliita hili zwazwa mkikuyu. Ni heri likijiita lenyewe, maanake si msapere wala mkenya. Yeye ni yule yule, yaani karubandika
 
Point of correction. Kiswahili kilikuwepo pwani ya africa mashariki miaka mingi kabla ya ukoloni. Mjerumani alikikuta na kukisambazwa nchi nzima kama lugha ya mawasiliano na wenyeji. Nyerere alikikuta Kiswahili kimeshasambaa nchini na kukitumia kutafuta uhuru nchi nzima. Tulipopata uhuru alikiendeleza kama kugha ya Taifa.Tuendelee kuanzia hapo.
 
Wakubali tu kutumia kiingereza mashuleni ila wasikubali kiswahili kififie alafu mwishowe kife kama mbwa koko.


Kiswahili kinathaminiwa Tanzania kwa sababu tu kinatumika Shuleni, kama kikifutwa itakuwa kama Kenya, Kenya Kiswahili ni lugha ya chokoraa, house boys gardener &Co.. lkn waliosoma au wanaojiona wamesoma hawatumii Kiswahili, kwa kifupi Kenya Kiswahili ni lugha ya utani na mzaha, demu wangu wa Kikenya nilivyomfahamu aligoma kuongea Kiswahili mpaka alipofika TZ ndo akajua kwamba kumbe Kiswahili ni Lugha ya heshima pia na leo hii anajivunia kuongea Kiswahili na kuwaona Wakenya wenzake wajinga!
 


Uko sawa kabisa, wengi wanaamini kabisa kwamba TZ tunaongea Kiswahili shauri ya Nyerere, siyo kweli, Nyerere aliteka hiyo sifa lkn ukweli ni kwamba alikikuta Kiswahili kama ulivyosema na hata kutumika Shuleni siyo Nyerere aliyeanzisha bali tangia ukoloni Kiswahili kilikuwa kama lugha ya kufundishia Elimu ya msingi, sema ndo hivyo kama yalivyo mambo mengi Nyerere ameliteka na hilo kwamba yeye ndiye aliyeanzisha, kwanza kama ukiangalia kwa undani Nyerere ndiye aliyekirudisha Kiswahili nyuma kwani alikataaa kisitumike Elimu ya juu, laiti kama Wazungu (Wajerumani) wangebakia TZ basi leo hii labda Kiswahili kingekuwa kinatuimika hadi Elimu ya juu!
 
Naona wanzuki ya leo haijatiwa maji mengi sana.
 
Asilimia kubwa Watanzania wanafeli kwa kutokujua kiingereza. Kiingereza ni lugha ya kimataifa na inatumiwa na mataifa mengi, wewe ni nani ujitenge nayo? Labda uwe na utajiri wa kutosha na bidhaa zako uandike kwa kiswahili ili mataifa mengine wajifunze kiswahili. Mfano mzuri ni nchi tatu za Afrika mashariki, wenzetu wapo mbali kielimu kwa kutilia maanani kiingereza. Tuamke sasa tujifunze kiingereza
 
Acha kudanganya watu wewe, watoto wotewa Kikwete wamesoma shule na Clio bus serikali.
 
Utaoa lini mkuu? Tunataka kuja kula pilau kwenye sherehe
 
Kiswahili is native to Kenya and Tanzania. Kenya is a more popular country of the two countries and if you mention Swahili anywhere in the world, Kenya comes to mind, not Tanzania. And yes, some copy paste: The Swahili tribe is found along the coastal areas of Kenya, as well as Tanzania and Mozambique. They make up less than 1% of the total Kenyan population. Today, the largest populations of Swahili can be found in Zanzibar and Mombasa. So mtu kutoka Mwanza or Arusha kuja kuargue ati ni mswahili kushinda mtu kutoka Lamu ama Malindi ama Mombasa ni nonsense. Those three towns are more Swahili than 99% of Tanzania
 
Swahili was used in those countries waaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaay before Nyerere came to Kenya. Its even native to coastal Kenya
 
Jaribu kutofautisha utamaduni wa waswahili na lugha ya kiswahili japo lugha ipo kwenye utamaduni ila kwa huku bongo karibia nchi nzima na makabila mengi hasa ya kibantu yamesaidia kwenye kukuza lugha ya kiswahili ndo maana hata mtu wa Mwanza au hata Arusha nae anaweza tu kua mswahili kwa huku mswahili sio kabila bali ni tamaduni na kwa hii nchi utamaduni wa mswahili haupo pwani tu umetapakaa karibia nchi nzima (kiswahili ni mchanganyiko wa lugha za kibantu na za watu wageni hivyo hivyo kwa utamaduni wa waswahili umechanganya tamaduni za kibantu na za wageni waliokuja ukanda huu uswahili sio kabila kama huko mnavyochukulia ndo mana huko mtu akisema mswahili tayari mshafikiria ni mtu wa pwani)
 
Sidhani kama kuna sababu yoyote ya kutumia nguvu kupingana na ukweli kwamba Nyerere ana mchango mkubwa sana katika kueneza na kukikuza kiswahili Tanzania. Kabla ya uhuru kiswahili kilikua kinazingumzwa zaidi katika ukanda wa pwani kama ilivyokua kwa Kenya, baada ya uhuru Nyerere aliweka juhudi za makusudi za kukikuza kiswahili nchi nzima Kwa kukifanya kuwa lugha ya kufindishia ktk shule za msingi jambo ambalo hadi leo Kenya haijalifanya, vipi Kenya inaweza kusema kiswahili ni lugha us Taifa wakati shughuli mbalimbali zote za serikali ikiwemo binge, mahakama, na karibu hotuba zote za viongozi hutolewa kwa kiingereza?

Hivyo hivyo ndivyo ilivyokua ktk ukabila, Nyerere alikuta Tanzania ina ukabila no watemi no machifu mbalimbali walikua hawataki kuachia maeneo yao, Nyerere alijua ukabila ni hatari Sana, Malena kabisa akaanza kazi ya kupambana na ukabila, kitu ambacho mzee Jommo Kenyatta hakukifanya.
 

Uswahili na Mswahili vilianzia Pwani, wengine wote mlidakia tu, unakuta mtu hujui kuongea lugha yako ya asili hata salamu kisa unaona ushamba, eti kuongea Kiswahili pekee yake ndio unajiona mjanja, kwa uzembe hutaki kujifunza lugha yoyote nyingine, ukisikia mtu anaongea kingereza unamuita mtumwa, akiongea lugha ya asili unamuita mshamba, halafu hata uandishi wenu wa Kiswahili huwa majanga.
Hamna kitu cha ovyo kwamba uwe una uandishi wa ovyo kwenye Kiswahili, halafu kingereza hukijui, lugha ya asili huijui, huna lugha hata moja uliyoimudu, unakua kama zombi.
 
Hivi sisi (Tanzania) Kiingereza ni cha nini wakati Uingereza iko kilomita zaidi ya 10,764+ toka Tanzania. Hatuhitaji lugha za kikoloni ili tuendelee, tuboreshe elimu yetu tutafika tu. Kwani China, Japan, na nchi zingine huko Asia wamefikaje? Kiingereza si kila kitu, hatukihitaji hata kidogo.LAZIMA tuondokane na ujinga wa kubeza lugha za watu, waangalieni wapuuzi wacameroon jinsi wanavyouana kugombania lugha za watawala wao (Kifaransa na kiingereza). Ni ujinga sana huu.
 
Sisi ni WaTanzania na lugha yetu ya taifa ni Kiswahili hayo mengine yakuongezea kachumbari tu
 
Vile kunaenda, bora kusoma ki china ukiwa mkenya. Hata matangazo yako kwa lugha ya madarin

Bongolala shindeni hapo. Hawa wachina wenyewe wanaelewa kingereza sana. Wanafunzi huko uchina siku hizi wanafunzwa kingereza kuanzia darasa la tatu.
 
Bongolala shindeni hapo. Hawa wachina wenyewe wanaelewa kingereza sana. Wanafunzi huko uchina siku hizi wanafunzwa kingereza kuanzia darasa la tatu.
Halafu wakawaletea midude yao imeandikwa kichina teh haya nendeni pia mkasome kichina
 

Kiswahili kimetumiwa Kenya hadi siku za ukoloni. Ujinga wenu wa kulimbikizia Nyerere sifa hana.
Na kama ulivyoambiwa hapo juu, Kiswahili kimetandaa kwa sababu ya juhudi za wakenya.

Ili ufunze watu lugha mpya, lazima kwanza uongee lugha yao. In short, you have to speak 2 languages, something Tanzanians can't do.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…