Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 16,419
- 26,594
Waziri Mkuu wa Uingereza, Margaret Thatcher aliwahi kusema, serikali haina duka wala biashara au shamba. Serikali inaendeshwa kwa kodi zinazotozwa kwa wananchi wake.
Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.
Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote. Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.
Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao. Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.
Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.
Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).
Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.
Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.
Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.
Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.
Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.
Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote. Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.
Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao. Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.
Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.
Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).
Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.
Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.
Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.
Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.