Watanzania watu wa ajabu, wanapenda maendeleo lakini hawataki kugharamia hayo maendeleo kwa kodi

Watanzania watu wa ajabu, wanapenda maendeleo lakini hawataki kugharamia hayo maendeleo kwa kodi

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
Waziri Mkuu wa Uingereza, Margaret Thatcher aliwahi kusema, serikali haina duka wala biashara au shamba. Serikali inaendeshwa kwa kodi zinazotozwa kwa wananchi wake.

Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.

Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote. Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.

Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao. Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.

Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.

Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).

Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.

Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.

Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.

Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.
 
Nenda kasome tena uchumi na maswala ya kodi..kwa kifupi serikali inatakiwa itengeneze mazingira mazuri ya kufanya biashara watu wawekeze yenyewe ije kuchukua kodi..sasa shida inaanzia hapa serikali inataka ichukue kiasi sawa na aliefanya uwekezaji.

1. Kwenye miamala ya simu service prodiver (Tigo,Vodacom, Airtel) wao wameshafanya uwekezaji kwenye infrastructure, minara,manpower etc. Kwaio wao warudishe gharama zao wameanzisha huduma kadha wa kadha i.e kutuma na kupokea hela sasa kwa kuangalia gharama walizotumia wameweka kiwango fulani cha ili kufikisha gharama hizo husika kwa mtumiaji wa mwisho.

2. Shida inaanzia hapa i.e kutuma kiasi fulani ni 400 tsh na kiasi cha kutolea ni 300 tshs...tukumbuke kwamba hio kampuni ya simu baada ya kutoa mapato na matumizi yake faida iliopatikana inatozwa 30% (corporate tax) pia inalipa PAYE kutoka kwa income tax kitu kisichoeleweka ni kutaka serikali nayo ichukue hela toka kwenye hizo gharama za kutuma na kutolea wakati baadae inakuja kukata kodi katika mahesabu ya mwisho wa mwaka hicho ndo hakikubaliki maana mzigo wote anasukumiziwa mlaji wa mwisho(mtuma hela)

3. Porojo za kujenga madaraja, mashule, mahospitali hazina uzito sababu hayo majengo sio kwamba yameanza kujengwa baada ya tozo kuanzishwa serikali imekua ikikusanya kodi toka sehemu mbali mbali tangu kupatwa kwa uhuru sasa iweje ndo useme kwamba tozo hizi ni za kufanyia hivyo vitu,kodi zingine zinaenda kufanyia vitu gani? Hapo unakuta kuta LC200 na Lc300 zinanunualiwa kwenye misafara etc isio kua na tija

4. Kwanza kabisa kujenga barabara,mahospitali, mashule hayo ni majukumu ya serikali sio fadhila..siku watu watakapo amka na kujua majukumu ya serikali na wajibu wake kwa wanachi ni upi ndio tutaelewena..hakika hio siku itafika hapo waongo waongo ndo watakapo kua wamefikia mwisho.

Principles zipi za taxation zinazotumika kutoza kitu mara mbili mbili?
 
Nenda kasome tena uchumi na maswala ya kodi..kwa kifupi serikali inatakiwa itengeneze mazingira mazuri ya kufanya biashara watu wawekeze yenyewe ije kuchukua kodi..sasa shida inaanzia hapa serikali inataka ichukue kiasi sawa na aliefanya uwekezaji.

1. Kwenye miamala ya simu service prodiver (Tigo,Vodacom, Airtel) wao wameshafanya uwekezaji kwenye infrastructure, minara,manpower etc. Kwaio wao warudishe gharama zao wameanzisha huduma kadha wa kadha i.e kutuma na kupokea hela sasa kwa kuangalia gharama walizotumia wameweka kiwango fulani cha ili kufikisha gharama hizo husika kwa mtumiaji wa mwisho.

2. Shida inaanzia hapa i.e kutuma kiasi fulani ni 400 tsh na kiasi cha kutolea ni 300 tshs...tukumbuke kwamba hio kampuni ya simu baada ya kutoa mapato na matumizi yake faida iliopatikana inatozwa 30% (corporate tax) pia inalipa PAYE kutoka kwa income tax kitu kisichoeleweka ni kutaka serikali nayo ichukue hela toka kwenye hizo gharama za kutuma na kutolea wakati baadae inakuja kukata kodi katika mahesabu ya mwisho wa mwaka hicho ndo hakikubaliki maana mzigo wote anasukumiziwa mlaji wa mwisho(mtuma hela)

3. Porojo za kujenga madaraja, mashule, mahospitali hazina uzito sababu hayo majengo sio kwamba yameanza kujengwa baada ya tozo kuanzishwa serikali imekua ikikusanya kodi toka sehemu mbali mbali tangu kupatwa kwa uhuru sasa iweje ndo useme kwamba tozo hizi ni za kufanyia hivyo vitu,kodi zingine zinaenda kufanyia vitu gani? Hapo unakuta kuta LC200 na Lc300 zinanunualiwa kwenye misafara etc isio kua na tija

4. Kwanza kabisa kujenga barabara,mahospitali, mashule hayo ni majukumu ya serikali sio fadhila..siku watu watakapo amka na kujua majukumu ya serikali na wajibu wake kwa wanachi ni upi ndio tutaelewena..hakika hio siku itafika hapo waongo waongo ndo watakapo kua wamefikia mwisho.

Principles zipi za taxation zinazotumika kutoza kitu mara mbili mbili?
Suala la kodi si tozo pke yake.
Sula ni pana zaidi.

Ujiulize wewe mwenyewe, je umewekeza wapi laki yako moja ili irudishe faida na kodi juu?
Tupanue mawazo yawe outward looking na si inward looking.
Watu wasifikirie kuwa mwekezaji ni yule mhindi, yule mzungu au yule warabu.

Uwekezaji unaanzia na sisi wenyewe.
Na watanzania wengi wakiwekeza uzalishaji huo ndio utatoa na kodi hata kama ni kidogo sana.
 
Suala la kodi si tozo pke yake.
Sula ni pana zaidi.

Ujiulize wewe mwenyewe, je umewekeza wapi laki yako moja ili irudishe faida na kodi juu?
Tupanue mawazo yawe outward looking na si inward looking.
Watu wasifikirie kuwa mwekezaji ni yule mhindi, yule mzungu au yule warabu.

Uwekezaji unaanzia na sisi wenyewe.
Mzee kama haufanyi biashara huwezi kunielewa ila ipo hivi kwa mfumo wa kodi wa Tanzania ili uweze kubaki na faida + mtaji ni lazima ukwepe kodi ndo utasurvive sababu mazingira ya kufanya biashara ni magumu sana ofisi zinazochukua kodi + tozo zipo zaidi ya 4 na kila moja ina nguvu usipp weka mambo sawa unajiandaa kukwamishwa...haswa kwa wale tunaofanya biashara ambazo zimekua regulated na taasisi zingine...kikwako kikubwa ni serikali na mfumo mzima wa kodi..sio rafiki kwa ustawi au ukuaji wa baishara na mitaji...ila kama wewe ni mvaa tai huwezi nielewa...
 
Shida ya hapa kwetu kodi zetu hazina mpangilio.

Wewe unayejipeleka kusajili biashara au kampuni yako ndiye unayekomolewa bila kiasi. Kuna wakulima wakubwa sana lakini jee kuna kodi inayoeleweka wanayolipa? Wafanyabiashara wadogo au raia wengine wanalipa kodi ipi? Hata kama ni shilingi mia kwa mwaka lakini kila raia anatakiwa alipe kodi.

Ndiyo maana mjerumani alianzisha kodi ya kichwa ili kila mwananchi asikwepe kulipa kodi.
 
Waziri Mkuu wa Uingereza, Margaret Thatcher aliwahi kusema, serikali haina duka wala biashara au shamba. Serikali inaendeshwa kwa kodi zinazotozwa kwa wananchi wake.
Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.

Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote.
Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.

Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao.
Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.

Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.

Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).

Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.
Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.

Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.
Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.
Kwa nini mnaposha kwa makusudi? Haya uliyoandika ulisikia lini watanzania wakiyasema? Mbona kodi zilikuwepo na hakuna aliyelalamika?
 
Shida ya hapa kwetu kodi zetu hazina mpangilio.

Wewe unayejipeleka kusajili biashara au kampuni yako ndiye unayekomolewa bila kiasi. Kuna wakulima wakubwa sana lakini jee kuna kodi inayoeleweka wanayolipa? Wafanyabiashara wadogo au raia wengine wanalipa kodi ipi? Hata kama ni shilingi mia kwa mwaka lakini kila raia anatakiwa alipe kodi.

Ndiyo maana mjerumani alianzisha kodi ya kichwa ili kila mwananchi asikwepe kulipa kodi.
Naungana na wewe.

Tatizo la ukadiriaji, ukusanyaji na tax base , ni tatizo sugu nchini. Wanansiasa wameliingilia na kulitumia kama fimbo ya aidha kukomoana au hata kumfunga mfanya biashara.

Lakini kimsingi lazim ziwepo sera ambazo zitamlenga KILA MWANANCHI alipe kodi, gata kama ni kidogo sana.
Miundombinu inatumiwa na kila mtu, kodi yake inaweza kuwa kodi ya kichwa.
 
Naungana na wewe.
Tatizo la ukadiriaji, ukusanyaji na tax base , ni tatizo sugu nchini.Wanansiasa wameliingilia na kulitumia kama fimbo ya aidha kukomoana au hata kumfunga mfanya biashara.
Lakini kimsingi lazim ziwepo sera ambazo zitamlenga KILA MWANANCI alipe kodi, gata kama ni kidogo sana.
Miundombinu inatumiwa na kila mtu, kodi yake inaweza kuwa kodi ya kichwa.
Kweli kabisa. Unaona hawa wanasiasa wetu wao ndiyo wa kwanza kujipa mamalaka ya kujisamehe kodi lakini wanataka wenzao walipe kodi za kila aina.
 
Watanzania walio wengi hawana tatizo na hizo kodi. Tatizo lipo kwa watunzaji wa hizo kodi! Wana ujanja ujanja mwingi.

Maana hao viongozi ndiyo wapigaji wakubwa wa hizo kodi zao, kupitia maisha yao ya kifahari wanayoishi, huku wale watoaji wakiishi maisha ya dhiki kubwa! Wanalazimisha wananchi masikini kulipa hizo kodi, huku wenyewe wakijipa misamaha!


Wamejaza vyeo lukuki kwenye serikali huku vikiwa havina umuhimu/ulazima wowote ule! Mfano Wakuu wa Wilaya, Mikoa, Mar Das, Ma Ras, Wabunge wa viti maalum, nk!! Hawa wote wanakula mishahara na posho za bure tu! Hivyo serikali inatakiwa kupunguzwa matumizi yake yasiyo ya lazima, na ipunguze vitendo vyake vya rushwa na ufisadi ili wananchi tulipe kodi kwa moyo.

Hawana ubunifu wa kutengeneza vyanzo vipya! Na badala yake wanakata kodi mara mbili, au zaidi kwenye vyanzo vile vile! Nchi ina raslimali za kila aina! Ila karibia zote wamezibinafsisha kwa Mabeberu, halafu mwisho wa siku wanapewa mrabaha mbuzi wa 3%! Na wakati mwingine hawapati chochote!

Katika mazingira ya aina hii, kwa yeyote yule atakayepata nafasi ya kukwepa hizo kodi, akwepe tu! Maana hakuna namna nyingine ya kupata unafuu wa maisha.
 
Waziri Mkuu wa Uingereza, Margaret Thatcher aliwahi kusema, serikali haina duka wala biashara au shamba. Serikali inaendeshwa kwa kodi zinazotozwa kwa wananchi wake.
Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.

Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote.
Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.

Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao.
Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.

Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.

Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).

Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.
Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.

Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.
Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.
Shida tuna imani ndogo na wanaotoza.

Tuliambiwa kuna mkopo wa covid,na ajabu pesa ya tozo inafanya kazi ile ile ya mkopo wa covid!
Kuna wasi wasi sana na huenda tunapigwa
 
Watanzania walio wengi hawana tatizo na hizo kodi. Tatizo lipo kwa watunzaji wa hizo kodi! Wana ujanja ujanja mwingi.

Maana hao viongozi ndiyo wapigaji wakubwa wa hizo kodi zao, kupitia maisha yao ya kifahari wanayoishi, huku wale watoaji wakiishi maisha ya dhiki kubwa! Wanalazimisha wananchi masikini kulipa hizo kodi, huku wenyewe wakijipa misamaha!


Wamejaza vyeo lukuki kwenye serikali huku vikiwa havina umuhimu/ulazima wowote ule! Mfano Wakuu wa Wilaya, Mikoa, Mar Das, Ma Ras, Wabunge wa viti maalum, nk!! Hawa wote wanakula mishahara na posho za bure tu! Hivyo serikali inatakiwa kupunguzwa matumizi yake yasiyo ya lazima, na ipunguze vitendo vyakevya rushwa na ufisadi ili wananchi tulipe kodi kwa moyo.

Hawana ubunifu wa kutengeneza vyanzo vipya! Na badala yake wanakata kodi mara mbili, au zaidi kwenye vyanzo vile vile! Nchi ina raslimali za kila aina! Ila karibia zote wamezibinafsisha kwa Mabeberu, halafu mwisho wa siku wanapewa mrabaha mbuzi wa 3%! Na wakati mwingine hawapati chochote!

Katika mazingira ya aina hii, kwa yeyote yule atakayepata nafasi ya kukwepa hizo kodi, akwepe tu! Maana hakuna namna nyingine ya kupata unafuu wa maisha.
Kwa kweli hili la KILA MTU ALIPE KODI wanasiasa wanalikwepa.
Ifike muda hili suala la wanasiasa lazima kulipa kodi lipigiwe kura na wananchi.
 
Waziri Mkuu wa Uingereza, Margaret Thatcher aliwahi kusema, serikali haina duka wala biashara au shamba. Serikali inaendeshwa kwa kodi zinazotozwa kwa wananchi wake.
Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.

Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote.
Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.

Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao.
Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.

Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.

Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).

Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.
Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.

Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.
Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.
Tatizo la tanzania ni ujinga basi..acheni kizazi hiki kipite na ujinga wake..
 
Tatizo la tanzania ni ujinga basi..acheni kizazi hiki kipite na ujinga wake..
Kwa kukusaidia hakuna nchi iliyoendelea kwa kubebesha wananchi maskini mzigo wa kodi

Europe imeendelea kwa sababu ya colonialism, nchi za uarabuni zimeendelea kwa sababu ya mafuta, south Africa iliendelea kwa sababu ya madini, china imeendelea kwa speed ya juu kwa sababu walikua na Kodi ndogo ikavutia viwanda kutoka nchi za magharibi kwenda kufungua china sababu ya Kodi ndogo

Hio nchi ambazo zinakodi kubwa wameweka baada ya kuendelea na kuwa ustaarbu Mkubwa mfano nchi za gulf countries ndo wameanza kuweka Kodi kama VAT walikua hawana

Ni jambo la ajabu kuwabebesha mzigo mkubwa wananchi maskin kama watanzania huku ukiwaambia nchi Ina utajiri wa kutupa wa rasilimali
 
Kwa kukusaidia hakuna nchi iliyoendelea kwa kubebesha wananchi mzigo wa kodi

Europe imeendelea kwa sababu ya colonialism, nchi za uarabuni zimeendelea kwa sababu ya mafuta, south Africa iliendelea kwa sababu ya madini, china imeendelea kwa speed ya juu kwa sababu walikua na Kodi ndogo ikavutia viwanda kutoka nchi za magharibi kwenda kufungua china sababu ya Kodi ndogo

Hio nchi ambazo zinakodi kubwa wameweka baada ya kuendelea na kuwa ustaarbu Mkubwa mfano nchi za gulf countries ndo wameanza kuweka Kodi kama VAT walikua hawana

Ni jambo la ajabu kuwabebesha mzigo mkubwa wananchi maskin kama watanzania huku ukiwaambia nchi Ina utajiri wa kutupa wa rasilimali
Hawa viongozi wetu hamna kitu! Nchi yetu inapakana na DRC yenye raslimali za kika aina! Badala ya kujenga viwanda vya kuchenjua madini kule Kigoma na vile vya maliasili ya misitu, ili tunufaike kupitia kodi na mauzo ya hayo madini!

Wao wako busy kuwadhulumu wananchi wao masikini wa mali na kipato! Hali ikiendelea, hatutashangaa kushuhudia vikundi vya kigaidi vikianza kujitokeza ndani ya nchi yetu. Watu watachoka kuonewa na kudhulumiwa, huku viongozi wenyewe wakiishi maisha ya peponi.
 
Back
Top Bottom