Watanzania watu wa ajabu, wanapenda maendeleo lakini hawataki kugharamia hayo maendeleo kwa kodi

Watanzania watu wa ajabu, wanapenda maendeleo lakini hawataki kugharamia hayo maendeleo kwa kodi

Waziri Mkuu wa Uingereza, Margaret Thatcher aliwahi kusema, serikali haina duka wala biashara au shamba. Serikali inaendeshwa kwa kodi zinazotozwa kwa wananchi wake.
Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.

Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote.
Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.

Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao.
Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.

Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.

Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).

Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.
Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.

Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.
Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.
VAT ni nini?
 
Watu wako tayari kulipa kodi+tozo
Na serikali wabane matumizi,waache matumizi yasiyokuwa na tija na mambo ya anasa anasa
Twende sawa
Siyo unakamua kule alafu nyie huko mnajiachiaaaa tu

Ova
 
Kwanza na wao wakati umefika wakatwe kodi na walipishwe tozo.
Ili twende sawa sawa

Ova
 
Watu wako tayari kulipa kodi+tozo
Na serikali wabane matumizi,waache matumizi yasiyokuwa na tija na mambo ya anasa anasa
Twende sawa
Siyo unakamua kule alafu nyie huko mnajiachiaaaa tu

Ova
Serikali iachane na sula la kuwanunulia mawaziri magari ya kifahari.
Watumie magari yale ya kula mafuta kidogo kama X-Trail.
 
Wasalaam,

Kama jina la uzi linavyosema, nauliza ni kweli kwamba vyanzo vya mapato ni tozo tuu hatuna angle nyingine ambayo inaweza kumpumzisha Mtanzania na kumfanya asijute kuwa Mtanzania?

Kwa nijuavyo mimi kuna Tax revenues na non tax revenues, sasa ni jitihada gani zimefanyika katika kuhakikisha tunapata fedha za kutosha kupitia resources zetu ili kumpimzisha mwananchi na tozo/taxes?

Ni wakati sasa wa nchi hii kuwa na VISION ya kueleweka na sio kila anayeingia analeta mambo yake, nchi hii ina madini ya kutosha na ya kila aina, ina gesi ya kutosha na ina bandari ina mifugo, bahari ya uvuvi, ardhi yenye rutuba vitu ambavyo ni muhimu katika ukanda huu, ni kwa namna gani hivi vitu vinasaidia wananchi.

Viongozi ni wakati sasa muwe wabunifu na kuacha kufikiria kirahisi rahisi, mkumbuke the more you are taxing people the more you rise their awareness, so are you ready to dig your own graves?
 
Waziri Mkuu wa Uingereza, Margaret Thatcher aliwahi kusema, serikali haina duka wala biashara au shamba. Serikali inaendeshwa kwa kodi zinazotozwa kwa wananchi wake.
Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.

Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote.
Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.

Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao.
Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.

Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.

Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).

Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.
Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.

Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.
Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.
Mi nahis umeandika ujingaaaaa
 
Wasalaam,

Kama jina la uzi linavyosema, nauliza ni kweli kwamba vyanzo vya mapato ni tozo tuu hatuna angle nyingine ambayo inaweza kumpumzisha Mtanzania na kumfanya asijute kuwa Mtanzania?

Kwa nijuavyo mimi kuna Tax revenues na non tax revenues, sasa ni jitihada gani zimefanyika katika kuhakikisha tunapata fedha za kutosha kupitia resources zetu ili kumpimzisha mwananchi na tozo/taxes?

Ni wakati sasa wa nchi hii kuwa na VISION ya kueleweka na sio kila anayeingia analeta mambo yake, nchi hii ina madini ya kutosha na ya kila aina, ina gesi ya kutosha na ina bandari ina mifugo, bahari ya uvuvi, ardhi yenye rutuba vitu ambavyo ni muhimu katika ukanda huu, ni kwa namna gani hivi vitu vinasaidia wananchi.

Viongozi ni wakati sasa muwe wabunifu na kuacha kufikiria kirahisi rahisi, mkumbuke the more you are taxing people the more you rise their awareness, so are you ready to dig your own graves?
Haya ndio mawazo mfu ya watu wapenda vya bure.
Mtu anasema kuna madini mengi tu ya bure, uvuvi na ardhi yenye rutuba.
Halafu mtu huyu anategemea hizo rasilmali ztenmee kwa miguu zenyewe kwenda Hazina!!!
Mtu anaongea na kujitoa kutoka kwenye scenario, its them, not me kuleta mapato, mimi ni mnufaika tu!

Hivi tumelogwa na nani kwa kutokuwa na moyo wa uwekezaji sisi wenyewe?
 
1. Gesi za kila aina
2. Madini ya kila aina
3. Utalii - Vivutio vya kila aina
4. Maji ya kutosha
5. Samaki wa kila aina
6. Ardhi yenye rutuba kulima mazao ya kila aina
7. Misitu
8. Bandari kuhudumia nchi za jirani
9. Mtaji wa watu
10. AMANI

Yote hapo juu hayana tija yoyote kwa nchi yetu kwa sababu tunaongozwa na viongozi wa ovyo, hawana maono na ubinafsi/kujijali wao kwanza badala wananchi.
Kwa juhudi zako wewe mwenyewe , umewekeza nini?
Au unamsubiri mjombatoka Uarabuni, Ulaya, Uchina -akukatie pori, alete hela zake za mkopo wa uwekezaji, aajiri wafanyakazi na azalishe mali.

Wewe uko ofisini kusubiri kodi!!
Hapo ndipo tulipologwa!
 
Sio wajinga wanasiasa walishawaaminisha nchi hii Ina utajiri wa rasilimali wa kutupa Sasa kwanin uwabebeshe mzigo wa kodi
Rasilimali ambayo bado huja anza kuitumia sio rasilimali.. mfano madini yaliyopo chini ya ardhi ni mengi sana ila kwa vile hayaja anza kutumika hayana faida bado
 
Waziri Mkuu wa Uingereza, Margaret Thatcher aliwahi kusema, serikali haina duka wala biashara au shamba. Serikali inaendeshwa kwa kodi zinazotozwa kwa wananchi wake.

Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.

Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote. Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.

Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao. Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.

Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.

Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).

Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.

Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.

Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.

Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.
Lengo lako kubwa ni kutibua watu nyongo. Halafu ukae kando uone wanavyochemka...
 
Nenda kasome tena uchumi na maswala ya kodi..kwa kifupi serikali inatakiwa itengeneze mazingira mazuri ya kufanya biashara watu wawekeze yenyewe ije kuchukua kodi..sasa shida inaanzia hapa serikali inataka ichukue kiasi sawa na aliefanya uwekezaji.

1. Kwenye miamala ya simu service prodiver (Tigo,Vodacom, Airtel) wao wameshafanya uwekezaji kwenye infrastructure, minara,manpower etc. Kwaio wao warudishe gharama zao wameanzisha huduma kadha wa kadha i.e kutuma na kupokea hela sasa kwa kuangalia gharama walizotumia wameweka kiwango fulani cha ili kufikisha gharama hizo husika kwa mtumiaji wa mwisho.

2. Shida inaanzia hapa i.e kutuma kiasi fulani ni 400 tsh na kiasi cha kutolea ni 300 tshs...tukumbuke kwamba hio kampuni ya simu baada ya kutoa mapato na matumizi yake faida iliopatikana inatozwa 30% (corporate tax) pia inalipa PAYE kutoka kwa income tax kitu kisichoeleweka ni kutaka serikali nayo ichukue hela toka kwenye hizo gharama za kutuma na kutolea wakati baadae inakuja kukata kodi katika mahesabu ya mwisho wa mwaka hicho ndo hakikubaliki maana mzigo wote anasukumiziwa mlaji wa mwisho(mtuma hela)

3. Porojo za kujenga madaraja, mashule, mahospitali hazina uzito sababu hayo majengo sio kwamba yameanza kujengwa baada ya tozo kuanzishwa serikali imekua ikikusanya kodi toka sehemu mbali mbali tangu kupatwa kwa uhuru sasa iweje ndo useme kwamba tozo hizi ni za kufanyia hivyo vitu,kodi zingine zinaenda kufanyia vitu gani? Hapo unakuta kuta LC200 na Lc300 zinanunualiwa kwenye misafara etc isio kua na tija

4. Kwanza kabisa kujenga barabara,mahospitali, mashule hayo ni majukumu ya serikali sio fadhila..siku watu watakapo amka na kujua majukumu ya serikali na wajibu wake kwa wanachi ni upi ndio tutaelewena..hakika hio siku itafika hapo waongo waongo ndo watakapo kua wamefikia mwisho.

Principles zipi za taxation zinazotumika kutoza kitu mara mbili mbili?
Unafaa kuwa waziri wa fedha, alafu MWINGULU akalime huko milima SEKENKE
 
Watanzania walio wengi hawana tatizo na hizo kodi. Tatizo lipo kwa watunzaji wa hizo kodi! Wana ujanja ujanja mwingi.

Maana hao viongozi ndiyo wapigaji wakubwa wa hizo kodi zao, kupitia maisha yao ya kifahari wanayoishi, huku wale watoaji wakiishi maisha ya dhiki kubwa! Wanalazimisha wananchi masikini kulipa hizo kodi, huku wenyewe wakijipa misamaha!

Wamejaza vyeo lukuki kwenye serikali huku vikiwa havina umuhimu/ulazima wowote ule! Mfano Wakuu wa Wilaya, Mikoa, Mar Das, Ma Ras, Wabunge wa viti maalum, nk!! Hawa wote wanakula mishahara na posho za bure tu! Hivyo serikali inatakiwa kupunguzwa matumizi yake yasiyo ya lazima, na ipunguze vitendo vyakevya rushwa na ufisadi ili wananchi tulipe kodi kwa moyo.

Hawana ubunifu wa kutengeneza vyanzo vipya! Na badala yake wanakata kodi mara mbili, au zaidi kwenye vyanzo vile vile! Nchi ina raslimali za kila aina! Ila karibia zote wamezibinafsisha kwa Mabeberu, halafu mwisho wa siku wanapewa mrabaha mbuzi wa 3%! Na wakati mwingine hawapati chochote!

Katika mazingira ya aina hii, kwa yeyote yule atakayepata nafasi ya kukwepa hizo kodi, akwepe tu! Maana hakuna namna nyingine ya kupata unafuu wa maisha.
Kweli leo nimeamini watu wenye akili zao wako uraiani alafu zero brain ndo ziko madarakani, hasa Mwigulu yule [emoji1664]

Big up sana brother.
 
Lengo lako kubwa ni kutibua watu nyongo. Halafu ukae kando uone wanavyochemka...
Njoo huku Stocholm, Sweden na uine wananchi wake wanavyokatwa kodi kwa kila kitu.
Lakini kodi za wenzetu zinatumika vizuri sana.
Wabunhe wanalipa kodi, na hata mawaziri.

Kodi zinatumika kuendeleza afya, usafiri, uendeshaji miji na elimu ni bure.
 
Suala la kodi si tozo pke yake.
Sula ni pana zaidi.

Ujiulize wewe mwenyewe, je umewekeza wapi laki yako moja ili irudishe faida na kodi juu?
Tupanue mawazo yawe outward looking na si inward looking.
Watu wasifikirie kuwa mwekezaji ni yule mhindi, yule mzungu au yule warabu.

Uwekezaji unaanzia na sisi wenyewe.
Na watanzania wengi wakiwekeza uzalishaji huo ndio utatoa na kodi hata kama ni kidogo sana.
Siyo lazima uwekeze ndio ulipe kodi, kodi inalipwa na mlaji. Nikitumia fedha zangu ktk manunuzi ninalipa kodi pia.
 
Waziri Mkuu wa Uingereza, Margaret Thatcher aliwahi kusema, serikali haina duka wala biashara au shamba. Serikali inaendeshwa kwa kodi zinazotozwa kwa wananchi wake.

Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.

Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote. Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.

Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao. Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.

Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.

Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).

Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.

Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.

Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.

Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.
Ukifuatilia malalamiko kwa undani, siyo kuwa watu hawaoni umuhimu wa kulipa kodi, la hasha, bali ni uhalisia (fairness) ya kodi/tozo yenyewe. Mfano mimi mwajiriwa nakatwa kodi kwenye mshahara, halafu nikienda benki kuchukua mshahara nakatwa kodi tena kwenye mshahara ule ule. Pili matumizi ya serekali na taasisi zake ni ya kufuru. Chukulia mfano waziri mwenye dhamana anakuja na tozo kwenye mwamala hata wa Tzs 5,000 wakati huo huo ananunua gari la Tzs 500m. Yes tukamuliwe kodi/tozo - na ni wajibu wetu kulipa kodi - lakini siyo fedha zisifujwe na wakubwa.
 
Ukifuatilia malalamiko kwa undani, siyo kuwa watu hawaoni umuhimu wa kulipa kodi, la hasha, bali ni uhalisia (fairness) ya kodi/tozo yenyewe. Mfano mimi mwajiriwa nakatwa kodi kwenye mshahara, halafu nikienda benki kuchukua mshahara nakatwa kodi tena kwenye mshahara ule ule. Pili matumizi ya serekali na taasisi zake ni ya kufuru. Chukulia mfano waziri mwenye dhamana anakuja na tozo kwenye mwamala hata wa Tzs 5,000 wakati huo huo ananunua gari la Tzs 500m. Yes tukamuliwe kodi/tozo - na ni wajibu wetu kulipa kodi - lakini siyo fedha zisifujwe na wakubwa.
Kwa hiyo njia sahaihi ni kukomalia waziri asitumie vibaya mali ya umma, au alipie matumizi yake yanayoonekana ni anasa.
 
Back
Top Bottom