Watanzania watu wa ajabu, wanapenda maendeleo lakini hawataki kugharamia hayo maendeleo kwa kodi

Watanzania watu wa ajabu, wanapenda maendeleo lakini hawataki kugharamia hayo maendeleo kwa kodi

Waziri Mkuu wa Uingereza, Margaret Thatcher aliwahi kusema, serikali haina duka wala biashara au shamba. Serikali inaendeshwa kwa kodi zinazotozwa kwa wananchi wake.

Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.

Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote. Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.

Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao. Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.

Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.

Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).

Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.

Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.

Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.

Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.

Uko sahihi, je zile raslimali mnazosema tunazo mpaka wazungu watuonea wivu ziko wapi, kwanini zisiuzwe ili kutupatia fedha?

Unashangaa watu kutaka serikali itoe huduma zote, wakati kila hela za kodi zikitolewa na wananchi zinaitwa ni fedha za rais? Kwanini zisiitwe kodi za wananchi ili watu wasione Serekali ndio yenye hizo fedha?

Tozo za nini wakati viongozi wanatumia fedha za wananchi bila huruma? Kama rais alienda huko nje ambako hajapigiwa kura, akapikizwa basi na hakufa, kwanini hapa ambapo amepigiwa kura atembee na misururu mirefu ya magari kwa kisingizio cha kulinda usalama wake?
 
Watz hupinga kila kitu Cha serikali,hakuna walichounga mkono,walipinga kuhama analogia,walipinga shule za kata,walipinga vitambulisho vya nida, wanapinga,wanapinga mbolea ya ruzuku...hawana jema
Wewe ni mrundi?

Watanzania hatupingi kulipa kodi ndio maana umeajiriwa kuendesha gari la 500M lililonunuliwa kwa kodi zetu
 
Kazi ya serkali ni kubuni vyanzo vya kodi kwa kutumia rasilimali zake

Kazi ya serikali ni kuendesha taasisi zake zote ikiwemo wizara ya Elimu na Afya. Kujenga madarasa na Vituo vya Afya ni wajibu siyo 'favour' wala haiwezi kusemwa ni mafanikio! Ni wajibu wa serikali iliyopo madarakani

Watanzania wanalipa kodi kwa bidhaa zote na huduma wanazotumia.
Kukusanya kodi ni sehemu tu, matumizi ya kodi ni sehemu nyingine

Mafanikio ya kodi yanatokana na mambo mawili, kukusanya na matumizi yake. Katika nchi yetu matumizi ya hovyo yasiyo na ulazima yanagharimu serikali na mzigo huo anautwisha mwananchi kwa jina la TOZO

Waziri Nchemba kasema kuna watu 500 wanalipwa mishahara ya scale ile ile ya kuteuliwa na Rais ingawa hawafanyi kazi hizo. Haya ni matumizi mabaya ya kodi yanayolazimisha ukusanyaji kwa njia ya Tozo

Matumizi ya serikali na taasisi zake ni makubwa sana. Mbunge anajua kituo chake cha kazi ni Dodoma, ana nyumba lakini bado analipwa pesa nyingi kila akikaa Bungeni mbali ya mshahara mnono.

Ukitaka kujua kuna tatizo, piga hesababu za Taasisi ya Bunge kwa siku moja tu halafu zidisha mara vikao
Kwanini mkoa mmoja una RC mmoja, mkoa huo huo una Wabunge 7 etc?

Kama tunahitaji kodi kwanini hatupunguzi vikao vya 'Bunge' kwa siku 20 tu kwa mwaka! piga hesababu

Kwanini maafisa wanunuliwe V8 ? Kwanini wasipewe pesa za nauli na kuwe na gari chache za Idara na Wizara?
Kwanini karani ajilipie nauli ya kazini halafu alipe TOZO ya kununua V8?

Hoja si kodi au TOZO , hoja ni matumizi mabaya ya fedha yanayolazimisha serikali kutoza tu bila kuangalia namna ya kukusanya kutoka vyanzo vingine. Mfano, tuna madini ya HELIUM kule katavi yanayotafutwa duniani, nani anafikiria ni chanzo kizuri cha mapato?

Kama serikali imeishiwa mbinu, kwanini wasiache wengine wenye mawazo tofauti kama Zambia au Kenya waje na mbinu mpya! Hatuwezi kuishi kwa kukinga Bakuli ughaibuni na kuminya wauza mchicha miaka 60 ya Uhuru

JokaKuu Pascal Mayalla Tindo
Umedadavua vizuri sana.

Kwa kuongezea, tusijilinganishe na nchi zilizoendelea kwa historia tofauti kama US na Sweden. Tujilinganishe na wenzetu wenye uchumi wa kiwango kama sisi au ambao hivi karibuni wameweza kupiga hatua kutoka hali inayofanana na sisi na kuweza kuendelea zaidi mfano zile nchi zinazoitwa Tiger economies - Singapore, Taiwan, nk.

Je, hizi tiger economies ziliweza kuendelea kwa misingi ya kujikita kwenye kukamua na kukusanya kodi kwa wanachi wake?
 
Mzee kama haufanyi biashara huwezi kunielewa ila ipo hivi kwa mfumo wa kodi wa Tanzania ili uweze kubaki na faida + mtaji ni lazima ukwepe kodi ndo utasurvive sababu mazingira ya kufanya biashara ni magumu sana ofisi zinazochukua kodi + tozo zipo zaidi ya 4 na kila moja ina nguvu usipp weka mambo sawa unajiandaa kukwamishwa...haswa kwa wale tunaofanya biashara ambazo zimekua regulated na taasisi zingine...kikwako kikubwa ni serikali na mfumo mzima wa kodi..sio rafiki kwa ustawi au ukuaji wa baishara na mitaji...ila kama wewe ni mvaa tai huwezi nielewa...
Sio Kweli.
 
Tanzania ni nchi ya ajabu VIONGOZI WANAPENDA maendeleo Ila hawataki kupunguza gharama za kila siku katika uendeshaji wa Serikali.
 
Kiufupi ,wanywaji wanywaji wa vileo wantakiwa kupewa tuzo ya ulipaji Kodi bila manunguniko.

Kwa miaka mingi serikali imekua ikiongeza Kodi kwenye vinywaji ,na gharama hizo hubebwa na wanywaji. Cha ajabu hayajawahi kutokea malalamiko kama haya ya Tozo.
 
Hata hiyo kodi kwenye uagizaji magari tulipaswa kuipinga kwa nguvu zote ila basi tu.

Kodi ni sawa au kubwa kuliko bei ya bidhaa yenyewe ushaona wapi?

Siku watu wakiridhika na matumizi ya kodi zao hakuna atayelalamika.

Waziri asiyekuwa na wizara??
 
Cleopa Msuya, alipokuwa Waziri wa Fedha, alisema , kila mtu ataubeba msalaba wake mwenyewe.
Wakamchukia.
ukiacha cha Arusha utakua kijana safi. Haiwezekani kabla ya kunipa mshahara unaukata kodi. Kinachobaki unaniwekea bank halafu unavizia ukate tena kodi ninapoichukua hiyo hela toka bank
 
Waziri Mkuu wa Uingereza, Margaret Thatcher aliwahi kusema, serikali haina duka wala biashara au shamba. Serikali inaendeshwa kwa kodi zinazotozwa kwa wananchi wake.

Wananchi hawakupenda sana kauli hiyo, lakini akawaambia hivyo ndiyo ilivyo kwenye free market economy.

Hivyo ndivyo ilivyo duniani pote. Serikali haifanyi biashara wala kuwekeza.

Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao. Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi.

Sasa hapa kwetu Mwalimu alijaribu kuitumia serikali kuwekeza katika mashirika mengi ya Umma. Mashirika haya karibu yoote yalikufa, pamoja na uwekezaji mkubwa wa serikali.

Mwinyi alipoingia, aliingiza sera za kulegeza sharti ya biashara na kuiondoa serikali kwenye biashara.
Mkapa alijiongeza kwa kutengeza taratibu za ukusanyaji kodi na usimamizi mzuri kiserikali katika miradi yake(mfano TANROADS).

Tatizo kubwa ka wananchi walio wengi wa Tanzania ni kufikiri kuwa serikali ndio ikope kwa mjomba fulani huko nje ili wananchi wapate kazi, wapate fedha na waishi maisha mazuri.

Watu hawajifikirii kuanzisha miradi, biashara uwekezaji na kutafuta mitaji kwa ajili hiyo.

Mbaya zaidi watu wanafikiri hela yao ni yao, isiguswe na mtu yeyote lakini waendelee kupata huduma za bure toka serikalini.

Hili suala la TOZO ni la kulitazama kwa jicho la tatu.

majibu ya mada yako utayapa humu kwanini watanzania hawataki kutoa hao matozo... nchi hii ni ngumu sana.
 
Kodi haileti maendeleo. Kodi ni kwaajili ya posho za watawala na kugharamia maisha yao ya anasa.
 

majibu ya mada yako utayapa humu kwanini watanzania hawataki kutoa hao matozo... nchi hii ni ngumu sana.
Watu hawataki kuwekeza hata kwenye frame ya duka, lakini wanataka elimu bure, matibabu bure, na barabara za lami wanataka hadi mlangoni.
Lakini kulipa kodi inakuwa shughuli pevu, na wabunge wenyewe wanaongoza kwa kutolipa kodi.
 
ukiacha cha Arusha utakua kijana safi. Haiwezekani kabla ya kunipa mshahara unaukata kodi. Kinachobaki unaniwekea bank halafu unavizia ukate tena kodi ninapoichukua hiyo hela toka bank
Kwa kulinganisha tu, Magfuli aliitumia TRA kubeba fedha za wafanyabiashara toka kwnye mabenki kwa nguvu, mkashangilia.
Sasa litaka ninyi ndo msiguswe?
 
Mjeledi ni muhimu sana ili tusonge mbele.
tukibembelezana hatuwezi kupiga hatua ya maendeleo.
Malengo ya wapingaji ni kuchelewesha dhamira njema ya Serikali kutuletea maendeleo.......
naishauri Serikali isihangaike na kelele za wachawi.
 
…Serikali makini duniani kote zinatengeneza mazinira ya uwekezaji kwa WANANCHI WAKE ili waweze kupata kodi kutokana na biashara zao. Huo lazima uwe msingi wa nmna ya kupata kodi...

Lawama zako kwa wananchi zinakinzana na ulichokisema kwenye hiyo paragraph. Serikali imeshindwa kutengeneza hayo mazingira, lakini wewe unataka wananchi waunge mkono hizo tozo bila kujali kama wana vyanzo vya pesa ya kulipa hizo tozo au la.
 
Back
Top Bottom