Watanzania wengi ni watu wasiokuwa na ustaarabu katika kuongea

Duh.
Kichuguu, hakuna cha stress wala cha kuwa na maisha au kuwa na elimu ndogo!

Wewe unaona sababu ni nini?

Kwa maoni yangu, naamini kabisa kuwa chanzo cha tatizo ni Lugha.

Najua wengi wanaotupa na kurusha matusi hapa JF ni wageni, ni wakuja hao.

Matusi yanatoka kwa wageni ambao sio wazungumzaji na wala hawajazaliwa hapa na kujua Lugha ya kiswahili, kutokana na kwamba wamezaliwa na kulelewa katika nchi za kigeni ambako walijifunza lugha na tamaduni tofauti na za kwetu.

Kwanini wanalazimisha lugha zao na utamaduni wa lugha za kigeni ziwe lugha zetu huku wakipuuza tamaduni na maadili yetu yanayounda Lugha yetu?

Tafakari tu. Ukiweza jibu, jibu.



Nina mifano na ni mingi hata kutoka hapa Jamvini.


Mijamaa inatusokomezea lugha na tamaduni zao za kigeni bila ya kushesimu mila na maadili yetu ambayo ndio yanayounda Lugha ya kuzungumza na lugha ya Mawasiliano.

Sikubaliani kwamba "Ukiongea na Mtanzania na mkashindwa kukubaliana huwa anakurushia matusi ya nguoni" si sahihi na yanaegemea kumdhihaki Mtanzania zaidi.

Nadhani suala, ni ukosefu wa heshima na kutothamini utofauti na mapana wa lugha na tamaduni.
 
tunajikuta black america eti na ujanja!
 
Ustaarabu ni zero, how you do anything is how you do everything, katika nyanja zote sisi ustaarabu ni zero...nilikutana na mtu kwenye basi, Wala hatujuani Sasa katika maongezi yetu ya kawaida nikagundua huyu siyo wa kuendelea kuongea naye tu ikabidi ninyamaze na hili nadhani alilijua akawa Sasa anapiga stori na mtu wa jirani, Yani bila kumkubalia anachosema tayari basi maneno mabovu yanamtoka, kukubali kila kitu napo binafsi siwezi kabisa.
 
Tatizo ni hiki chama chakavu mkuu...😜
 
Humu jf wakikosa hoja za kujibu katika ushindani wataanza kukagua sentensi kama ulisahau nukta basi watatukana. Hiki kizazi cha kujisifia uchawa shida sana.
 
"If you look at their mode of life and their lifestyle in general, you can observe that blacks are born with the situation like an half-mad mentality and mindsets."
Jan Smuts, a former first Prime Minister of Union of South Africa.
 
Huku ni kuongea katika maandishi. Kwani kuongea ni lazima matamshi pekee? Nafikiri ujifunze aina za lugha mkuu.
Sikijua mkuu,kumbe unaweza kuongea katika maandishi?mi nadhanj kuongea katika maandishi ni nukuu tu
 
Njaa huleta hasira kali na hasira kali ni kama uharo usipokimbilia maliwatoni unakuchafua.
 
Mjinga sio tusi Bali mtu asiyefahamu kitu flani na mpumbavu ni mjinga pro max
 
ustaarabu sio taifa bali ni mtu mwenyewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…