Uchaguzi 2020 Watanzania wengi sasa wanamiliki smartphone ili kupashana habari za uchaguzi hasa zinazohusu wapinzani

Uchaguzi 2020 Watanzania wengi sasa wanamiliki smartphone ili kupashana habari za uchaguzi hasa zinazohusu wapinzani

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Kwa wake wanaodhani kuwa kudhibiti vyombo vya habari kuripoti habari za wapinzani kutawasaidia, wajue tu wanajidanganya kwani hivi sasa watanzania wengi wanamiliki smartphone hasa maeneo ya mijini, hivyo watazitumia kupashana habari za uchaguzi zikiwemo habari za wapinzani.

Lissu kasema wametishwa kuripoti habari zake na kwamba wanamuogopa mtu mmoja ila akaongeza kuwa ,watu sasa watutimia WhatsApp kupashana habari za uchaguzi.

Ukweli ni kwamba,Lissu kataja WhatsApp kama mfano tu, ila watu watatumia Facebook,Instagram, Twitter na mitandao mingine kama huu wa JamiiForums kusambaza na kupashana habari za nini kitakachokuwa kinajiri kwenye mkutano ya kampeni ya wapinzani hata kama watu wa TV na magazeti hawataripoti.

Uzuri wa haya mambo ni kuwa,watu wakipuuza hizi media,hata like kitakachokuwa kinaripotiwa na hizi media pia nacho kitapuuzwa, hivyo wataopata hasara ni hao watakaokuwa wanategeme hizi media ziwabebe.

Wao waendelee tu kujidanganya wakati watu Siku hizi wameanza kutegemea social media zaidi kama chanzo cha kupata habari huku mainstream media zikibaki kutumika kwakuwa tu ziko majumbani mwetu.

Siku hizi watu wanasikiliza habari kwenye tv huku teyari wana taarifa za matukio karibu yote ya siku husika tena taarifa hizo wakizipata pasipo kuchujwa ili kumsitiri mtu au kuficha baadhi ya mambo.

Mfano mzuri ni ujio wa Lissu ambao ulitangazwa zaidi kupitia social media lakini karibu kila mtu alikuwa na taarifa na alipokelewa na watu wengi utadhani tukio husika liliitangazwa na vyombo vikubwa vya habari mwezi mmoja kabla.

Labda yule Malaika wa kuzima mitandao ashuke ndio itakuwa ponepone yao ingawa nae anaonekana kukwama huko mawinguni.

Imekula kwao mwaka huu.
 
Mimi siku nyingi siangalii tena tv za Tz wala kusikiliza radio. Simu yangu ni kila kitu.. Gb moja kwa siku powa kabisa.. Labda na simu zizuiliwe kurusha habari
Mimi mwenyewe sku hizi sina habari na magazeti wala tv za humu ndani kabisa.
 
Ni kweli ila Kuna watu hawana smat Wala tv,ila mamuzi yao yapo kwenye sanduku ,huwa awangalii mtu ila rangi ya chama.
 
Hata wasiporusha habari za Lissu tunazipata instantly na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii na pia huku mtaani tunawapa elimu wasio na access na internet/mitandao.
 
Serikali ya CCM HAIJAFANYA KITU. Sasa hao wananchi hizo smartphones, WhatsApp na Twitter wanazitoa wapi hapa Tanzania?
Una mtzamo duni sana.Elewa tu,hali ingekuwa nzuri,hata huko vijijini karibu kila mtu angekuwa anamiliki smartphone akiwa na uhakika wa kuwa na umeme wa kuichaji.
 
Hata hiyo mitandao akiamua tu anaizima au unafikiri hilo liko nje ya uwezo wake?

Kiuhalisia mamlaka ikiamua kufanya figisi,hamna ujanja wowote.
 
Hata hiyo mitandao akiamua tu anaizima au unafikiri hilo liko nje ya uwezo wake?

Kiuhalisia mamlaka ikiamua kufanya figisi,hamna ujanja wowote.
Akizima nani mwenye akili atamuelewa na kumpigia kura?
 
Tunaishukuru sana serikali ya ccm hasa hasa awamu ya tatu ya Daktari Jakaya Mrisho Kikwete baba wa Demokrasia , uwazi na maendeleo ya kasi nchini Tanzania kwa kuweka misingi ya wananchi kuwa na uwezo wa kumiliki simu janja kwa unafuu.


Ubarikiwe sana mzee mtoto wa Khalfani , ndugu Daktari Jakaya Mrisho Kikwete mwana wa ukaya.

Kupitia serikali ya Kikwete watanzania wengi walitimiza ndoto zao ambazo nyingi zimevurugwa kwa sasa.
 
Mimi siku nyingi siangalii tena tv za Tz wala kusikiliza radio. Simu yangu ni kila kitu.. Gb moja kwa siku powa kabisa.. Labda na simu zizuiliwe kurusha habari
Tutaanzisha mamlaka rasmi ya kudhibiti Matumizi ya simu.
 
Watu smartphone ni kwa kuombea connection ya video za x za celebrities wa bongo.
 
Back
Top Bottom