Watanzania wenye vipato vya chini wanao somesha English Mediums wanateseka hadi nawaonea huruma

Watanzania wenye vipato vya chini wanao somesha English Mediums wanateseka hadi nawaonea huruma

Mkuu me naona wa medium akiwa kichwa na wa kayumba akawa kichwa, utakuta wa kayumba anamzidi social skills
kama kujiamini,kuongea na watu,kukabili changamoto n.k wa medium mara nyingi anakuwa na academic skills tu, hana social skills. Hivyo anapotea maana anajikuta mjuaji, lakini pia ana uoga uoga kama ndezi na chuo ukipeleka undezi/ujuaji hutoboi
English medium social skills wanazo ila kwa watu wa class yao

Watu wao wa karibu wa kucheza nao ku socialize ni watoto wa wabunge mawaziri,wafanyabiashara wakubwa nk hupeana happy birthdays nk

Huwezi waona wana socialize na maskini ndio maana huwaoni huko mitaani wakicheza rede kama watoto wa uswahilini na hata kuoa au kuolewa wanaenda na class yao sio ya uswahilini

English medium ni njia mojawapo ya kupandisha class ya mtoto.aondokane na uswahiliswahili wa mitaani
 
Nashukuru Mungu nilijitoa kwenye utumwa wa kujitakia na Sasa naishi kwa Amani kabisa watoto niliwatoa EM nimewaleta Kayumba sina Tena stress na mambo yanaenda vizuri na watoto wanafanya vizuri darasani. Twisheni ya nguvu. Aliyekuwa la 4 mwaka jana kapata A zote Masha'Allah.

Shoga zangu tuliokuwa tunasomesha wote EM karibu wote wamewarudisha Kayumba wanao wamebaki wachache ambao eti wanaogopa kuchekwa wataonekana wameshindwa maisha ila mateso Yao Sio ya dunia hii, mikopo kama yote, wananuka madeni na ndani hawana asset, hawana viwanja watoto wanalala chini ilimradi wasome EM..

Sasa najiuliza mateso yote hayo ya Nini wakati hata Kayumba wanaweza soma vizuri tu na Chuo wakafika kama.wanavyo fika wengine.

Poleni Sana watanzania wenzangu ambao bado mpo kwenye utumwa huo. Mungu awaongoze Sana mshituke mapema.

Sisemi kusomesha mtoto EM ni Vibaya ila Uwe na uwezo mkubwa Sana WA kifedha na assets za kutosha.
Km.wtt walishapata msingi skuli za EM ukiwapeleka Kayumba wanatusua tu kama kawaida.
Mie pia nna mpango huo. Nasubiri wajivute walau mpk la 7 Insha'Allah
Hii idea nnayo zamani tu
 
English medium social skills wanazo ila kwa watu wa class yao

Watu wao wa karibu wa kucheza nao ku socialize ni watoto wa wabunge mawaziri,wafanyabiashara wakubwa nk hupeana happy birthdays nk

Huwezi waona wana socialize na maskini ndio maana huwaoni huko mitaani wakicheza rede kama watoto wa uswahilini na hata kuoa au kuolewa wanaenda na class yao sio ya uswahilini

English medium ni njia mojawapo ya kupandisha class ya mtoto.aondokane na uswahiliswahili wa mitaani
Ni kweli sometimes kuna haja ya kujitoa mhanga kuvunja ile vicious cycle of poverty ya kuzunguka na watu masikini kua na marafiki masikini kuoa watoto wa masikini kuzaa watoto masikini kua na wajukuu masikini, kwasababu matajiri una mahara pakuwakuta na ku-socialise nao isipo kua kuenda kwenye shule za private English medium
 
Mzazi akishakosa pesa za kulipa ada EM ataanza kujifariji kuwa kidumu na ufagio ni kuzuri sana na ndio maana mtu kama alikuwa masikini kiasi gani akishapata pesa za kutosha utamkuta anaanza ku-google kuhusu madhara ya kula ugali, dagaa kauzu na tembele
 
Wakati flani nimiwa mwalimu nilienda kusimamia mitihani shule ya binafsi. Ulikuwa mtihani wa kidato cha pili. Watoto kama 78 hivi katika hiyo shule binafsi. Matokeo yao yalikuwa division one wote. Wkt huo nafundusha serikalini na kidato hichohicho watoto 260 kulikuwa na division one 8, two 15, three 30, four 45 waliobaki zero.

Mytake. Uandishi wa essay(maelezo) ya hoja wale watoto 78 walikuwa smart mno. Mtoto anamwaga lugha ya malkin kurasa 2 hadi 3.

Kule kwangu wale watoto wenye division one waliotokea EM wanamwaga lugha vema, sasa njoo hawa wa kuanzia division 3 huku kwetu, yaan mtoto kuuganisha sentence hawezi. Page moja haifiki hata katikati na wanaishia kukopi maswali na majibu ya uongo kujazia essays.

Anaempleka mwanae EM anampa mtaji mwanae..wengine endeleeni kukejeli.
Watoto wenu ndio wale mkiondoka duniani, hawana foundation. Walimu 50 wa serikalini utakuta anayefanya kwa moyo mmoja ni 5. Hawa ndio husaidia sana.

Private walimu 50 makanjanja utakuta 3 hadi 5 hawa ni ndg na jamaa wa Mkurugenzi wa shule.

Fuja pesa nunua magari na kunywa bia ili mwanao akasome kwa kumsubiri Mama samia acheke.

Walimu asilimia 98 wale senior wanamajumba yao, wanaishi vzr na watoto wao wanawapeleka EM kwa kawaida wakistaafu hawana ufahari. Mungu awabariki walimu wote wa EM na Government mimi mawaita maafisa elimu
 
Sasa najiuliza mateso yote hayo ya Nini wakati hata Kayumba wanaweza soma vizuri tu na Chuo wakafika kama.wanavyo fika wengine.
 
Wahindi wanaishi nyumba za kupanga za National Housing na wanasomesha watoto shule za bei mbaya

Mtu kuwa anapanga nyumba haina maana kuwa ni maskini
Usijifananishe na wahindi. Wenzako wengi wao nyumba za babu Zao zilitaifishwa wakati wa Nyerere. Alafu kingine wengi wao hapa ni Foreigners ulitegemea wajenge?

Kibongo bongo usipokuwa na nyumba ni kiashiria bado unajitafuta

Mkuu me naona wa medium akiwa kichwa na wa kayumba akawa kichwa, utakuta wa kayumba anamzidi social skills
kama kujiamini,kuongea na watu,kukabili changamoto n.k wa medium mara nyingi anakuwa na academic skills tu, hana social skills. Hivyo anapotea maana anajikuta mjuaji, lakini pia ana uoga uoga kama ndezi na chuo ukipeleka undezi/ujuaji hutoboi

Kweli Kabisa
 
Pesa ina nguvu, labda hao ambao wanao struggle kulipia ada watoto wao kitu ambacho pia ni kawaida katika maisha. Wewee ambae unasifia kayumba ndio nguvu ya pesa yako imeishia hapo na haimanishi kuwa hizo kayumba ni bora kuliko EM. Ajabu ninaloliona hapa ni kutaka kuufanya uwezo wako mdogo wa kipato kufanya shule hizo za K kuonekana ni bora. Siku uwezo wako wa kipesa ukibadirika utawaza tofauti. Kama watoto wenu wako vizuri katika shule za K basi elewa kuwa Kama wangekuwa EM basi wangekuwa vizuri zaidi kuliko walivyo sasa.

Uzi ufungwe!
 
Unajua mtoto anauma eeeee. Just imagine katoto kako kananyanyasika mtaani hadi kanakonda kakiona vigari vya njano vinawabeba wenzake waende shule.. hata kama wewe una ka Vitz kako unampeleka hapo kayumba, lakini yeye bado atatamani school bus... mbaya zaidi vitoto vya hizo miedium vinacheza kwa kiinglish muda woteee.. ... katoto kako kanakodoa macho tu... hakana raha mtaani, hakana raha nyumbani, kanatamani kangezaliwa kwa jirani. Hapo ndipo utakuta Mzazi anaamua kujitosa... kama mbwai na iwe mbwai wote watasoma huko huko kwenye kingereza cha kucheza na wenzao. Labda muishauri serikali ya government yenu ibadilishe mitaala, iweke na skulibasi. KUNA WALIONIELEWA
Hoja ya kitoto kabisa kwahiyo mtoto kila anachotamani unampa😁😁😁nyie ndo mnatengeneza watoto wasio na uwezo mzuri wa kufikiri na wenye kufake maisha maana hata wazazi walifake maisha.


Muandae mtoto aweze kujitambua mapema acheni porojo na hoja mufilisi kama hizi.
 
Kila mtu afanye anavyoona inafaa kwa ajili ya vizazi vyake. Kama wazee wetu walilima na kujinyima kwa ajili ya elimu zetu, walioimq kahawa, mahindi na ndizi ili tukasome. Kwa nini sisi tuone kusomesha watoto ni utumwa.

Kweli shule za serikali ni dhaifu sana, kama unawapenda watoto wako na unajibidisha kufanya kazi hutaruhusu wakasome huko.
Very true. Ku-struggle kwenye maisha ni jambo la kawaida na si dhambi. Hata hizo shule tulizosoma zamani wazee walijinyima sana na ku-struggle sana. Sasa uache kumpeleka mtoto shule nzuri kisa ada inasumbua? Labda kama mtu huna kipato kwa sababu mbalimbali za kimaisha kama kupoteza kazi. Kwanza mbali na kujua kiingereza pia upeo wa watoto wa private na government schools ni tofauti kabisa
 
English medium social skills wanazo ila kwa watu wa class yao

Watu wao wa karibu wa kucheza nao ku socialize ni watoto wa wabunge mawaziri,wafanyabiashara wakubwa nk hupeana happy birthdays nk

Huwezi waona wana socialize na maskini ndio maana huwaoni huko mitaani wakicheza rede kama watoto wa uswahilini na hata kuoa au kuolewa wanaenda na class yao sio ya uswahilini

English medium ni njia mojawapo ya kupandisha class ya mtoto.aondokane na uswahiliswahili wa mitaani
Fainali wakishamliza chuo hiyo class yao unayoongelea ya kufake hapo baada ya kumaliza chuo ndo huwa inaonekana vizuri wale wa BOLT na UBER wanaanza kupanda bodaboda na dalalada😁😁😁😁😀😀😀


Huku mtaani mambo ni tofauti kabisa wale waliokuwa wanajitengatenga baada ya kumaliza chuo huwa wqnakuwa kama kuku walionyeshewa😀😀😀maisha ni hatua hutakiwi kufake utadhindwa kuishi na watu.
 
Siku hizi kuna kama kaugonjwa fulani kwa wazazi wa kileo,utasikia mzazi akisema mi mwanangu awezi kuteseka kama mimi,kamwe sitampeleka kayumba!,,mara sitaki atembee umbali fulani,,ooh nitafanya kila namna asiende kayumba nk nk,, watoto wanalelewa kimayai sana na wazazi wa sampli hii,ndo hao wanaingia gharama kubwa wasizoweza kuzimudu.
 
Usijifananishe na wahindi. Wenzako wengi wao nyumba za babu Zao zilitaifishwa wakati wa Nyerere. Alafu kingine wengi wao hapa ni Foreigners ulitegemea wajenge?

Kibongo bongo usipokuwa na nyumba ni kiashiria bado unajitafuta



Kweli Kabisa
Mtibeli ukiwekeza hela sehemu sahihi hizo nyumba za national housing (NHC) mtu yoyote anakaa.

Ujenzi wa nyumba huwa ni garama sana ukitaka kuamini hii. Tafuta mtu anayejenga muulize ametumia shingapi😀😀😀wengi watajificha kwenye kivuli ooohh mimi sipigi hesabu mara oohhh ukipiga utashindwa kujenga.Ila kiukweli kabisa a standard house kiwanja kilichopimwa na barabara inayopitika mitaa imepangiliwa yaani kwa makadirio ya chini sio chini ya milioni 80 unaizika hapo. Sasa hii mishahara ya sereikali 700k mpaka 2million kuna wa kujenga hivi.Akijitahidi sana hapo atakopa na nyumba itaishia kwenye plaster.Wengi wanajenga kwenye viwanja vya 20×20 nyumba imebanana hata sehemu ya kupita kuzunguka nyumba hamna.

Wewe saivi ukiwekeza hela kwenye mashamba ya miti,mashamba ya matunda na viwanja vya low density vilivyopimwa.Ukijikita na kuwekeza kwenye bonds na hisa. Huna haja ya kujenga maisha yako yote utaishi kwenye appartment maana wewe umefanya uwekezaji sahihi unaozalisha pesa kila leo na kupanda thamani ni tofauti na ungezika hizo hela, hiyo hiyo millioni 80 kwa kujenga nyumba.Ujenzi sio uwekezaji ni upotevu wa nguvu na rasilimali.

Serikali ingeruhusu tu baadhi ya kampuni kubwa zenye mitaji ndo zijenge ili kuwe na standard ya nyumba za kuishi na kuondoa tatizo la makazi holela na viwanja ambavyo havijapimwa.Mtu akitaka nyumba ananunua au akope alipe kidogokidogo mpaka amalize mkopo.
 
Kwani anasoma EM maisha yote? Si miaka 7 tu?!, wacha tupambane kujenga msingi imara wa nyumba ya kisasa.
Sekondari tutawarudisha huku kayumba.
Primary wacha tuumizane huku EM maana mtoto akiwa mdogo ndio muda muafaka wa kumjenga kimtazamo tofauti
Mkuu hata sekondari usijaribu kuwapeleta hizi government school, mtoto mpeleke shule nzuri aelewe maisha ni furaha
 
Back
Top Bottom