Wateja wa Mabenki chukueni tahadhari kubwa, kuna wizi kwenye tozo na commission zao

Wateja wa Mabenki chukueni tahadhari kubwa, kuna wizi kwenye tozo na commission zao

Nadhani shida sio maBank shida ni watawala wetu wanaotaka kuvuna wasipopanda ..wee humsikii yule Waziri anaefanyaga kazi ya uafisa habari wa mitandao ya simu?....tungekuwa na watawala wanaojali watu wao wasingekuwa wanaweka makodi ya hovyo hovyo

Sent from my CPH2179 using JamiiForums mobile app
Hizi pesa ndizo baadae ccm huchukua kiasi fulani kuendeshea mambo yao hasa chaguzi.
 
Kwa kweli haya mabenki bila kuyafikisha mahakamani, yataendelea na huu wizi. Wanatamba wametengeneza faida kumbe ni kwa kuwaibia wateja.

Fikiria muamala mmoja wanaiba kama sh 2,000 hivi. Mwezi mmoja ukitoa pesa yako kupitia ATM 10m, ina maana watakuwa wamekuibia = 10,000,000÷400,000 = 25×2,000=50,000. Wakifanya hivyo kwa wateja 10,000; watakuwa wamefanikiwa kuiba = 50,000×10,000 = 500,000,000 kwa mwezi. Kwa mwaka, watatengeneza bilioni 6.

Kuna benki nyingine, siitaji jina kwa sababu waliomba sana msamaha. Wao kwenye miamala miwili ya jumla ya shilingi laki 8, nilitoa kwenye ATM kutoka kwenye account yangu ya dola, walinikata tozo dola 2,700. Yaani nilitoa laki 8, halafu tozo ikawa zaidi ya shilingi milioni 6. Yaani system yao ikawa inazikata dola kama shilingi. Baada ya kulalamika, walirudisha baada ya siku 5.
Huu wizi unaofanyika sana, na vile watu wengi hatuko makini basi hilo linafanyika kirahisi sana. Usishangae ukakuta serikali inajua jambo hili, na si ajabu ni wafaidika wa huu uhuni.
 
Baada ya tozo za madelu kuanza nilikuta CRDB wamelamba laki na kumi na tano kwenye akaunti yangu, nilivyofuatilia kwenye statement ndo nikakutana na hayo makato lukuki ambayo mengine hayaeleweki wanakata nini na yanaweza kujirudia mfululizo kabla hujatoa pesa nyingine.

Walinimbia niandike barua kwa meneja kulalamika, lakini niliona hawafuatilii chochote zaidi ya kunipotezea muda. Baada ya hapo siamini kabisa pesa zangu kukaa benki, kiasi kwamba hata ukinilipa milioni tano sasa hivi benki naweza kuvunja miguu kwenda kuichomoa.

Huu utaratibu wa madelu kuvuna pesa za watu kwenye mabenki na kwenye miamala ya simu ni utaratibu uliopitwa na wakati sawasawa na kipindi cha kodi ya kichwa ambayo Mkapa aliiondoa, eti mchumi first class....​
 
CRDB wanalalamikiwa sana kila Kona.

Kama wapo humu wasikie hili,hata Mimi haya maeneo niliyopo CRDB kila mtu anasema ni Wezi Wezi.Ushauri wangu kwao wafuate miongozo ya kazi na makato halisi kama yanavyojieleza.Watu watawakimbia kwa style hii.
 
Back
Top Bottom