Watoto hawaimbi nyimbo za Sunday school na Kaswida tena, mdau alalama akitoa maoni dira ya taifa 2050

Watoto hawaimbi nyimbo za Sunday school na Kaswida tena, mdau alalama akitoa maoni dira ya taifa 2050

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Mchakato wa kukusanyika maoni ya dira ya taifa ya maendeleo 2050 ukiendelea umekutana na maoni ya mmoja wa raia akilalamika maadili ya Mtanzania yakizidi kupotea hasa kwa watoto, raia huyu amelalama watoto kuacha kuimba nyimbo za Sunday school na kaswida badala yake wanaimba "vibuno", "honey" "siendi siendi".
Tumsikilize hapa,
 
Sijaelewa kwa nini serikali inapoteza rasilimali fedha na muda kumuuliza kila mtu anataka nini kuelekea 2050. Ninachofahamu kazi kama hizi huwa wanachukuliwa wataalamu mbalimbali kutoka vyuo kadhaa na taasisi chache muhimu kisha wanamaliza kazi yote ndani hata ya mwezi mmoja tu na wanatoka na document moja ya mpango iliyonyooka.
 
Hilo ni jukumu la mzazi sio kazi ya serikali. Hawa wabongo ifike mahali wajue majukumu yao. Tunataka serikali ifanye majukumu yake ila sio kuingilia kila kitu.
 
Mchakato wa kukusanyika maoni ya dira ya taifa ya maendeleo 2050 ukiendelea umekutana na maoni ya mmoja wa raia akilalamika maadili ya Mtanzania yakizidi kupotea hasa kwa watoto, raia huyu amelalama watoto kuacha kuimba nyimbo za Sunday school na kaswida badala yake wanaimba "vibuno", "honey" "siendi siendi".
Tumsikilize hapa,
View attachment 3060907
Jana nimepishana na coaster imebeba wanafunzi wa primary nadhani ni shule ya government wanaimba kwa sauti kale ka wimbo ka honey ka zuchu
 
Sijaelewa kwa nini serikali inapoteza rasilimali fedha na muda kumuuliza kila mtu anataka nini kuelekea 2050. Ninachofahamu kazi kama hizi huwa wanachukuliwa wataalamu mbalimbali kutoka vyuo kadhaa na taasisi chache muhimu kisha wanamaliza kazi yote ndani hata ya mwezi mmoja tu na wanatoka na document moja ya mpango iliyonyooka.
Watu wanaangalia angle moja tu ya ulaji. Kiuhalisia wanachokifanya ni upotevu wa rasilimali muda na pesa, mwisho wa siku hakuna watakachofanya cha maana na hayo maoni.
 
Sijaelewa kwa nini serikali inapoteza rasilimali fedha na muda kumuuliza kila mtu anataka nini kuelekea 2050. Ninachofahamu kazi kama hizi huwa wanachukuliwa wataalamu mbalimbali kutoka vyuo kadhaa na taasisi chache muhimu kisha wanamaliza kazi yote ndani hata ya mwezi mmoja tu na wanatoka na document moja ya mpango iliyonyooka.
Serikali iko sahihi, wewe ndiye huielewi kabisa dhana ya ushirikishwaji. Hata uchukue maprofesa kutoka Havard University ni lazima wakusanye maoni ya wananchi ili baadae wayachambue na kutaweka kitaalamu. Kama serikali ingetaka kufanya kama usemavyo basi hata kusingekuwa na sababu ya kuwa na uwakilishi au kuchukua maoni kwenye miswaada na tume mbalimbali. Mawazo kama yako ndiyo hupelekea miswaada wakati mwingine kuwekewa muda mfupi sana wa kupokea maoni ya wananchi, kwa sababu inawezekana hata bungeni wameshawajua kwamba hamna time na mambo hayo, kiasi kwamba hata mngepewa Mwezi mzima hakuna mwenye time, watu wako bize na mipira, betting, Diamondi vs Kiba etc. Matokeo yake sheria ikipita na pengine kodi imepandishwa ndiyo watu wanashtuka na kulalamika. Tabia hii ya jamii kukwepa uwajibikaji kwenye masuala muhimu ya maendeleo ya nchi, na kuamini kwamba ni kazi ya serikali na wao haiwahusu ndiyo chanzo kikubwa cha kukosa maendeleo,hasa pale tunapokuwa na viongozi wasiokuwa wawajibikaji.
 
Serikali iko sahihi, wewe ndiye huielewi kabisa dhana ya ushirikishwaji. Hata uchukue maprofesa kutoka Havard University ni lazima wakusanye maoni ya wananchi ili baadae wayachambue na kutaweka kitaalamu. Kama serikali ingetaka kufanya kama usemavyo basi hata kusingekuwa na sababu ya kuwa na uwakilishi au kuchukua maoni kwenye miswaada na tume mbalimbali. Mawazo kama yako ndiyo hupelekea miswaada wakati mwingine kuwekewa muda mfupi sana wa kupokea maoni ya wananchi, kwa sababu inawezekana hata bungeni wameshawajua kwamba hamna time na mambo hayo, kiasi kwamba hata mngepewa Mwezi mzima hakuna mwenye time, watu wako bize na mipira, betting, Diamondi vs Kiba etc. Matokeo yake sheria ikipita na pengine kodi imepandishwa ndiyo watu wanashtuka na kulalamika. Tabia hii ya jamii kukwepa uwajibikaji kwenye masuala muhimu ya maendeleo ya nchi, na kuamini kwamba ni kazi ya serikali na wao haiwahusu ndiyo chanzo kikubwa cha kukosa maendeleo,hasa pale tunapokuwa na viongozi wasiokuwa wawajibikaji.
Singapore, Malaysia, Korea Kusini na China kama wangefuata huu mtindo wa kumuuliza kila mtu anataka nini kwenye mipango ya nchi leo hii bado wangeendela kuwa vijiji vya wakulima peasants na wavuvi wa mitumbwi tu.

Ili nchi iendelee kwa kasi lazima kuwe na wataalamu(technocrats) wazalendo wachache wanaopanga mambo ya kitaifa na viongozi wazalendo na waadilifu watekelezaji.
 
Tanzania viongozi wanakuaga na mawazo mazuri tatizo linakuja katika utekelezaji, wazo la dira ya taifa 2050 ni zuri ila namna ya kutekeleza sasa
 
Singapore, Malaysia, Korea Kusini na China kama wangefuata huu mtindo wa kumuuliza kila mtu anataka nini kwenye mipango ya nchi leo hii bado wangeendela kuwa vijiji vya wakulima peasants na wavuvi wa mitumbwi tu.
You missed my point, read between the lines. Maoni ya wananchi huchukuliwa kwa uwakilishi au sample. Tanzania ina watu 60 million, hivi unaweza kuwahoji wote?? Really?? Ndiyo maana hiyo mikutano ya kukusanya maoni kuhusu dira ya nchi huwezi kuiona ikiitishwa kila nyumba 10. Hata miswaada ya bunge wakikusanya maini wanafuata uwakilishi kwa makundi ya jamii kufika kutoa maoni au kutuma maoni yao. Mwisho mimi huwezi kunishawishi kwamba udikteta ndiyo huleta maendeleo kama hizo nchi ulizotaja. Mbona nchi za Scandinavia zenye maendeleo makubwa na raia wenye furaha zinajali sana maoni ya wananchi wake?
 
You missed my point, read between the lines. Maoni ya wananchi huchukuliwa kwa uwakilishi au sample. Tanzania ina watu 60 million, hivi unaweza kuwahoji wote?? Really?? Ndiyo maana hiyo mikutano ya kukusanya maoni kuhusu dira ya nchi huwezi kuiona ikiitishwa kila nyumba 10. Hata miswaada ya bunge wakikusanya maini wanafuata uwakilishi kwa makundi ya jamii kufika kutoa maoni au kutuma maoni yao. Mwisho mimi huwezi kunishawishi kwamba udikteta ndiyo huleta maendeleo kama hizo nchi ulizotaja. Mbona nchi za Scandinavia zenye maendeleo makubwa na raia wenye furaha zinajali sana maoni ya wananchi wake?
Kuchukua wataalamu kutoka vyuoni na taasisi mbalimbali muhimu ndio maoni yenyewe hayo, huo mtindo wa sasa hivi kuuliza watu katika majukwaa na mikutano ya kisiasa haufai.
Kuna mwingine anasema viongozi wa dini walipwe mshahara na serikali, mwingine anasema umri wa kuoa uwekewe ukomo wa miaka 30, huyu mwingine anasema watoto waimbe kwaya na kaswida, kwa vurumai hizi zinazoitwa utoaji maoni hiyo dira itakuwaje sasa??
 
Back
Top Bottom