Watoto kutokuripoti kidato cha kwanza baada ya kupangiwa shule, serikali ndio sababu. Serikali isikwepe wajibu

Watoto kutokuripoti kidato cha kwanza baada ya kupangiwa shule, serikali ndio sababu. Serikali isikwepe wajibu

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari!

Nimefuatilia habari za mikoa mbalimbali na wilaya zake, watoto wengi ambao wamepangiwa shule za sekondari kuanza kidato cha kwanza hawajaripoti shule mpaka leo. Yawezekana wapo wazazi ambao wanajichanga ili wawapeleke watoto wao shule na pia wazazi wengine hawana mpango wowote.

Yote kwa yote serikali ndio sababu kuu isikwepe wajibu wake.

Sababu hizi ndizo zilizopelekea mpaka sasa watoto wengi ambao wamepangiwa shule za sekondari kutokuripoti shule:

1. Umaskini
Pamoja na serikali kujinasibu kugawa elimu bure lakini kwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza anapaswa kuandaliwa angalau kwa sh. Laki mbili za mahitaji yake muhimu ya shule. Serikali ya CCM ione aibu kwakuwa miaka zaidi ya 60 ya uhuru imetengeneza wamaskini wengi sana. Kuna Mtanzania laki mbili ya pamoja hawezi kuipata mpaka auze shamba lake ambalo linampa msosi.

2. Ukosefu wa ajira

Mzazi aliyeuza mali zake kumsomesha mwanae akidhani ataajiriwa ili aikomboe familia yake leo hii kijana kamaliza degree na hana ajira na kulima hataki kageuka mdhululaji mjini, hana faida kwa wazazi. Sasa mzazi kujitoa kafara kwa mtoto mwingine hawezi.

3. Udhaifu wa elimu ya Kitanzanja
Waliosoma kama hawajaajiriwa hawana utofauti na wasiosoma ndani ya jamii zao. Wazazi hawana msukumo wa kuwasomesha watoto wao.
 
Hoja zote tatu ni dhaifu sana kutetea lengo la mada yako.

Kwenye hoja ya kwanza hujaelezea umaskini wa watu hususani wa mtu mmoja mmoja kwa sababu mpaka sasa nchi yetu ipo kwenye relative poverty kutoka absolute poverty.

Ningekubaliana na wewe Kama ungeniambia umasikini umepelekeaje wanafunzi kutoripoti shule ikiwa changamoto kubwa ya malipo ya ada serikali imeondoa?

Hoja ya pili umezungumzia ukosefu wa ajira lakini umeshindwa kuhusanisha ukosefu wa ajira na wanafunzi kutoripoti shule na kituko kingine umesema mzazi kauza mali zake ili asomeshe na matokeo yake akakosa ajira. Je, ni kweli mzazi anatakiwa kuuza mali ili asomeshe kipindi hiki?

Hoja ya tatu nitakubaliana na wewe ikiwa tu tutakubaliana kwamba udhaifu huo unasababishwa na wasomi wenyewe. Nchi nyingine wasomi wana nguvu sana na wanaungana kufanya jambo moja. Badala vijana wasomi waungane kutafuta fursa ila wanaungana kukutana vijiweni kwenye kamari, hivi kweli kabisa hata wewe utamheshimu msomi wa namna hii kutwa yupo kijiweni na wahuni kucheza kamari?
 
Hoja hazina mashiko.

Mkuu, peleka mtoto shule,usimuangamize na kumuua kwa ujinga. Umaskini chanzo kikuu ni mtu binafsi sio serikali.

Hao wazazi wasiopeleka shule ndio hao hao maskini wanaokimbia majukumu,kazi na uvivu wa kukata kujihangaisha. Na wengine Wana Plan kugeuza watoto kitega uchumi na nguvu kazi za kubeba majukumu ya wazazi. Mfano kuwaozesha,kufanya kazi za kilimo,kuchunga mifugo n.k
 
Pelekeni watoto shule,sio baada ya miaka kadhaa mnaaza kunyooshea vidole makabila fulani kwamba wametawala serikalini na kwenye ajira kwa ujumla.
 
Write your reply. Inakatisha tamaa unamsomesha mtoto mpaka chuo kikuu mwishowe anashnda kijiweni hana kazi yule aliyeishia std7 ananafuu au yuko vzuri kimaisha.mwishowe mzaz anaona ni bora alime anaweza kuwa na maisha mazuri kuliko kusoma nakuishia mtaani
 
Mmeamua kumshambulia Mtoa mada ila anachosema ndio ukweli, changamoto pekee ninayoiona hapa ni namna ya uwasilishaji.

Na sasa mnavyokataa kuwa Umasikini kuchangia kumbe basi ni nini? kwamba mamia ya Wazazi wameamua tu kususa kupeleka Watoto shule, ili iweje sasa?.

Hivi kwani kuna changamoto gani kwa Mzazi kwa suala la kumwambia tu Mtoto amka nenda shule?. kwani mimi Mzazi napoteza nini hapo?.

Kwanza Mtoto mwenyewe keshapata taarifa za kuchaguliwa, Shule aendayo anaifahamu na wala mimi Mzazi sihitaji kutumia nguvu yoyote...ila sasa Mtoto kabla ya kwenda shule anapewa Fomu ya maelekezo ya kujiunga (joining instruction) inayohusisha gharama...na hapo ndio Mzazi na Mtoto wanaanza kupigana chenga.

Zinatakiwa Uniforms +Mihuri ya shule, Tracksuit, Sweta, tai, Madaftari zaidi ya 10 yanayouzwa kati ya sh 2000-2500 na Viambatisho vingine kadhaa, nauli ya kila siku kwa wale waliopangiwa mbali na nyumbani, pesa ya chakula cha mchana shuleni, kuna wanachoita (remedial) Mzazi unatakiwa kutoa hela ya kila mwisho wa mwezi, Mwanafunzi anatakiwa aende na Rubber Squizer n.k.

Na hapa ndipo mtafutano kati ya Mzazi na Mtoto unaanza. Na si kweli kwamba Wakubwa mkishatamka basi na Walimu wanaacha hivyo, Walimu wana sumbua sana Wanafunzi huku nyuma ingawa mtajifanya hamjui. Lakini
Walimu wanahakikisha Mwanafunzi asiyekamilisha hayo anakosa amani hapo Shuleni + Mtoto Mwenyewe kuishia kutengwa, kwa mfano kama hajachanga ananyimwa chakula huku wenzake wanakula.

Wala sijasema ni Serikali inapaswa kumgharamia Mwanafunzi maana mtaishia tu kuhoji "kwa nini ulizaaa"....nilichojaribu kufafanua hapa ni sababu halisi ambazo zinawakabili zaidi ya asilimia 95 ya Wazazi na Wanafunzi.

Ninyi Mlioajiriwa au Wenye vipato mnaropokwa kirahisi tu mnachojisikia lakini niwaambie tu hili wala si tatizo tu kwa Serikali bali ni tatizo pia kwa Mzazi, sio jambo rahisi kwa Mzazi anayelea peke Mtoto anakusimamia hapo analia kisa tu hujakamilisha mahitaji yake ya Shule aende. Mwisho huwa Mama analia na Mtoto analia.

Walau nimemsikia Mbunge wa Monduli yeye aliamua kwenda kwenye mzizi wa tatizo lakini sio tu kusimama na kuanza kuwatishia Wazazi.

Na Mtoa uzi anaposema ukosefu wa ajira unachangia sioni ni kipi hamuelewi hapa?, hivi kama huyu Mzazi anatafuta ajira hata tu ya kuwa Msaidizi wa Mama lishe na anakosa unafikiri wewe unayekula na kuvimbiwa kila siku utaona ni tatizo?.
 
nilitaka kuandika hili leo ili wadau wachanganue chanzo ni nini maana inapelekea mpaka ma DC na RC wameamua kufanya msako pamoja na kujenga madarasa wanafunzi hakuna
 
Kuna changamoto moja iko Mkoa wa Mara wilaya ya Musoma Mjini ,

Kwakweli tungeomba wahusika wajitahidi kwa awamu ijayo kumekua na usumbufu mkubwa kwa watoto wanaotakiwa kuripoti kidato cha kwanza.
Badala ya kuwapangia watoto shule zilizopo jirani na makazi yao wanapangiwa shule zilipoko umbali wa zaidi ya kilometa 10 , na ukizingatia maeneo ya jirani kuna shule ,badala wapelekwe hapo unakuta watoto kutoka mbali ndio wanaletwa hapo.

Mfano watoto kutoka Nyakato ,na maeneo yote ya jirani wanapelekwa shule ya Nyabisarye iliyoko vijijini ,ilihali kuna shule za jirani kama Bweri, Baruti na mshikamano.

Watoto miaka 13 atembee usiku akiwahi magari yanayopita ,ashuke huko maporini na kutembea kilometa 2 mpaka shule ni mateso.

Si hilo mnagomea masuala ya uhamisho na kusistia aripoti na mzigo wa macounter ya Quire 3(12) mgongoni jmn mbn mateso.

Wekeni utaratibu wa uhamisho kwa wanafunzi waishio mbali maana ni makosa yenu rekebisheni.
 
Mmeamua kumshambulia Mtoa mada ila anachosema ndio ukweli, changamoto pekee ninayoiona hapa ni namna ya uwasilishaji.

Na sasa mnavyokataa Umasikini kuchangia kumbe basi ni nini? kwamba mamia ya Wazazi wameamua tu kususa kupeleka Watoto shule?.

Hivi kwani kuna changamoto gani kwa Mzazi kwa suala la kumwambia tu Mtoto amka nenda shule?. kwani mimi Mzazi napoteza nini hapo.

Kinchotokea ni kuwa Mtoto mwenyewe keshapata taarifa za kuchaguliwa, Shule anaifahamu na wala Mzazi sihitaji kutumia nguvu yoyote...ila sasa Mtoto kabla kwenda shule anapewa Fomu ya maelekezo ya kujiunga inayohusisha gharama...na hapo ndio Mzazi na Mtoto wanaanza kupigana chenga.

Zinatakiwa Uniforms +Mihuri ya shule, Tracksuit, sweta, tai n.k, Madaftari 12 yanayouzwa kati ya elfu mbili hadi mbili mia tano, nauli ya kila siku kwa wale waliopangiwa mbali na nyumbani, pesa ya chakula cha mchana, kuna wanachoita (remedial) Mzazi unatakiwa kutoa hela ya kila mwisho wa mwezi, anatakiwa aende na Rubber Squizer. Na hapa ndipo mtafutano kati ya Mzazi na Mtoto unaanza. Na si kweli kwamba mkishatamka basi na Walimu wanaacha hivyo, Walimu wana sumbua sana Wanafunzi huku nyuma ingawa mtajifanya hamjui.

Wala sijasema ni Serikali inapaswa kumgharamia Mwanafunzi maana mtaishia tu kuhoji "kwa nini ulizaaa"....nilichojaribu kufafanua hapa ni sababu halisi ambazo zinawakabili zaidi ya asilimia 95 ya Wazazi na Wanafunzi.

Ninyi Mlioajiriwa au Wenye vipato mnaropokwa kirahisi tu mnachojisikia lakini niwaambie tu hili wala pia si jambo rahisi kwa Mzazi anayelea peke, kwani hali huwa ni Mama analia na Mtoto analia kadri siku zinavyotaka akaripoti shuleni na hana cha kwenda nacho.

Walau nimemsikia Mbunge wa Monduli yeye aliamua kwenda kwenye mzizi wa tatizo lakini sio tu kusimama na kuanza kuwatishia Wazazi.

Na Mtoa uzi anaposema ukosefu wa ajira unachangia sioni ni kipi hamuelewi, hivi kama huyu Mzazi anatafuta ajira hata ya Msaidizi wa Mama lishe anakosa unafikiri wewe unayevimbiwa utaona ni tatizo?.
Uko sahihi kabisa,maisha yamekua magumu sana uku mtaani,hao wanaopiga makelele tayari wameshiba maana wanakula milo mitatu kwa siku,hawawezi elewa kinachoendelea kwa mtu asie na kipato maalumu hata mlo mmoja ni shughuli pevu... [emoji174]
 
Hoja zote tatu ni dhaifu sana kutetea lengo la mada yako.

Kwenye hoja ya kwanza hujaelezea umaskini wa watu hususani wa mtu mmoja mmoja kwa sababu mpaka sasa nchi yetu ipo kwenye relative poverty kutoka absolute poverty.

Ningekubaliana na wewe Kama ungeniambia umasikini umepelekeaje wanafunzi kutoripoti shule ikiwa changamoto kubwa ya malipo ya ada serikali imeondoa?

Hoja ya pili umezungumzia ukosefu wa ajira lakini umeshindwa kuhusanisha ukosefu wa ajira na wanafunzi kutoripoti shule na kituko kingine umesema mzazi kauza mali zake ili asomeshe na matokeo yake akakosa ajira. Je, ni kweli mzazi anatakiwa kuuza mali ili asomeshe kipindi hiki?

Hoja ya tatu nitakubaliana na wewe ikiwa tu tutakubaliana kwamba udhaifu huo unasababishwa na wasomi wenyewe. Nchi nyingine wasomi wana nguvu sana na wanaungana kufanya jambo moja. Badala vijana wasomi waungane kutafuta fursa ila wanaungana kukutana vijiweni kwenye kamari, hivi kweli kabisa hata wewe utamheshimu msomi wa namna hii kutwa yupo kijiweni na wahuni kucheza kamari?
Kama mleta hoja hukumuelewa na wewe ni msomi wa digirii ya mlimani..unafikiri kuna haja ya wazazi kupeleka watoto wao shuleni?
 
Mmeamua kumshambulia Mtoa mada ila anachosema ndio ukweli, changamoto pekee ninayoiona hapa ni namna ya uwasilishaji.

Na sasa mnavyokataa Umasikini kuchangia kumbe basi ni nini? kwamba mamia ya Wazazi wameamua tu kususa kupeleka Watoto shule?.

Hivi kwani kuna changamoto gani kwa Mzazi kwa suala la kumwambia tu Mtoto amka nenda shule?. kwani mimi Mzazi napoteza nini hapo.

Kinchotokea ni kuwa Mtoto mwenyewe keshapata taarifa za kuchaguliwa, Shule anaifahamu na wala Mzazi sihitaji kutumia nguvu yoyote...ila sasa Mtoto kabla kwenda shule anapewa Fomu ya maelekezo ya kujiunga inayohusisha gharama...na hapo ndio Mzazi na Mtoto wanaanza kupigana chenga.

Zinatakiwa Uniforms +Mihuri ya shule, Tracksuit, sweta, tai n.k, Madaftari 12 yanayouzwa kati ya elfu mbili hadi mbili mia tano, nauli ya kila siku kwa wale waliopangiwa mbali na nyumbani, pesa ya chakula cha mchana, kuna wanachoita (remedial) Mzazi unatakiwa kutoa hela ya kila mwisho wa mwezi, anatakiwa aende na Rubber Squizer. Na hapa ndipo mtafutano kati ya Mzazi na Mtoto unaanza. Na si kweli kwamba mkishatamka basi na Walimu wanaacha hivyo, Walimu wana sumbua sana Wanafunzi huku nyuma ingawa mtajifanya hamjui.

Wala sijasema ni Serikali inapaswa kumgharamia Mwanafunzi maana mtaishia tu kuhoji "kwa nini ulizaaa"....nilichojaribu kufafanua hapa ni sababu halisi ambazo zinawakabili zaidi ya asilimia 95 ya Wazazi na Wanafunzi.

Ninyi Mlioajiriwa au Wenye vipato mnaropokwa kirahisi tu mnachojisikia lakini niwaambie tu hili wala pia si jambo rahisi kwa Mzazi anayelea peke, kwani hali huwa ni Mama analia na Mtoto analia kadri siku zinavyotaka akaripoti shuleni na hana cha kwenda nacho.

Walau nimemsikia Mbunge wa Monduli yeye aliamua kwenda kwenye mzizi wa tatizo lakini sio tu kusimama na kuanza kuwatishia Wazazi.

Na Mtoa uzi anaposema ukosefu wa ajira unachangia sioni ni kipi hamuelewi, hivi kama huyu Mzazi anatafuta ajira hata ya Msaidizi wa Mama lishe anakosa unafikiri wewe unayevimbiwa utaona ni tatizo?.
Mtoto wangu alifaulu vizuri Form IV nikampeleka Form VI hakupenda kuendelea na A Level akaniambia anachotaka kufanya. Tukamlazimisha kwenda Form V baada ya miezi 4 akaniambia tena I am not comfortable na akanipa sababu zake na mifano juu. Nikam-convince kuwa amalize Form VI then ataenda anakotaka. Baada ya kumaliza Term ya kwanza hakutaka kurudi shule. Akaniambia anachotaka kusomea nikaona anyway so long as hajakataa kusoma ngoja nimpeleke anakotaka. Sijajutia uamuzi wake.
 
Kama mleta hoja hukumuelewa na wewe ni msomi wa digirii ya mlimani..unafikiri kuna haja ya wazazi kupeleka watoto wao shuleni?
Hiki ndio kinachonishangaza juu ya wasomi wa Tanzania, hapo pengine na wewe ni msomi kabisa lakini unawaza kutompeleka mtoto wako shule?
 
Hapa Mbeya mjini ili umpeleke motto shule unatakiwa:
1. Uchonge dawati
2. Peleka rim
3. Uniform pea mbili hii ni pamoja na masweta.
4. Ndoo na ufagio
5. Daftari kaunta kumi.
6. Vipimo kwa daktari.
7. Form imechukuliwa kwa elfu tatu na baadhi ya shule elfu kumi.
Ni vitu vyepesi ukivitazama lakini ni mzigo mzito kwa maskini. Maana wengine wameshindwa hata kuchukua form. Elimu bure ni siasa.
 
Hoja zote tatu ni dhaifu sana kutetea lengo la mada yako.

Kwenye hoja ya kwanza hujaelezea umaskini wa watu hususani wa mtu mmoja mmoja kwa sababu mpaka sasa nchi yetu ipo kwenye relative poverty kutoka absolute poverty.

Ningekubaliana na wewe Kama ungeniambia umasikini umepelekeaje wanafunzi kutoripoti shule ikiwa changamoto kubwa ya malipo ya ada serikali imeondoa?

Hoja ya pili umezungumzia ukosefu wa ajira lakini umeshindwa kuhusanisha ukosefu wa ajira na wanafunzi kutoripoti shule na kituko kingine umesema mzazi kauza mali zake ili asomeshe na matokeo yake akakosa ajira. Je, ni kweli mzazi anatakiwa kuuza mali ili asomeshe kipindi hiki?

Hoja ya tatu nitakubaliana na wewe ikiwa tu tutakubaliana kwamba udhaifu huo unasababishwa na wasomi wenyewe. Nchi nyingine wasomi wana nguvu sana na wanaungana kufanya jambo moja. Badala vijana wasomi waungane kutafuta fursa ila wanaungana kukutana vijiweni kwenye kamari, hivi kweli kabisa hata wewe utamheshimu msomi wa namna hii kutwa yupo kijiweni na wahuni kucheza kamari?
Hutakaa uelewe hata Yesu anarudi
 
Mmeamua kumshambulia Mtoa mada ila anachosema ndio ukweli, changamoto pekee ninayoiona hapa ni namna ya uwasilishaji.

Na sasa mnavyokataa kuwa Umasikini kuchangia kumbe basi ni nini? kwamba mamia ya Wazazi wameamua tu kususa kupeleka Watoto shule, ili iweje sasa?.

Hivi kwani kuna changamoto gani kwa Mzazi kwa suala la kumwambia tu Mtoto amka nenda shule?. kwani mimi Mzazi napoteza nini hapo?.

Kwanza Mtoto mwenyewe keshapata taarifa za kuchaguliwa, Shule aendayo anaifahamu na wala mimi Mzazi sihitaji kutumia nguvu yoyote...ila sasa Mtoto kabla ya kwenda shule anapewa Fomu ya maelekezo ya kujiunga (joining instruction) inayohusisha gharama...na hapo ndio Mzazi na Mtoto wanaanza kupigana chenga.

Zinatakiwa Uniforms +Mihuri ya shule, Tracksuit, Sweta, tai, Madaftari zaidi ya 10 yanayouzwa kati ya sh 2000-2500 na Viambatisho vingine kadhaa, nauli ya kila siku kwa wale waliopangiwa mbali na nyumbani, pesa ya chakula cha mchana shuleni, kuna wanachoita (remedial) Mzazi unatakiwa kutoa hela ya kila mwisho wa mwezi, Mwanafunzi anatakiwa aende na Rubber Squizer n.k.

Na hapa ndipo mtafutano kati ya Mzazi na Mtoto unaanza. Na si kweli kwamba Wakubwa mkishatamka basi na Walimu wanaacha hivyo, Walimu wana sumbua sana Wanafunzi huku nyuma ingawa mtajifanya hamjui. Lakini
Walimu wanahakikisha Mwanafunzi asiyekamilisha hayo anakosa amani hapo Shuleni + Mtoto Mwenyewe kuishia kutengwa, kwa mfano kama hajachanga ananyimwa chakula huku wenzake wanakula.

Wala sijasema ni Serikali inapaswa kumgharamia Mwanafunzi maana mtaishia tu kuhoji "kwa nini ulizaaa"....nilichojaribu kufafanua hapa ni sababu halisi ambazo zinawakabili zaidi ya asilimia 95 ya Wazazi na Wanafunzi.

Ninyi Mlioajiriwa au Wenye vipato mnaropokwa kirahisi tu mnachojisikia lakini niwaambie tu hili wala si tatizo tu kwa Serikali bali ni tatizo pia kwa Mzazi, sio jambo rahisi kwa Mzazi anayelea peke Mtoto anakusimamia hapo analia kisa tu hujakamilisha mahitaji yake ya Shule aende. Mwisho huwa Mama analia na Mtoto analia.

Walau nimemsikia Mbunge wa Monduli yeye aliamua kwenda kwenye mzizi wa tatizo lakini sio tu kusimama na kuanza kuwatishia Wazazi.

Na Mtoa uzi anaposema ukosefu wa ajira unachangia sioni ni kipi hamuelewi hapa?, hivi kama huyu Mzazi anatafuta ajira hata tu ya kuwa Msaidizi wa Mama lishe na anakosa unafikiri wewe unayekula na kuvimbiwa kila siku utaona ni tatizo?.
Dah umesawazisha vema sana huu mjadala. Naona wadau wanajibu juu juu wanaacha kuaddress issue au tatizo wanamshambulia mleta uzi as if ametukana au ameandika pumba.

Mleta uzi ameweka changamoto wazi bila shida.
 
Unaweza usijutie kwa sasa lakini kuna future gani kwenye kazi ya ufundi bomba?
Issue sio future gani katika "ufundi bomba".

Isuue ni uwezo wa kujitegemea baada ya kuhitimu hicho alichokitaka, na naamini alifanikiwa katika hili ndio maana ekiri hapa hakujutia katika kumuunga mkono mwanae katika alichokipenda.
 
Hoja zote tatu ni dhaifu sana kutetea lengo la mada yako.

Kwenye hoja ya kwanza hujaelezea umaskini wa watu hususani wa mtu mmoja mmoja kwa sababu mpaka sasa nchi yetu ipo kwenye relative poverty kutoka absolute poverty.

Ningekubaliana na wewe Kama ungeniambia umasikini umepelekeaje wanafunzi kutoripoti shule ikiwa changamoto kubwa ya malipo ya ada serikali imeondoa?

Hoja ya pili umezungumzia ukosefu wa ajira lakini umeshindwa kuhusanisha ukosefu wa ajira na wanafunzi kutoripoti shule na kituko kingine umesema mzazi kauza mali zake ili asomeshe na matokeo yake akakosa ajira. Je, ni kweli mzazi anatakiwa kuuza mali ili asomeshe kipindi hiki?

Hoja ya tatu nitakubaliana na wewe ikiwa tu tutakubaliana kwamba udhaifu huo unasababishwa na wasomi wenyewe. Nchi nyingine wasomi wana nguvu sana na wanaungana kufanya jambo moja. Badala vijana wasomi waungane kutafuta fursa ila wanaungana kukutana vijiweni kwenye kamari, hivi kweli kabisa hata wewe utamheshimu msomi wa namna hii kutwa yupo kijiweni na wahuni kucheza kamari?
Paragraph Yako ya mwisho umejaribu kuanika Ubovu wa mitaala yetu inayozalisha wasomi wa vijiwemni

Hongera sana. Haya ni matokeo ya Mitaala isiyokidhi Mahitaji ya jamii matokeo yake kuwa na wasomi wa vijiweni wanaocheza kamari
 
Back
Top Bottom