Watoto wa viongozi wakuu wa nchi walipwe ili kuwatia moyo

Watoto wa viongozi wakuu wa nchi walipwe ili kuwatia moyo

Naunga mkono hoja, ila malipo hayo sio kwa ajili ya kuwatia moyo bali ni compensation of loss of parental love and parental quality time with their children and kupunguza mateso ya ridicule kwa wazazi wao, wao ndio waathirika.

P
Tambua kuna mzazi maskini kucha kutwa anahangaika kutafuta mkate wa familia yake,alipe kodi ya nchi na kodi lukuki za familia yake ,anaamka saa kumi usiku kuwahi masokoni kuchagua bidhaa za kuuza.

Ulalaji wake ni saa nne au saa tano usiku.Ifike mahali tuache kuwaza kwa kutumia makalio,watoto wa viongozi wana shida ipi ukilinganisha na watoto wa masikini,poor african mindset
 
Walipwe tu.
Nchi za Dona Cantry Kama Tanganyika huwa raia wake wote wanalipwa.
Sembuse ndugu na marafiki wa viongozi, mbona ni wachache tu.

Walipwe naunga hoja mkono.
 
Unahitaji kuwa na mfano unapo4aka kutunfa sera.
Hii itakuwezesha kuaemq tufanye hili kama kule wanavyofanya hivi.( na wakifanya hivyo mambo yao yanaenda vizuri).
Serikali inapotoa kodi
za wananchi kumpa mtu huyu au yule,no vizuri ku double- check Kama mtu yule ana shida.
Kwa mfano hii muswada wa kuongeza ruzuku ya wenza wa marais wastaafu .
Ninavyofamu mimi Salma Kikwete no filthy rich.(Unaposema mtu ni "filthy rich" Ina maana ni tajiri sana,haina maana kwamba hela zake amezipata kwa njia za kifisadi).
Likewise,mama Anna Mkapa,I imagine,is filthy rich. Napita kule Mandela Road
naona ipo Mkapa Economic Zone.
Mama Janet Magufuli, I imagine,is filthy rich. Nikifikiria Magufuli alipofariki salami za rambi rambi zilitolewa na Prince Charles,Prince William ni Queen Elizabeth( of Blessed Memory).
Again,Mama Sitti Mwinyi. I imagine hakulalamika njaa ili Bunge limuongezee ruzuku.
Now,nimeshasahau nilikuwa naandika kuhusu Nini. Ah,yes ruzuku. Kwa sababu utasikia wanajeshi wastaafu wanasema hawajalipwa mafao.
Kwa nini Bunge linataka kuwafurahisha watu ambao wameshafurahi?
Will Parliament do this again?
Kwa sababu hii ndiyo maana ya Bunge,kuweka spies(wabunge) here and there na kupeleka msaada penye shida.
 
Hata wake za madereva wa viongozi walipwe waume zao wanatumia muda mwingi nje ya familia kuendesha viongozi
Naunga mkono hoja, hata waume wa makatibu muhitasi nao walipwe fidia wake zao wanashinda ofisini na bosi muda mwingi, wakati wa Bunge sometimes hadi saa 6 usiku!, mke anafika home exhausted, hiyo kushindwa kutekeleza yale majukumu ya ndoa kikamilifu. Hivyo waume zao wanastahili compensation!.
P
 
Tusiishie hapo tu hata wakwe zao yaani ukioa au kuolewa kwenye familia ya kiongozi pia ulipwe, ndugu wajomba mashangazi mabinamu na wajukuu wote walipwe.

Mpaka wafanyakazi wa ndani na wafungua mageti na madereva pia walipwe na serikali tena.

Maoni yangu naomba yaheshimiwe.👆✌️
msigwa
 
WATOTO WA VIONGOZI WAKUU WA NCHI WALIPWE ILI KUWATIA MOYO.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Nimefurahi muswada wa kuwalipa wenza wa viongozi wa nchi. Ni uzalendo wa hali ya juu sana. Hii itachochea maendeleo makubwa ya nchi.

Lakini ninaishauri pia serikali, isiishie tuu hapo iende mbali zaidi kuchochea maendeleo ya nchi yetu kwa kuwalipa na watoto wa viongozi wa taifa letu tukufu.

Watoto wa Marais Walipwe.
Watoto wa Makamu wa rais Walipwe.
Watoto wa Spika wa bunge walipwe
Watoto wa Waziri Mkuu walipwe!
Watoto wa Jaji Mkuu walipwe.
Watoto wa Ma-IGP walipwe.
Watoto wa Wakurugenzi wakuu wa TISS walipwe.

Wapewe Mishahara hata milioni moja au mbili au tatu hivi kwa mwezi. Hayo ndio maendeleo. Wazazi wao wanatumikia nchi hilo nani atabisha?

Wazazi wao wanatumia muda mwingi nje ya familia zao na kuhangaikia nchi, nani anabisha? Wazazi wao wanatukanwa na wananchi wakati mwingine bila kosa nani anabisha?

Walipwe! Walipwe! Tuwalipe! Kodi ni zetu na wao ni viongozi wetu. Tunafurahi wakilipwa. Sisi tutawatumikia kama wao wanavyotutumikia ili kuiendeleza nchi.

Watoto wa viongozi jiandaeni. Tutawalipa kila mwezi. Ni bora tuwalipe tuu kuliko mjilipe wenyewe kwa kificho. Hata tusipowalipa tunajua mtajilipa kivyovyote tuu.

Muswada upelekwe bungeni, kisha upitishwe. Watoto nao walipwe.
Ambao hawataki wahame nchi.

Tusiishie kuwalipa Wenza wao(waume na wake zao) twendeni mbele zaidi. Tuwe na jicho la mbali kama tai.

Mimi nimemaliza, hayo ni mawazo yangu. Kama hutaki hayo ni mawazo yako na kwangu sio shida.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Na wajukuu walipiwe ada za international schools sababu ndio viongozi wa kesho
 
Back
Top Bottom