Watoto wafundishwe masomo kwa kiingereza toka wanapoanza nursery school

Watoto wafundishwe masomo kwa kiingereza toka wanapoanza nursery school

Sio tu pesa,hata nyumbani kama mnaongea kiingereza mtoto anaweza kucatch up,mie nimesoma kayumba ila mzungu hanitoi jasho,bibi alihusika sana home kunikomalia kila nikitoka shule
Alikua ananikazania na story books na kunisemesha mpaka tukaanza kuelewana
Ni kweli b inategemea nyumbani man mazingira gani.
Na jingine huko shuleni, waalimu wana kiingereza?
Sikusoma English medium, ila waalimu wa kiingereza walitokea kujua nini wanachofundisha akiwemo mhindi, na nyumbani wazazi ni wasomi,vhatikuingea kiingereza ila ikitokea, kuna mazingira ya kuongea kiingereza unaongozwa, unarekebishwa n.k. vitabu mpaka novels zilikuwepo na nilianza kuzisoma nikiwa shule ya msingi. Sekondari haikuwa tatizo.
 
Elimu yetu inahitaji maboresho sana, lugha ikiwa ni moja wapo....English inakuja kuwa lugha ngeni kwa mwanafunzi kujifunza na kuiweza kuimudu , aongee na aandike English iliyonyooka sio kazi rahisi ilitakiwa aanze tangu nursery.

Kuna mwanafunzi wa form four nilikua nampa a,b,c za kusoma kwa ajili ya practical, nikamuelekeza akasome baadhi ya specimen kama maize seed and bean seed ambazo tayari walikua washafundishwa, baada ya dakika akarudi kuniuliza kati ya maize na beans ipi ni maharage...
Sijajua bado huyu shida ni lugha tu au kuna mengine.
Hapo ni wazi kuwa tatizo ni lugha.
 
Hadi TV ilikua marufuku kuangalia vipindi vya kiswahili
Ving'amuzi/Visimbuzi/Vising'ombe 🙂 au viite vyovyote upendavyo, siku hizi vipo hata kwenye kaya tajiri mpaka maskini. Siyo tena kipimo cha "ushua" kama ilivyokuwa zamani. Amri hiyo ya kupiga marufuku vipindi vya Kiswahili, hasa kwa mtoto anapokuwa na umri wa miaka sufuri (0) mpaka mitatu (3); na miaka mitatu (3) mpaka sita (6), huweza kumfanya mtoto kujifunza mwenyewe Kiingereza kwa mtindo wa uzamiaji ("immersion"). Shuhuda ziko nyingi Uswazi na vijijini watoto ghafla wanaanza kutema ung'eng'e kutokana na kuangalia katuni tu za Kiingereza.

Kwani Kiswahili nani aliwafundisha? Njia hiyohiyo hapo juu ya uzamiaji ndiyo ilitumika kumfanya mtoto ajue Kiswahili: kwa kusikia Kiswahili kila mahali.

Maria Montessori kaelezea hili KWA KIREFU.
 
Sijui tunakwama wapi aiseeh, na issue sio kwamba hawajui au hawaelewi kilichosahihi kufanyika laah asha wanajua kila kitu sema tuu hawataki
Kumbe hujui asilimia kubwa ya watoa maamuzi shule za English medium ndiyo biashara zao, sasa wakibadili mfumo si watakosa wateja? Ninachokiona hapa ni ubinafsi uliopitiliza wakati wenyewe watoto wao wanawapeleka nje ya nchi kusoma.

Na bado wanataka eti nchi iendelee sijui ni nani aliyetuloga.
 
Hili ndio wengi hawajui. Mm mwenyewe nimejua kimombo sababu nyumbani wazazi walikua hawaongei kiswahili. Ukiongea kiswahili hakujibu chochote na yeye anakutuma kwa kimombo. Japo nilisoma kayumba. Hadi TV ilikua marufuku kuangalia vipindi vya kiswahili, hadi leo mm huwezi ukanikuta nafatilia vipindi au habari za kiswahili
Woow😍
 
Ving'amuzi/Visimbuzi/Vising'ombe 🙂 au viite vyovyote upendavyo, siku hizi vipo hata kwenye kaya tajiri mpaka maskini. Siyo tena kipimo cha "ushua" kama ilivyokuwa zamani. Amri hiyo ya kupiga marufuku vipindi vya Kiswahili, hasa kwa mtoto anapokuwa na umri wa miaka sufuri (0) mpaka mitatu (3); na miaka mitatu (3) mpaka sita (6), huweza kumfanya mtoto kujifunza mwenyewe Kiingereza kwa mtindo wa uzamiaji ("immersion"). Shuhuda ziko nyingi Uswazi na vijijini watoto ghafla wanaanza kutema ung'eng'e kutokana na kuangalia katuni tu za Kiingereza.

Kwani Kiswahili nani aliwafundisha? Njia hiyohiyo hapo juu ya uzamiaji ndiyo ilitumika kumfanya mtoto ajue Kiswahili: kwa kusikia Kiswahili kila mahali.

Maria Montessori kaelezea hili KWA KIREFU.
Huo ung'eng'e anaoutema mtoto baada ya kuangalia katuni anaelewa maana yake? au anadaka tu yes..no...yes.....hapo atakariri baadhi ya maneno tuu halafu kuyaandika kwa usahihi atajuaje?
 
Sijui kingereza Mimi mkuu [emoji3]

Kingereza kililetwa na meli mkuu.

Kwa Kiswahili, kitabu kinaitwa: AKILI YA SPONJI. Kwenye hicho kitabu Montessori anasema akili ya mtoto husharabu elimu na maarifa (ikiwemo lugha) kama vile sponji linavyofyonza maji.

Endelea kukisoma kitabu hicho HAPA kwa Kiswahili cha kutafsiriwa na kompyuta.
 
Kingereza kililetwa na meli mkuu.

Kwa Kiswahili, kitabu kinaitwa: AKILI YA SPONJI. Kwenye hicho kitabu Montessori anasema akili ya mtoto husharabu elimu na maarifa (ikiwemo lugha) kama vile sponji linavyofyonza maji.

Endelea kukisoma kitabu hicho HAPA kwa Kiswahili cha kutafsiriwa na kompyuta.
Poa poa
 
Wasalaam wakuu

Hivi ni kwanini watoto wetu wasifundishwe masomo kwa kiingereza toka wanapoanza nursery?

Huu mfumo wa kuwafundisha kwa kiswahili mpaka la saba halafu waanze tena kufundishwa kwa kiingereza kuanzia form one ni mgumu mno

Mtoto akifundishwa kwa kiingereza tokea nursery school inamjenga anakuwa na uwezo mkubwa wa kuongea na kuandika kiingereza vizuri tu.

Watoto wafundishwe kwa kiingereza toka nursery school, hicho kiswahili kama kina faida basi wafundishwe kwa kiswahili tokea nursery mpaka chuo.

Serikali inakwama wapi kubadili huu mfumo wa elimu?

Wanasemaga samaki mkunje angali mbichi

Au mnaonaje wananzengo?
Kwa lugha myepesi unataka shule zote za msingi za serikali ziwe English media

Hilo linawwzekana kwa sasa nchi yetu ina waalimu wa kutosha kufanya kazi hiyo

Ila tatizo hao ambao wanatakiwa watoe maamuzi hayo wao hilo haliwagusi kwa sababu wao watoto wao wanasomesha English media

Kama mama SAMIA anataka watanzania wasimsahau maisha yote basi amuru shule zote za serikali ziwe English media

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kushikilia, kusimamia na kutetea kile kinachohusu nchi yako kwa misimamo yote...

kiwe kibaya au kizuri...
Sawa basi lugha ya kufundishia isibadilike toka nursery kama ni kiswahili kitumike mpaka chuo huko Kama ndo huo uzalendo unaoutaka wewe
 
Suala siyo la kusomesha watoto English Media schools Bali ni wizara ipeleke mswada bungeni wa kubadili lugha ya kufundishia kwa ngazi zote za elimu!
Kiingereza ni lugha ya dunia nzima kwa Sasa na ndio lugha kuu ya teknolojia ambayo ndiyo inayotawala uchumi wa dunia. Kama nchi tusijidanganye na kiswahili chetu kwani tutaendelea kuwa maskini daima dumu! Chungulia hapo Kenya na Uganda ambao wanaotumia kiingereza kufundishia ngazi zote huku wakiongea kiswahili fasaha kushinda hata sisi!
Tunaking'ang'ania kiswahili ili iweje ilihali kwasasa ni mother tongue kwa watoto wetu wengi? Waziri abadili hii kitu haraka kama kweli tuna lengo la kuingia na kubaki uchumi wa Kati!
 
Suala siyo la kusomesha watoto English Media schools Bali ni wizara ipeleke mswada bungeni wa kubadili lugha ya kufundishia kwa ngazi zote za elimu!
Kiingereza ni lugha ya dunia nzima kwa Sasa na ndio lugha kuu ya teknolojia ambayo ndiyo inayotawala uchumi wa dunia. Kama nchi tusijidanganye na kiswahili chetu kwani tutaendelea kuwa maskini daima dumu! Chungulia hapo Kenya na Uganda ambao wanaotumia kiingereza kufundishia ngazi zote huku wakiongea kiswahili fasaha kushinda hata sisi!
Tunaking'ang'ania kiswahili ili iweje ilihali kwasasa ni mother tongue kwa watoto wetu wengi? Waziri abadili hii kitu haraka kama kweli tuna lengo la kuingia na kubaki uchumi wa Kati!
[emoji122][emoji122]
 
Back
Top Bottom