Pichani watoto hawa wamekutwa wakisafiri uvunguni mwa basi la Happy Nation Bukoba - Mwanza:
Hadi wanafumwa huko chini walikuwa wameshamaliza angalau kilometers 200.
Hawa ndiyo ile sampuli ya watoto wa wakulima tunaotaka kuaminishana kwa nguvu kuwa wazazi wao sasa wanaouza chakula nje. Kwamba kwa sababu hiyo hawana shida ya chakula ila mijini."
Hii ndiyo Tanzania ambayo viongozi wake wako busy wanatumbua na wengine kupora pesa bila ya aibu kupeleka China huku chawa wakikenua.
======
Watoto sita wenye umri kati ya miaka 12 na 16 wamekamatwa na Jeshi la polisi mkoani Geita wakisafiri wakiwa chini ya basi kutoka mjini Bukoba mkoa wa Kagera kwenda jijini Mwanza, jambo ambalo ni hatari kwa maisha yao.
Watoto hao wanaodai kuishi kwenye kituo cha mabasi Bukoba wamedai walilazimika kusafiri wakiwa chini ya gari ili waweze kufika Mwanza ambako wanadhani kuna unafuu wa maisha ikilinganishwa na Bukoba.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti leo Februari 7, 2023 wakiwa kituo cha polisi Geita wamedai kwamba waliingia kwenye basi la Happy Nation saa 9 usiku na kujificha kwenye “chassis” ya gari hadi asubuhi lilipoanza safari ya kwenda Mwanza.
“Kuna mwenzetu alisema yeye aliwahi kupanda chini ya gari kutoka Bukoba hadi Mwanza na hakupata shida akatuambia maisha ya huko ni mazuri ndio maana tulikubali kwenda lakini tulipofika hapa tukakamatwa na polisi wakatuleta kituoni,” amesema mmoja wa watoto hao.
Amesema alilazimika kuishi mtaani baada ya mama yake kufariki na bibi anaewalea ni mzee asiye na uwezo, hivyo kulazimika kutafuta pesa ili aweze kumtunza bibi na mdogo wake.
Watoto sita wakamatwa wakisafirichini ya uvungu wa basi la Bukoba-Mwanza
Mtoto mwingine (16) amesema aliacha shule baada ya kufeli mtihani wa darasa la nne. Amedai kwamba hana wazazi na amekuwa akiishi na shangazi yake lakini alipigwa na mjomba wake na kuamua kutoroka na kuishi mtaani.
“Kwenye gari chini kuna chuma mbili moja inachemka nyingine haichemki, hiyo moja ndio tunabebana huko chini kuna vumbi tuu kukiwa na mvua na upepo huumii lakini kukiwa na vumbi unaweza kugongwa hata na jiwe. Mimi nimeshapanda tena kutoka Bukoba hadi Mwanza,” amesema mtoto huyo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Geita, Safia Jongo amethibitisha kukamatwa kwa watoto hao na kusema watoto hao wamebainika kuishi mtaani huku wengine wakilelewa kwenye kituo cha watoto cha Hekima kilichopo Bukoba.
Jongo amesema watoto hao wamekosa malezi ya wazazi na wengine kutelekezwa na familia baada ya wazazi wao kufa na kwamba watoto hao wanatunzwa ili taratibu za kiustawi wa jamii zikamilike na kuwa wazazi wa watoto hao watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria kwa kushindwa kuwa
Hadi wanafumwa huko chini walikuwa wameshamaliza angalau kilometers 200.
Hawa ndiyo ile sampuli ya watoto wa wakulima tunaotaka kuaminishana kwa nguvu kuwa wazazi wao sasa wanaouza chakula nje. Kwamba kwa sababu hiyo hawana shida ya chakula ila mijini."
Hii ndiyo Tanzania ambayo viongozi wake wako busy wanatumbua na wengine kupora pesa bila ya aibu kupeleka China huku chawa wakikenua.
======
Watoto sita wenye umri kati ya miaka 12 na 16 wamekamatwa na Jeshi la polisi mkoani Geita wakisafiri wakiwa chini ya basi kutoka mjini Bukoba mkoa wa Kagera kwenda jijini Mwanza, jambo ambalo ni hatari kwa maisha yao.
Watoto hao wanaodai kuishi kwenye kituo cha mabasi Bukoba wamedai walilazimika kusafiri wakiwa chini ya gari ili waweze kufika Mwanza ambako wanadhani kuna unafuu wa maisha ikilinganishwa na Bukoba.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti leo Februari 7, 2023 wakiwa kituo cha polisi Geita wamedai kwamba waliingia kwenye basi la Happy Nation saa 9 usiku na kujificha kwenye “chassis” ya gari hadi asubuhi lilipoanza safari ya kwenda Mwanza.
“Kuna mwenzetu alisema yeye aliwahi kupanda chini ya gari kutoka Bukoba hadi Mwanza na hakupata shida akatuambia maisha ya huko ni mazuri ndio maana tulikubali kwenda lakini tulipofika hapa tukakamatwa na polisi wakatuleta kituoni,” amesema mmoja wa watoto hao.
Amesema alilazimika kuishi mtaani baada ya mama yake kufariki na bibi anaewalea ni mzee asiye na uwezo, hivyo kulazimika kutafuta pesa ili aweze kumtunza bibi na mdogo wake.
Watoto sita wakamatwa wakisafirichini ya uvungu wa basi la Bukoba-Mwanza
Mtoto mwingine (16) amesema aliacha shule baada ya kufeli mtihani wa darasa la nne. Amedai kwamba hana wazazi na amekuwa akiishi na shangazi yake lakini alipigwa na mjomba wake na kuamua kutoroka na kuishi mtaani.
“Kwenye gari chini kuna chuma mbili moja inachemka nyingine haichemki, hiyo moja ndio tunabebana huko chini kuna vumbi tuu kukiwa na mvua na upepo huumii lakini kukiwa na vumbi unaweza kugongwa hata na jiwe. Mimi nimeshapanda tena kutoka Bukoba hadi Mwanza,” amesema mtoto huyo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Geita, Safia Jongo amethibitisha kukamatwa kwa watoto hao na kusema watoto hao wamebainika kuishi mtaani huku wengine wakilelewa kwenye kituo cha watoto cha Hekima kilichopo Bukoba.
Jongo amesema watoto hao wamekosa malezi ya wazazi na wengine kutelekezwa na familia baada ya wazazi wao kufa na kwamba watoto hao wanatunzwa ili taratibu za kiustawi wa jamii zikamilike na kuwa wazazi wa watoto hao watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria kwa kushindwa kuwa