Watu 20 wahofiwa kufariki baada ya basi walilokuwa wakisafiria kugongana na lori mjini Nzega, leo Oktoba 21, 2023

Watu 20 wahofiwa kufariki baada ya basi walilokuwa wakisafiria kugongana na lori mjini Nzega, leo Oktoba 21, 2023

Uwezo wa kiakili wa madereva na barabara haziruhusu gari kwenda zaidi ya speed 80kph. Hii magari yanayokuja Tz yasiwe na uwezo zaidi ya huo.
 
Dereva wa Lori alikua amesinzia ngoma ikahama njia
 
Ajali Uchama Nzega: Basi la Alpha limegongana na lori la GBP.
View attachment 2788128

===

Watu 20 wanahofiwa kufariki baada ya basi walilokuwa wakisafiria kugongana na lori mjini Nzega.

Akitoa taarifa ya ajali hiyo leo Jumamosi Oktoba 21, 2023, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Richard Abwao amesema ajali hiyo imehusisha basi la Alpha linalofanya safari zake kati Shinyanga na Dar es Salaam na kwamba wakati wa ajali, lilikuwa likitokea Shinyanga.

"Nimepata taarifa hiyo na sasa ndio naelekea eneo la tukio na taarifa kamili nitaitoa baada ya kufika na kujua hali ilivyo," amesema.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Naitapwaki Tukai amesema amepata taarifa ya ajali hiyo akiwa wilayani Sikonge katika maadhimisho ya miaka 100 ya Hospitali ya Misheni
inayomilikiwa na Kanisa la Moravian, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dk Batilda Burian.

Amesema baada ya baada ya kupata taarifa hiyo ameelekea kwenye eneo la tukio.

Hii ni ajali kubwa kuua idadi kubwa ya watu katika Mkoa wa Tabora kwa mwaka huu.

Mwananchi
Mkuu wa Wilaya ya Nzega anamwakilishaje Mkuu wa Mkoa wa Tabora huko Sikonge ambako siyo wilaya ya Nzega?
 
Hivi kwa wastani hii nchi watu wangapi wanakufa kwa ajali kila siku?
 
Nzega na sikonge zote zipo mkoa wa Tabora
Hizo ni wilaya tofauti. Mkuu wa wilaya ya Nzega hahusiki na Sikonge ambayo ina mkuu wa wilaya mwingine. Ni sawa na kusema Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni akamwakilishe Mkuu wa Mkoa wa Dar katika shughuli inayofanyika Temeke Yombo, eti kwa kuwa tu maeneo yote yako mkoa wa Dar.
 
Mungu atulinde sote, tuwa makini watumiaji wote wa barabara.
 
Hyo ajali aisee imeniogopesha sanaa.....uzembe wa dereva wa lorry imewacost abiria na dereva wa basi..

Afu dereva wa lorry katoka mzimaa...

Innalillah wainnailayh rajiuun..
 
Back
Top Bottom