Watu tuliopata A, B na C hatuna haja ya kuajiriwa

BIG THINKER

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2018
Posts
680
Reaction score
1,436
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza.

Inashangaza sana mtu Kidato cha Nne umepata One au Two harafu kidato, Kidato cha Sita pia ukatusua vizuri tu harafu ukaingia chuo. Chuo unatoka na GPA ya nzuri kabisa ya kwamba masomo ya chuo ww unayaweza. Hongera!

Harafu unakuja mtaani unaanza kulilia ajira za SERIKALI kwahiyo hiyo akili yako uliyoitumia kufauru darasani unashindwa kuitumia kufauru mtaani aibu kubwa sana kwako.

Utasema elimu yetu haimfundishi mtu kujiajiri, Sasa nakuuliza swali huyo aliyekomea darasa la Saba au kidato Cha nne akafel amewezaje kujiajiri Pumbavu sana. Mimi binafsi nimejiajiri sipokei mshahara wa SERIKALI hata mia pia siyo chawa wa mtu na Nina degree mbili.

Na nikwambie tu sina mpango wa kusaka ajira yoyote ya SERIKALI, natumia elimu yangu vizuri. Haiwezekan nipate one kidato cha nne cha SITA pia, chuo nipate GPA ya 4.7 harafu nishindwe na maisha ya mtaani ni aibu.

Kuna madhara makubwa sana kufauru kwa ujanja ujanja ukapata matokeo makubwa kumbe huna uwezo nayo. Haya Sasa unadgree yako unapambana uwe polisi Ili iweje kweli kazi ya polisi inahitaji degree!?

Na mimi naipongeza SERIKALI kuchukua madaraja ya chini division four na three Ili sisi tulio na one, two tuoneshane uwezo wa akili yetu kwa vitendo mtaani.

Baada ya kusema hayo nasema.

Nitarudi....

 
Unazijua requirements na mazingira ya kujiajiri, au mkibahatika kutusua mnajiona miamba sana wengine wote mazuzu. Watu wanatofautiana kwenye nyanja mbalimbali, usifikiri kwamba wote wana uwezo sawa wa kujiajiri au kuwa wajasiriamali.​
Kabisa mkuu.Nikumshukuru Mungu na kukaa kimya.
 
Unazijua requirements na mazingira ya kujiajiri, au mkibahatika kutusua mnajiona miamba sana wengine wote mazuzu. Watu wanatofautiana kwenye nyanja mbalimbali, usifikiri kwamba wote wana uwezo sawa wa kujiajiri au kuwa wajasiriamali.​
Kwanza uyo mtu katoka familia gan,kama ni familia ya uwezo ni rahs mtu kujiajir coz backup ya capital iko. je kwa aliyetoka famili masikin ni shida kupata hta mtaji bad TRA hawa hapa.
 
Unazijua requirements na mazingira ya kujiajiri, au mkibahatika kutusua mnajiona miamba sana wengine wote mazuzu. Watu wanatofautiana kwenye nyanja mbalimbali, usifikiri kwamba wote wana uwezo sawa wa kujiajiri au kuwa wajasiriamali.​
Hatujabahatika ingekuwa ni Bahati wote tungekuwa sehem Moja make watu wote tuna bahati
 
Mbona mwandiko tu unaonyesha sifuri kabisa, akili unaita akri basi sawa tuambie umejiajiri wapi
Na ukifika huku mtaani utaalam wako wote na ujuaji unauacha kwenye makaratasi,
Huku mtaani kwa watu waliofanikiwa akli wanaita akri pia na maisha Yao yako sawa tu
 
Arsenal 3-2 Mwamtesa United

Aliesoma akifanikiwa kuajiliwa mshahara wake unasoma 2M kwa mwezi hapo anapata take home 1.5M inayobaki ni makato ya Kodi na Nssf, unaonaje hapo, wewe mpika maandazi hapo karibu na Airport stand?

1.5M ร— 12 = ?

Usione wanaosomesha ni mafala kenge wewe,
 
Usione wanzako wavivu kisa wewe ushafanikiwa

Be humble
Wangekuwa wavivu sizan kama wangeza kupata one mashuleni


Nasema akli zilizowasaidia kufauru ziwasaidie pia kwenye maisha ya mtaani
 
Ufaulu darasani unaweza kuwa umetokana na kukariri tu ila sio kwamba mtu ni intelligent sana
Sio kweli watafute maTO utaona utofauti wao na wenye akili za kawaida, usigeneralize mambo
 
Wangekuwa wavivu sizan kama wangeza kupata one mashuleni


Nasema akli zilizowasaidia kufauru ziwasaidie pia kwenye maisha ya mtaani
KIWANDA chako kinaitwaje? Hapo ulipo unaweza ikawa hata Baiskeli tu ya miguu miwili huna
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ