Watu wa mikoani mnatujazia jiji letu

Watu wa mikoani mnatujazia jiji letu

Thread ya kijinga kuwahi kutokea hapa JF na haya ni matokeo ya kuwa na IQ ndogo.
Nina hasira sana.

Naanza na nyie watu wa mikoani ambao kila kukicha tunawapokea stand ya magu na mabegi yenu ya shangazi kaja, mkifika pale mnatapeliwa kwa kuuziwa sabuni eti mnadanganywa simu.

Nakukaribisha kwangu, kwenye chumba changu unapagawa na flat nchi 55 ukutani, sofa kali kitanda kikubwa unabaki unaduwaa maana hivi vitu vigeni kwenu ushamba huooo.

Nakupa pamba zangu huendane na watu wa Dar wasikushangae kwa manguo yako ya kishamba na maviatu yako meusi kama wanafunzi wa msingi, acheni ushamba.

Baada ya weeks kadhaa mnajiona tayari mshajua jiji na kuanza kubadilisha lafunzi eti niaje mwana kudadeki, nakulisha nakuvisha alafu unajiona mjanja wa Dar pumbavu zako.

Naomba serikali yangu iweke kuja Dar lazima uwe na Visa, maana mnajaza bure jiji letu pendwa kila mtu wa mikoani unawaza kuja tu Dar tushawachoka sasa.

Bakini huko Bush kwenu kwa hao mademu zenu wasiojua kukata mauno, hii ndo Dar.
 
Tupo wenyewe tumenyamaza tu watoto wa Shomvi. Mzaramo hasa hawezi kusema maneno haya, hawa ni wale wakuja tu, si unaona hata Kiswahili kinawapiga chenga mtu anaandika "lafunzi" badala ya lafudhi.

Watu wa asili wa miji mikubwa kikawaida huwa hawana ubaguzi, wanapenda wageni, huko kukosa ubaguzi ndiko kumefanya miji hiyo kufanikiwa.

Kuna siku nilikuwa New York City, naongea na OG mmoja mzee mweusi wa New York City, tulikuwa tunaongelea ubaguzi katika watu wa New York City wanaojiona wao watoto wa mjini. Akaniambia kuwa, wale watu wa New York City wenyewe wa asili miaka nenda miaka rudi huwa hawana noma na mtu, hawana ubaguzi, ila wale waliokuja miaka 10 au 20 iliyopita kutoka the Carolinas, Mississippi, Puerto Rico etc., ndio wenye kujifanya kwamba wao watu wa New York City sanaa, bado wanalimbuka na mji.

Sasa sisi ambao baba za bibi zetu ndio walijenga hayo majumba ya katikati Dar (baba yake bibi yangu kajenga kanisa la Azania Front, wamemaliza kujenga mwaka 1903, na kabla ya hapo familia ilikuwepo Dar es salaam) huwezi kutusikia tunatukana watu wa kuja.

Huwezi kumsikia Ali Tambaza akitukana watu wakuja na kwamba familia yao ya Jumbe Tambaza ndio wenyeji wa Dar.

Huwezi kusikia sisi kina Chanzi, kina Pazi, kina Shomvi, kina Chamgui tunawasema wakuja, labda kama utani wa jadi na watani wetu kina Rupia Wanyamwezi, na huu tunafanya kwa kujuana wenyewe bila kuhatarisha mahusiano, kuna sanaa yake.

Ukiona mtu anashikia bango kuwa yeye mtu wa Dar, na wengine ni wakuja, ujue huyo si mtu wa Dar.

Kiranga ChaNgeda Sakala Kandumbwa
Misheni Kota/Mwembetogwa/Mchafukoge/Kinyasini/ Upanga/ Oysterbay/ New York City.
Umenena vyema sana. Upewe maua yako.
 
Hata wewe ndugu mwandishi kwa hapo Daslam utakuwa wa kuja tu, hauna lolote. Kijana anaejipambania hawezi kujivuna kuwa na gheto na ndani anamiliki makochi na flatscreen.

Huo ni Umama!! (In somebody's voice).
 
Yaani kuishi dar ndio umeona kwamba dunia yote yako? Huu ni ushamba wa kijinga sana na isitoshe watu wa mikoani pamoja na ushamba wao wanakuzidi parefu mno kimaendeleo wewe endeleo kujivunia hilo geto lako.
Mpaka useme bado mkuu hujanipeleka shule acha shobo
 
Af ukute ni Hisense ndo unatunanga hivi

Bed lenyewe sofa la kichina

Nyie nyie watu wa Dar mna hilaa
😂madhara ya elnino yameshaanza, na ndo zimeanza mpaka May mwakani tuwe wavumilivu
 
Back
Top Bottom