Watu wa Mungu kulingana na hili linalo endelea ndani ya nchi yetu. Naomba tujifariji kwa neno la Mungu. Maana ukombozi umekaribia.

Mtu Alie Nyikani

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2022
Posts
949
Reaction score
2,038
Kutoka 14:14. Mithali 24:24. Zaburi 98:9. Mithari 14:34.

Kutoka 14 : 14 Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.

Mithali 24 : 24 Amwambiaye mtu mwovu, Wewe una haki; Kabila za watu watamlaani, taifa watamchukia.

Zaburi 98 : 9 Mbele za Bwana; Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa adili.

Mithali 14 : 32 Mtu mbaya husukumwa chini katika kutenda mabaya kwake; Bali mwenye haki ana matumaini katika kufa kwake.

Mithali 14 : 33 Hekima hukaa katika moyo wake mwenye ufahamu; Bali yaliyo ndani ya wapumbavu hudhihirika.

Mithali 14 : 34 Haki huinua taifa; Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.
 
🤣🤣🤣🤣🤣kumbe ni mlokole 🤭
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…