Watu wa sheria mtusaidie hapa

Watu wa sheria mtusaidie hapa

Maelezo yako pamoja na comments za wadau wote nilizosoma hapo chini, ukiachana na mambo sijui ya kisheria, zipo sawa na ndizo familia mbali mbali hufuata kugawana mirathi.

Huyo mtoto wa marehemu dada yako hana haki ya urithi wa moja kwa moja hapo.

Mlivyopanga na nduguzo kwamba muuze kisha mgao wa mirathi mumkumbuke na marehrmu ndugu yenu mmefanya jambo jema linalostahili pongezi, hamna tamaa za kijinga.

Kitu ambacho sijaelelewa, huyo mtoto wa marehemu, kazaliwa peke yake kwenye tumbo la marehemu?

Kama kazaliwa na wenzake, pia mgao mtakao mgawia marehemu ndugu yenu, inatakiwa muwagawanye na wenzake sawa kwa sawa.

Zoezi la kuuza liendelee na yote mliyopanga na dada zako yatekelezeni.

Huyo mtoto wa marehemu hana haki yoyote kuwapangia ama kuingilia suala hilo.
Uko sahihi mkuu, sisi tunataka kutumia ubinadamu tu kwamba kila mtu apate 10m bila kujali ni mtoto wa kike au wa kiume. Huyu dogo yupo mwanza mimi na mdogo wangu tupo dar, na mteja alikua ameshapatikana ilikua ni ku deposit pesa tu kwnye account. Mpaka sasa mteja kashagaili kununua hiko kiwanja. Lakini kwa ushauri wenu ngoja niendelee kutafuta mteja mwingine ili twende kibabe kama anavyotaka yeye
 
Nahisi hiki ndo alichomaanisha, maana kama atapata hizo 10M anajua kabisa hana pa kuzipeleka, au labda wao walimuuliza sababu nyengine nje ya hiyo?
Huyu dogo ni above 18 yrs. Sasa swala la yeye pesa atazipeleka wapi ni juu yake as long as sisi tumempa mgao wa mama yake ambao ni sawa na mgao wetu. Nilijaribu kumshauri pia kama walivyoshauri wadau wengine kwamba tumfungulie fixed account ili pesa yake ibaki kwa muda anaotaka yeye.
 
Yaani mjukuu anawazidi akili? Uzeni gawaneni fedha, yeye si ana Baba yake akadai urithi huko, hicho hakimuhusu...
Ninachokitaka ni kwamba huyu dogo nae apate kwa niaba ya marehemu mama yake ambae ni dada yangu. Lakini hili swala kama walivyoshauri wadau wengine inabidi nilipeleke kibabe.
 
Ninachokitaka ni kwamba huyu dogo nae apate kwa niaba ya marehemu mama yake ambae ni dada yangu. Lakini hili swala kama walivyoshauri wadau wengine inabidi nilipeleke kibabe.
Acha uzembe, mwambie haikuhusu tunauza...
 
Fata ushauri wa wadau hapo binti ashauriwe kufungua fixed account ili asizitapanye hizo pesa
 
Fata ushauri wa wadau hapo binti ashauriwe kufungua fixed account ili asizitapanye hizo pesa
Nimemshauri sana lakini nimekuja kugundua kwamba kuna baba yetu mdogo analitaka lile eneo ndo anamshauri yule binti akatae eneo lisiuzwe. Ndo maana nkaona kabla sijalianzisha nijue kwanza kisheria imekaaje
 
Habari.!

Nina kitu kimoja nataka nijue kutoka kwa wenzetu wa sheria.

Kuna kiwanja kipo maeneo ya Tegeta ambacho ni cha baba yetu ambae alishafariki miaka 20 iliyopita, aliacha watoto watatu, wa kiume mmoja ambae ni mimi na wa kike wawili.

Kwa bahati mbaya katika watoto wa kike, mmoja alifariki pia akaacha mtoto mmoja wa kike ambae yupo kidato cha sita. Kila mtoto ana mama yake.

Sasa kiwanja tunakiuza ili kila mmoja apate mgawo wake, sasa changamoto inakuja kwamba huyu mtoto wa dada yetu aliyefariki anapinga kisiuzwe tusubiri mpaka amalize masomo miaka mitano mbele huko.

Sasa je kisheria huyu mjukuu wa baba yetu ana nguvu ya kuzuia sisi tusiuze kiwanja? Maana kiwanja twauza 30m kila mtu atapata 10m. Kisheria imekaaje hii?
Huyo kachanganyikiwa mapema sana.

.........Mwambieni kwa Babu hakuna urithi.
 
Miaka mitano ni mingi aseeeeee!!!

Vipi ikitokea wote wawili mkafa?

Akabaki dogo tu?

Mwisho wa siku siku inakua vita kisa kiwanja cha babu.(halafu kumbuka watakua ni wengi, ila kiwanja kimoja, imaginewamebaki wajukuu tu halafu pakagundulika pana madini)

Epusha matatizo ya baadae mzee

Kiwanja kiuzwe leo leo.
Nani alikwambia ukiwa na kiwanja unamiliki mpaka madini yaliyoko chini ya ardhi? Ukimiliki kiwanja unaishia kuwa mpangaji kwenye ardhi ambayo iko chini ya serikali kwa maana ya Rais. Kwa maana nyingine wewe kwenye ardhi unamiliki ardhi na maotea yaliyoko juu ya ardhi. Chochote kilichopo chini ya ardhi ni mali ya serikali kama huamini chimba kifusi kutoka kwenye kiwanja chako pita nacho barabarani kama haujadaiwa kibali cha machimbo
 
Kutokana na nia nzuri mlio nayo mmshauri afungue fixed account ili hela yake mmuwekee huko. Lakini pia hujaeleza ikiwa huyo mtoto dadako alimuorodhesha popote kama mrithi wa mali zake na kama ndivyo anaweza kuweka zuio kupitia wosia wa mamake na si wa baba yenu.
Tunatumia busara tu lakini dada yetu hakumuorodhesha popote kuhusu urithi wake.
 
Maelezo yako pamoja na comments za wadau wote nilizosoma hapo chini, ukiachana na mambo sijui ya kisheria, zipo sawa na ndizo familia mbali mbali hufuata kugawana mirathi.

Huyo mtoto wa marehemu dada yako hana haki ya urithi wa moja kwa moja hapo.

Mlivyopanga na nduguzo kwamba muuze kisha mgao wa mirathi mumkumbuke na marehrmu ndugu yenu mmefanya jambo jema linalostahili pongezi, hamna tamaa za kijinga.

Kitu ambacho sijaelelewa, huyo mtoto wa marehemu, kazaliwa peke yake kwenye tumbo la marehemu?

Kama kazaliwa na wenzake, pia mgao mtakao mgawia marehemu ndugu yenu, inatakiwa muwagawanye na wenzake sawa kwa sawa.

Zoezi la kuuza liendelee na yote mliyopanga na dada zako yatekelezeni.

Huyo mtoto wa marehemu hana haki yoyote kuwapangia ama kuingilia suala hilo.
Kwa mama yake kazaliwa peke yake tu.
 
Back
Top Bottom