Watu wakimya (introverts) mnapataje marafiki wa kawaida ukubwani?

Watu wakimya (introverts) mnapataje marafiki wa kawaida ukubwani?

Nmepata maana yake 😂 nilimaanisha kuwa kama hao bears namna ulivyotuweka introverts tabia zetu tukiwa public ni tofauti na tukikutana na watu wa aina yetu 😂😂 kenge wee
😂😂 Me nilimaanisha kijapani Sasa🤣
 
Hahahahahahahaha
Kuna wakati natamani simu isiwe na sehemu ya call

I prefer sms kuliko call

Za kazini na wazazi sina ujanja
Kuna kipindi naweka flight mode kabisa

Au nikiwa kazini nasingizia meeting namwambia mtu tuma sms

Baadhi ya ndugu wameshasusa japo tukikutana nao niko social sana na nawapenda mno

Nasingizia kazi ila nachukia simu tu na sijui why nachukia
Nakuelewa vizuri aise...

Kuna muda nachoka simu yani sijisikii kuwasiliana na mtu

Mara nyingi wanaanza kunikumbuka wengine iwe ndugu ama rafiki nimekua mzito kwenye mawasiliano mpaka kuna muda najistukia

Mtu pekee ambae naweza kujitahidi ni mpenzi tena awe ni yule wa caring na yeye otherwise mood inapungua akiwa wa bze sana

Napenda sms zaidi kuliko calls

Japo kuna muda nachangamana fresh but hali hiyo haidumu kwa muda mrefu
 
Kuna muda natamani kujichanganya na kuwa na marafiki nashindwa.

Kila nikijaribu kuingia kwenye ulimwengu wa marafiki nayokutana nayo huko ni unafiki chuki fitan nk. Naamua kujiondoa naona wanayofanya si sahihi

Unakuwa na marafiki ukishapata maendeleo kidogo kuwazidi wao tayar chuki zinaanza yalinishinda
Ukiumwa nitakutembelea ukiwa na shida nitakusaidia

Lakini mazoea siyawezi hujenga chuki
Kama unaenjoy kua mwenyewe fanya hivyo maana ni vibaya sana kua sehemu unayo hisi thamani yako imeshuka au kujihisi vibaya.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Hahahahahahahaha
Kuna wakati natamani simu isiwe na sehemu ya call

I prefer sms kuliko call

Za kazini na wazazi sina ujanja
Kuna kipindi naweka flight mode kabisa

Au nikiwa kazini nasingizia meeting namwambia mtu tuma sms

Baadhi ya ndugu wameshasusa japo tukikutana nao niko social sana na nawapenda mno

Nasingizia kazi ila nachukia simu tu na sijui why nachukia

[emoji16][emoji16][emoji16]kumbe tupo wengi mi nikishasalimiana na mtu au nikikutana na mtu nayejua anamaneno mengi njiamoja kama ajaniona naweza ingia ata uvunguni mwa gari ili tu tusionane akanganzaa salaam nyingi nyingi[emoji16] pia kunatabia ambayo inanitesa zaidi nikiwa kwenye group na mwenyeji wangu yupo alafu story zinapigwa napenda sana kusikiliza na kucheka panapobidi na kuchangia kiasi lakini kimbebe ni pale mwenyeji wangu anapotoka kidogo af nibakie na watu nisio na chemistry nao hua naona ile meza ni kubwa[emoji16] ifeel morecomfortable napokua nawatu wachache tuloshibana atakama ni mmoja.
 
Hulka moja wapo ya watu wakimya (introverts) ni ugumu wa kujichanganya na kuzoeana na watu wapya. Hii inapelekea wengi wanajikuta hawana marafiki ukitoa watu wachache wale waliofahamiana wakati wa chuo/sekondari, biashara/kazini. Siku zinavyosonga na wanavyozidi kukukua kimaisha "cycle" ya marafiki alionao inazidi kupungua. Anabakiwa na zaidi familia tu na rafiki mmoja au wawili.

Anajikuta imefika weekend mtu anatamani kujiachia kidogo na kubadili mawazo ila akiangalia hana watu wa kujumuika nao. Akiingia bar/mgahawa anakuta majamaa wamekaa kwenye meza kwa vikundi, inabidi aidha akae meza yake mwenyewe au akae counter...lakini anakosa ile ladha ya urafiki na uhusiano walionayo wengine kwenye maisha ambapo hubadilishana mawazo na kupeana changamoto chanya za kimaisha.

Kwa upande mwingine wanakuwa ni watu wanaojitegemea (independent) kifikra na kwa mambo mengi hufanya maamuzi na kuendesha maisha bila kutegemea ushauri au mawazo ya wengine. Pia kutokana na kutokuwa na watu wengi huwa hawana zile drama/changamoto za marafiki.

Faida za marafiki ni nyingi kuliko hasara, hebu introverts toeni mbinu za kupata marafiki wapya ukubwani.
Mimi pia ni miongoni mwao ,,ila trick nliotumia kupata marafiki ,,nakumbuka baada ya kuhamia mtaa Fulani nikajiaribu kumtafuta contawar Wa mtaa yani MTU mwenye ushawishi kijiweni nkajizoesha kwake Na yeye ndo akapelekea nkapata marafiki wengi Na connection kupitia yeye ,,, wewe kama unataka kua Na marafiki mtafte MTU ambae unahisi ana ushawishi kwa watu ,,
 
Nimetoka kupata dawa za Impiramine kwenye hospitali moja kubwa hapa DSM.

Sielewi ni Introvert au ni nini. Nina loneliness moja ya kufa hata kufanya majukumu yangu sitaki kabisa. I hope it won't get worse.

I don't want to be an Introvert. It hurts.
Unaendeleaje mkuu sasa hivi?
 
iko hivi nna marafiki kutokana na backgrounds kuna hawa old friends, school mates, colleagues na hata room mates lakini sasa wote wananichukulia kama mtu wao wa karibu sana....kwa kila mmoja na nafasi yake

Ila tatizo mimi nawachukuliq kawaida sina yule best friend mpaka leo ila hao wanadhani mimi ni best friend wao utakuta najua vitu vingi kuhusu wao ila hao wanajua 30% kuhusu mimi!

Hivi hapo ni nn kifupi hamna mtu ntakaefunguka kwake na kujiachia 100% awe mzazi/ mpenzi always naweka guard... sijawahi amini mtu
 
iko hivi nna marafiki kutokana na backgrounds kuna hawa old friends, school mates, colleagues na hata room mates lakini sasa wote wananichukulia kama mtu wao wa karibu sana....kwa kila mmoja na nafasi yake

Ila tatizo mimi nawachukuliq kawaida sina yule best friend mpaka leo ila hao wanadhani mimi ni best friend wao utakuta najua vitu vingi kuhusu wao ila hao wanajua 30% kuhusu mimi!

Hivi hapo ni nn kifupi hamna mtu ntakaefunguka kwake na kujiachia 100% awe mzazi/ mpenzi always naweka guard... sijawahi amini mtu

Wanaume na nyie mnakuaga na so called best friends???
 
Back
Top Bottom